Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Hili ni swali ambalo kila mwanachadema na mpenda demokrasia anatamani leo litendeke kupitia Kamati Kuu. Lakini ipi sababu hasa ya kwanini wafukuzwe? Nini faida kwa CHADEMA ikiwafukuza? Nini hasara kwa CHADEMA ikiwaacha ndani ya Chama?
Tuanze na hili la kwanza, Baada ya kinachoitwa Uchaguzi ambacho sisi CHADEMA hatutambui kama ni Uchaguzi, Chama kilikaa chini na kutotambua chochote kitokanacho na uchaguzi huo. Halima Mdee na genge lake wakiwa ni moja wajumbe katika Kamati Kuu ya Chama iliyokaa na kutotambua uchaguzi huo.
Maazimio ya Chama pamoja na mambo mengine, yalikuja na madai ya msingi makuu matatu, 1. Tume ya Uchaguzi mpya huru na Haki iundwe, 2. Uchaguzi Urudiwe chini ya Tume Huru mpya, 3. Mchakato wa Katiba mpya uendelee pale ilipoishia Tume ya Jaji Warioba.
Ili kuhakikisha madai ya CHADEMA yanaishinikiza serikali ikubali kukaa mezani, CHADEMA ilijenga msingi wa mambo makuu matatu ambayo ndio silaha yake leo na kesho.
1. Ilikuwa ni Kushikilia Viti Maalumua ambavyo kwa namna Bunge lilivyokuwa, lilikosa uhalali wa kuwa Bunge la Vyama vingi. Hii ndio ilikuwa sila kuu kabisa ambayo serikali ilikuwa lazima ihitaji maridhiano na Upinzani, na dalili za serikali kutaka maridhiano na upinzani zilishaanza kuonekana wazi.
2. Jumuiya za Kimataifa kuishinikiza Tanzania kulegeza mbinyo wa demokrasia na kueleza wazi juu ya Uchaguzi ulikuwa Batili. Hili ni silaha kubwa na tayari EU ilishatoa msimamo huo na Uingereza na Marekani zinapiga jalamba.
3. Ni mapokeo ya Umma dhidi ya Chama kabla na Baada ya Matokeo.
Hayo matatu yalikuwa na bado ni silaha muhimu kwa harakati za CHADEMA kuhakikisha haki ya kidemokrasia nchini inapatikana kwa wazi. Halima Mdee yote haya alishiriki na anayajua vema.
Maadui walifeli na wamefeli kwenye kila eneo, hawana pakuanzia wala pakuishia, Sehemu waliyoona itajaribu kuwasitiri ni kujaribu kuwarubuni wanawake hawa kupitia Halima Mdee, Si kwamba Chama hakijui mipango yao yote tangu mwanzo, Kinajua kila kitu ambacho Halima na genge lake walikuwa wakifanya nje ya mfumo wa chama. Amelilia wembe ataupata
Viti maalumu deadline ni bunge la Mwezi wa nne, Naomba kurudia kusisitiza, Viti Maalumu Deadline ni bunge la mwezi wa Nne. Chama kinajua kucheza karata hii si vile Mdee na wenzake wanavyotaka kuaminisha umma. Halima kama Mwenyekiti wa BAWACHA anajua jambo hili kuwa Chama kilikuwa na mkakati gani na Chama ndio msimamizi wa Mabaraza yote.
Sasa katika tafsiri ya vita, Mtu anayeasi mapambano kama Mdee na kuungana na watesi na kuahidiwa kulindwa daima, unamsameheje abaki kwenye Chama? Labda hicho chama kinamalengo ya kwenda waliko CUF, TLP, NCCR nk. Lakini kama kinataka kuendelea kuaminika kwa UMMA ni lazima kiondokane na watu wa aina hii.
Faida ya Kwanza wakifukuzwa ni kwamba Watakosa uhalali wa kisheria kuwa wabunge wanaowakilisha CHADEMA Bungeni hata wakilindwa na Serikali. Pili Jumuiya za Kimataifa bado zitaendelea kutotambua bunge kuwa ni la vyama vingi kwakuwa Chama Kikuu cha Upinzania hakina Mbunge yoyote Bungeni. Madai ya Upinzani mbele ya Jumuiya za kimataifa yataendelea kuwa halali na yenye nfuvu. Kwahiyo ile mishemishe ya dola kujaribu kubumba upinzani feki Bungeni itakuwa imeingia luba.
Hasara kubwa kwa CHADEMA ikiwaacha, itapoteza uaminifu kwa umma wa mamilioni ya Wapenda denokrasia duniani, Pili Jumuiya za kimataifa zitakiona kama chama kisichoaminika mbele ya Watanzania na kwamba malalamiko yote ya Chama mbele ya Jumuiya za Kimataifa yatakosa uhalali. Na tatu, sasa Dola itakuwa haina tena hata wazo tu la kusukumwa kusikiliza madai ya upinzani juu ya Tume huru ya Uchaguzi, Katiba Mpya nk.
Halima Mdee na genge lake wana machaguo mawili tu, 1. Ni kujivua Ubunge na kubaki na Chama, 2. Ni kubaki na Ubunge na kwenda kwa dola. Uchaguzi ni wao... Kamati Kuu inawasubiri waamue nayo iamue... Wananchi wameshaamua.
Ikiwa Mdee na wenzake watachagua chaguo la pili, Chama kichague moja kubaki imara kwakuondoa wahuni hawa, au Kife kifo chepesi kwa kukubaliana na vurugu za Dola.
Ok, Usikose Kusoma VITABU hivi:
1. Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Bei ni 80,000/= (Kitabu Maalumu kwa wafanyamaamumzi/waliopevuka kiakili)
2. Strategy: The Road to Power, Bei ni 1,700,000/= (Kitabu Maalumu kwa wagombea Ubunge na Urais)
3. Mapambano ya Madaraka, bei ni 30,000/= (Kitabu Maalumu kwa Wagombea uenyeviti Mitaa/vijiji, Udiwani na watu wote)
4. Mtu baada ya Mtu, Bei ni 80,000/= (Kitabu kwaajili ya wote). KIKO MITAMBONI.
Nunua kwa:
TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)
Tuma majina yako na ulipo
(Dar ni free delivery)
Nje ya Dar nauli 8,000/=
Instagram Follow @yerickonyerere_
Tuanze na hili la kwanza, Baada ya kinachoitwa Uchaguzi ambacho sisi CHADEMA hatutambui kama ni Uchaguzi, Chama kilikaa chini na kutotambua chochote kitokanacho na uchaguzi huo. Halima Mdee na genge lake wakiwa ni moja wajumbe katika Kamati Kuu ya Chama iliyokaa na kutotambua uchaguzi huo.
Maazimio ya Chama pamoja na mambo mengine, yalikuja na madai ya msingi makuu matatu, 1. Tume ya Uchaguzi mpya huru na Haki iundwe, 2. Uchaguzi Urudiwe chini ya Tume Huru mpya, 3. Mchakato wa Katiba mpya uendelee pale ilipoishia Tume ya Jaji Warioba.
Ili kuhakikisha madai ya CHADEMA yanaishinikiza serikali ikubali kukaa mezani, CHADEMA ilijenga msingi wa mambo makuu matatu ambayo ndio silaha yake leo na kesho.
1. Ilikuwa ni Kushikilia Viti Maalumua ambavyo kwa namna Bunge lilivyokuwa, lilikosa uhalali wa kuwa Bunge la Vyama vingi. Hii ndio ilikuwa sila kuu kabisa ambayo serikali ilikuwa lazima ihitaji maridhiano na Upinzani, na dalili za serikali kutaka maridhiano na upinzani zilishaanza kuonekana wazi.
2. Jumuiya za Kimataifa kuishinikiza Tanzania kulegeza mbinyo wa demokrasia na kueleza wazi juu ya Uchaguzi ulikuwa Batili. Hili ni silaha kubwa na tayari EU ilishatoa msimamo huo na Uingereza na Marekani zinapiga jalamba.
3. Ni mapokeo ya Umma dhidi ya Chama kabla na Baada ya Matokeo.
Hayo matatu yalikuwa na bado ni silaha muhimu kwa harakati za CHADEMA kuhakikisha haki ya kidemokrasia nchini inapatikana kwa wazi. Halima Mdee yote haya alishiriki na anayajua vema.
Maadui walifeli na wamefeli kwenye kila eneo, hawana pakuanzia wala pakuishia, Sehemu waliyoona itajaribu kuwasitiri ni kujaribu kuwarubuni wanawake hawa kupitia Halima Mdee, Si kwamba Chama hakijui mipango yao yote tangu mwanzo, Kinajua kila kitu ambacho Halima na genge lake walikuwa wakifanya nje ya mfumo wa chama. Amelilia wembe ataupata
Viti maalumu deadline ni bunge la Mwezi wa nne, Naomba kurudia kusisitiza, Viti Maalumu Deadline ni bunge la mwezi wa Nne. Chama kinajua kucheza karata hii si vile Mdee na wenzake wanavyotaka kuaminisha umma. Halima kama Mwenyekiti wa BAWACHA anajua jambo hili kuwa Chama kilikuwa na mkakati gani na Chama ndio msimamizi wa Mabaraza yote.
Sasa katika tafsiri ya vita, Mtu anayeasi mapambano kama Mdee na kuungana na watesi na kuahidiwa kulindwa daima, unamsameheje abaki kwenye Chama? Labda hicho chama kinamalengo ya kwenda waliko CUF, TLP, NCCR nk. Lakini kama kinataka kuendelea kuaminika kwa UMMA ni lazima kiondokane na watu wa aina hii.
Faida ya Kwanza wakifukuzwa ni kwamba Watakosa uhalali wa kisheria kuwa wabunge wanaowakilisha CHADEMA Bungeni hata wakilindwa na Serikali. Pili Jumuiya za Kimataifa bado zitaendelea kutotambua bunge kuwa ni la vyama vingi kwakuwa Chama Kikuu cha Upinzania hakina Mbunge yoyote Bungeni. Madai ya Upinzani mbele ya Jumuiya za kimataifa yataendelea kuwa halali na yenye nfuvu. Kwahiyo ile mishemishe ya dola kujaribu kubumba upinzani feki Bungeni itakuwa imeingia luba.
Hasara kubwa kwa CHADEMA ikiwaacha, itapoteza uaminifu kwa umma wa mamilioni ya Wapenda denokrasia duniani, Pili Jumuiya za kimataifa zitakiona kama chama kisichoaminika mbele ya Watanzania na kwamba malalamiko yote ya Chama mbele ya Jumuiya za Kimataifa yatakosa uhalali. Na tatu, sasa Dola itakuwa haina tena hata wazo tu la kusukumwa kusikiliza madai ya upinzani juu ya Tume huru ya Uchaguzi, Katiba Mpya nk.
Halima Mdee na genge lake wana machaguo mawili tu, 1. Ni kujivua Ubunge na kubaki na Chama, 2. Ni kubaki na Ubunge na kwenda kwa dola. Uchaguzi ni wao... Kamati Kuu inawasubiri waamue nayo iamue... Wananchi wameshaamua.
Ikiwa Mdee na wenzake watachagua chaguo la pili, Chama kichague moja kubaki imara kwakuondoa wahuni hawa, au Kife kifo chepesi kwa kukubaliana na vurugu za Dola.
Ok, Usikose Kusoma VITABU hivi:
1. Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Bei ni 80,000/= (Kitabu Maalumu kwa wafanyamaamumzi/waliopevuka kiakili)
2. Strategy: The Road to Power, Bei ni 1,700,000/= (Kitabu Maalumu kwa wagombea Ubunge na Urais)
3. Mapambano ya Madaraka, bei ni 30,000/= (Kitabu Maalumu kwa Wagombea uenyeviti Mitaa/vijiji, Udiwani na watu wote)
4. Mtu baada ya Mtu, Bei ni 80,000/= (Kitabu kwaajili ya wote). KIKO MITAMBONI.
Nunua kwa:
TigoPesa 0715865544
M-Pesa 0755865544
Airtel Money 0788887887
HaloPesa 0624452045
(Yericko Nyerere)
Tuma majina yako na ulipo
(Dar ni free delivery)
Nje ya Dar nauli 8,000/=
Instagram Follow @yerickonyerere_