Ni ushawahi kushuhudia jeuri ya pesa

Ni ushawahi kushuhudia jeuri ya pesa

mr pipa

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2021
Posts
3,513
Reaction score
7,499
Baada ya safar ndefu na kuona sasa unaingia usiku, nikawa nimepitia mji mmoja hivi nichukue chumba nilale kiufupi nilipata.

Majira ya saa nne usiku akaja jamaa mmoja kuuliza chumba akajibiwa vimeisha kilichofanyika jamaa akamwambia muhudumu anahitaji awatoe wateja wote alafu yeye alipie mara tatu ya tulio lipia.

Punde si punde muhudumu akatugongea wateja tuamke tukatafute guest house nyingine tukarudishiwa pesa zetu na buku tano ya nyongeza kilichofuata jamaa alikusanya magodoro yote akajaza chumba kimoja akayalalia.

Dah kuja kusikia taarifa za jamaa asubuhi kumbe ni mchimba madini kaotea huko asee nililaani sana kile kitendo
 
Na hizo jeuri maranyingi zinatokeaga maeneo ya migodini...
Kipindi flani nilikua igodima-chunya,nimeingia bar nipate mbili nichukue na mlupo nikalale...kuna dogo alikuja pale kaunta akazuia kaunta yote halafu akasema bar yote tutoke nje anataka kuoshea gari mle ndani ya bar...halafu inaoshewa pombe za kaunta na yoyote atakae jitolea kuosha ndiye atakae baki ndani na atalipwa 150k...
Lakn maajabu tulibaki wawili tu mimi yeye na wahudumu,kumbe waliowengi walikua maponcha wa migodin hawakutaka dharau....
Na ndio mara ya kwanza kupiga 3some kwa gharama za msandawe yule
 
Mimi napenda sana wali dagaa. Siku moja nikaenda mgahawani, kuagiza wali dagaa yule mhudumu akanijibu dagaa wanauzwa na ugali tu. Nikamwomba anisaidie tu, akanijibu kama huna hela anipe wali maharage. Nikaona nijibu mapigo.

Nikamwambia anipe ugali na dagaa na wali ili nipate dagaa, alipoleta nikamwambia katupe ugali jalalani. Akiwa anajiona fala nikamwambia naomba kulipa bills za wote wanaokula muda huu. Kulikuwa na wateja kama sita hivi. Ikanitoka kama 53k hivi kulinda heshima ya JF
 
Mimi napenda sana wali dagaa. Siku moja nikaenda mgahawani, kuagiza wali dagaa yule mhudumu akanijibu dagaa wanauzwa na ugali tu. Nikamwomba anisaidie tu, akanijibu kama huna hela anipe wali maharage. Nakaona nijibu mapigo.

Nikamwambia anipe ugali na dagaa na wali ili nipate dagaa, alipoleta nikamwambia katupe ugali jalalani. Akiwa anajiona fala nikamwambia naomba kulipa bills za wote wanaokula muda huu. Kulikuwa na wateja kama sita hivi. Ikanitoka kama 53k hivi kulinda heshima ya JF
Unaringa sana wewe jamaa
 
Ilikuwa weekend Moja tupo bar tunapiga beer 🍺 lager na washikaji,
Basi punde si punde akaingia dogo akiwa na wenzake kama wanne wakanunua vinywaji vya bei kali kama Hennessy wakafungua wakanywa kidogo Wakaacha hapo
Madogo wakaletewa bill ikasoma kama milion 4 wakalipa wakaondoka yani kama hakuna kilichotokea
 
Mimi napenda sana wali dagaa. Siku moja nikaenda mgahawani, kuagiza wali dagaa yule mhudumu akanijibu dagaa wanauzwa na ugali tu. Nikamwomba anisaidie tu, akanijibu kama huna hela anipe wali maharage. Nakaona nijibu mapigo.

Nikamwambia anipe ugali na dagaa na wali ili nipate dagaa, alipoleta nikamwambia katupe ugali jalalani. Akiwa anajiona fala nikamwambia naomba kulipa bills za wote wanaokula muda huu. Kulikuwa na wateja kama sita hivi. Ikanitoka kama 53k hivi kulinda heshima ya JF
Kihasibu hio imekaaje
 
Ngoja nisubscribe huu uzi.
Siku nikijisikia kunywa chai naingia najichotea.
Screenshot_20251111-181333~2.jpg
 
Kuna njema mwaka jana imetoka zake migodin imefika stend alikuwa akielekea mbinga to njombe anafika stend kakuta bus imejaa alichokifanya akaenda kwenye ofic husika ya mabus akaodi gari tatu ya nyuma akaweka beg ya mbele kofia yakamsindiza hadi huko nyumban kwake sehem ya kulipa elfu 20 alitumia milion mbil na upuuz tembea ujionee
 
Back
Top Bottom