Ni sahihi kuchimba kisima maji kipindi cha masika?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Ni sahihi kuchimba kisima cha maji kipindi cha mvua?

Sikuwa na mpango wa kukichimba muda huu, lakini mtu anayelihudumia shamba langu kwa sasa kaniambia anaweza kukichimba kwa bei nafuu hadi ayakute maji. Nilipomwambia kuwa visima vianvyochimbwa nyakati za mvua zinaweza kuishiwa maji wakati wa kiangazi, kajibu kuwa hilo likitokea, atakifukua tena hadi ayakute maji.

Kwa wenye uzoefu, nini ushauri wenu?
1. Ni kweli kuwa kisima kichimbwacho kwa mikono nyakati za mvua zina uwezekano wa kuishiwa maji wakati wa kiangazi?

2. Ikiwa kisima kitakaukiwa maji wakati wa kiangazi, kuna uwezekano wa kupata maji endapo kitafukuliwa zaidi kwenda chini?

Asanteni🙏🙏🙏
 
Ni sahihi kuchimba kisima cha maji kipindi cha mvua?

Sikuwa na mpango wa kukichimba muda huu, lakini mtu anayelihudumia shamba langu kwa sasa kaniambia anaweza kukichimba kwa bei nafuu hadi ayakute maji. Nilipomwambia kuwa visima vianvyochimbwa nyakati za mvua zinaweza kuishiwa maji wakati wa kiangazi, kajibu kuwa hilo likitokea, atakifukua tena hadi ayakute maji.

Kwa wenye uzoefu, nini ushauri wenu?
1. Ni kweli kuwa kisima kichimbwacho kwa mikono nyakati za mvua zina uwezekano wa kuishiwa maji wakati wa kiangazi?

2. Ikiwa kisima kitakaukiwa maji wakati wa kiangazi, kuna uwezekano wa kupata maji endapo kitafukuliwa zaidi kwenda chini?

Asanteni🙏🙏🙏
Mkuu si vema kuchimba kisima kipindi cha masika( kipindi cha mvua)
SABABU:
1. Ni rahisi kisima kuangukia na kuleta madhara au kuharibu utaratibu wa uchimbaji.
2.Si rahisi kujua kina halisi ulipo mkondo wa maji mengi yasiyo kaka kwasababu kipindi cha mvua maji hupanda juu na kukutana na ya mvua yanayo kwenda chini l hivyo pakichimbwa kidogo tu maji hutoka mengi mnoo lakini haya dumu, hupungua, hukauka au huisha.
 
Mkuu si vema kuchimba kisima kipindi cha masika( kipindi cha mvua)
SABABU:
1. Ni rahisi kisima kuangukia na kuleta madhara au kuharibu utaratibu wa uchimbaji.
2.Si rahisi kujua kina halisi ulipo mkondo wa maji mengi yasiyo kaka kwasababu kipindi cha mvua maji hupanda juu na kukutana na ya mvua yanayo kwenda chini l hivyo pakichimbwa kidogo tu maji hutoka mengi mnoo lakini haya dumu, hupungua, hukauka au huisha.
🙏🙏🙏
 
Mwambie akuchimbie futi 60 , muelewane kwa futi atakapoyakuta maji mengi kabla ya hizo futi .

Kipindi cha kiangazi anamalizia, mm nilichimba futi 60, kipindi cha kiangazi nilipata maji yaliyokuwa yakinitosheleza.
Kaniambia atachimba kwa sh 2,500/= kwa futi.

Kwa ukanda huu, si rahisi kuvuka mita 30 kabla ya kukuta maji. Hofu yangu ni kuwa endapo atayakuta maji wakati huu wa mvua, tuseme kwenye umbali wa futi 20, yakikauka kipindi cha kiangazi itawezekana kuchimba tena kwa kuongezea urefu hadi kuyakuta maji? Huo tu ndiyo wasiwasi wangu. Kama itawezekana, nitamruhusu hasa ikizingatiwa kuwa bei yake ni rahisi sana.
 
Kuchimba kisima wakati wa masika ni jambo zuri sanaaa kwa sababu maji hushuka chini zaidi kiasi kwamba ukiona kayakuta maji hata pipa 3, msimu wa kiangazi ujue pana lita zaidi ya elf2 wakati maji yamepanda juu.

Niamini mimi kiongozi mpe kazi kijana na advance kabisa j3 ni XMass.
 
Kaniambia atachimba kwa sh 2,500/= kwa futi.

Kwa ukanda huu, si rahisi kuvuka mita 30 kabla ya kukuta maji. Hofu yangu ni kuwa endapo atayakuta maji wakati huu wa mvua, tuseme kwenye umbali wa futi 20, yakikauka kipindi cha kiangazi itawezekana kuchimba tena kwa kuongezea urefu hadi kuyakuta maji? Huo tu ndiyo wasiwasi wangu. Kama itawezekana, nitamruhusu hasa ikizingatiwa kuwa bei yake ni rahisi sana.
Kwa bei hiyo ni rahisi sana, lkn je eneo ulilopo na mazingira yake hali ya maji ikoje?
Yaani ni Kame au ina maji mengi? Je ww uko kwenye muinuko au bondeni?

Kama upo eneo tambarare basi jitahidi kuchimba eneo ambalo kama kuna BONDE .
 
Kuchimba kisima wakati wa masika ni jambo zuri sanaaa kwa sababu maji hushuka chini zaidi kiasi kwamba ukiona kayakuta maji hata pipa 3, msimu wa kiangazi ujue pana lita zaidi ya elf2 wakati maji yamepanda juu.

Niamini mimi kiongozi mpe kazi kijana na advance kabisa j3 ni XMass.
Mkuu, ni kweli hayo? Mbona inasemekana maji hushuka chini zaidi kipindi cha kiangazi na kupanda nyakati za mvua? Au umeuwasilisha ujumbe kwa "code" mkuu?
 
Kwa bei hiyo ni rahisi sana, lkn je eneo ulilopo na mazingira yake hali ya maji ikoje?
Yaani ni Kame au ina maji mengi? Je ww uko kwenye muinuko au bondeni?

Kama upo eneo tambarare basi jitahidi kuchimba eneo ambalo kama kuna BONDE .
Kaniambia anaweza kuchimba hata futi 150. Na kwa eneo shamba lilipo, sidhani kama ataenda zaidi ya futi 30 bila kukutana na maji.
 
Ni sahihi kuchimba kisima cha maji kipindi cha mvua?

Sikuwa na mpango wa kukichimba muda huu, lakini mtu anayelihudumia shamba langu kwa sasa kaniambia anaweza kukichimba kwa bei nafuu hadi ayakute maji. Nilipomwambia kuwa visima vianvyochimbwa nyakati za mvua zinaweza kuishiwa maji wakati wa kiangazi, kajibu kuwa hilo likitokea, atakifukua tena hadi ayakute maji.

Kwa wenye uzoefu, nini ushauri wenu?
1. Ni kweli kuwa kisima kichimbwacho kwa mikono nyakati za mvua zina uwezekano wa kuishiwa maji wakati wa kiangazi?

2. Ikiwa kisima kitakaukiwa maji wakati wa kiangazi, kuna uwezekano wa kupata maji endapo kitafukuliwa zaidi kwenda chini?

Asanteni🙏🙏🙏
Achana na mambo ya visima. Chukua pesa mwagilia moyo
 
Achana na mambo ya visima. Chukua pesa mwagilia moyo
Kuna shida mkuu kuchimba kisima?

Wahudumu wa shamba wameshauri kuchimba kisima baada ya kuona shamba linahitaji kisima. Na aliyetoa huo ushauri ndiye anayetaka kuchimba kwa bei nafuu kwa kuwa naye ni mmoja wa wahudumu wa shamba, na hela itakayotumika haitoki kwenye matumizi yangu binafsi bali ya shamba.

Kuna shida kwa shamba kujichimbia kisima chake kwa gharama zake?
 
Kaniambia anaweza kuchimba hata futi 150. Na kwa eneo shamba lilipo, sidhani kama ataenda zaidi ya futi 30 bila kukutana na maji.
Futi 250 !!!? Hiyo hapana, chukulia futi 40 ni sawa na mlingoti wa umeme au container lile kubwa .

Sasa pima kwenda chini, kwa jinsi walivyochimba kwangu na uzoefu nilioupata uwezekano wa kawaida kuchimba bila kuhitaji nyongeza ya HEWA ni futi 80.
 
Mkuu una kibali cha kuchimbiwa kisima kwasababu above 14 mita unatakiwa uwe na kibali ambacho unatakiwa ukipate kutoka kwenye ofisi za bonde zenye mamlaka hayo otherwise unatafuta kesi.
Sidhani kama maji yatakuwa chini sana zaidi ya futi thelathini ardhini.
 
Back
Top Bottom