Ni nini upya wa Katiba Mpya?

Zed

JF-Expert Member
Mar 28, 2009
434
252
Hili ni swali ambalo wananchi wanajiuliza ingawa sio kwa maneno hayo au muktasari kama lilivyo hapo juu. Wananchi wanajiuliza swali kwa maneno kama: je katiba mpya itaniletea chakula au itaondoa dhuluma, itanisadia kutumia rasilimali zangu vema? itathamini kura yangu na kuyafaa maisha yangu?

Majibu ya wanasiasa na wanaharakati wa vuguvugu la katiba mpya nayo pia hayatofautiani sana na maswali ya wananchi; wao wanayo ndoto katiba ya mfumo ule ule huku wakitegemea uwazi na uwajibika zaidi, haki zaidi sheria zaidi kupunguza nguvu za rais nk ila kwa namna gani mfumo huo utahakikishia haya hilo halibainishwi. Katiba mpya ni uhakika wa kuchaguliwa kwao kwa bunge lile lile kwa kutumia "tume huru".

Upya katika katiba mpya upo katika neno moja tu „UGATUZI“ (Devolution) „mfumo wa uwakilishaji madaraka na ugavi wa matumizi ya rasilimali kutoka serikali kuu kwenda kwa uongozi wa magatuzi au serikali za majimbo, mkoa au mitaa“ kwa namna hii ni kuwarudishia wananchi uhuru na madaraka ya kujiamulia mambo yao wenyewe kwa mstakabali na rasilimali zao na vizazi vijavyo (ambayo ndio maana demokrasia). Jambo ambalo liliporwa na wakoloni na baadae serikali baada ya ukoloni na baadae hawakuona umuhimu wa kuwarudishia wananchi hayo, hivyo wakawa wakoloni weusi.

Historia ya nchi yetu tangu ukoloni na haswa baada ya ukoloni umejenga hofu kubwa kwa jambo hili la Ugatuzi. Ikiwa ni janjanja ya kubakiza madaraka kwa wakoloni weusi ingawa Mlw Julius Nyerere 1972 alijaribu kwa tahadhari sana huku akiilinda siasa yake changa wakati huo ya ujamaa na kujitegemea kwa kuleta ugatuzi akiuta „Madaraka Mikoani“ Ila uwoga hakuitekeleza azma hiyo. Mfumo wa uteuzi wa viongozi Kama maRC na MaDC uliendelea kubaki badala ya uchaguzi

Nchi zilizo na maendeleo ya kweli nyingi ni zile zilizofanya ugatuzi: Marekani, Ujerumani, Kanada, India, Singerpore, Gabon, Austria, Malaysia, Brazil na Kenya ambayo tangu ianze kutumia mfumo huo Demokrasia yake inakua na uchumi unaanza kufanya mabadiliko majimboni na mashinani.

Ikiwa Tanzania inataka maendeleo yenye kubadisha Maisha ya watu hainabudi kutengeneza KATIBA MPYA itakayozingatia na kufanya UGATUZI.

NB Uchangiaji wa Kichuguu upo Off-point!
 
Mnazungumziaga Maendeleo ya nchi kama Marekani halafu mnataka copy and paste Kwa Tanzania. ..
Marekani utajiri unamilikiwa na asilimia moja Tu ya population..
Wamarekani Hadi Leo wanalia na mifumo kama electrol college n.k...
Media zina influence Sana .kuna bado wale madalali wanaitwa lobbyists ambao ndo wanaamua Nani awe senetors au Rais na policy ipi ipite ipi ikwame n.k....

Mtakuja kudanganya watu waingie mkenge washindwe kutoka tupeleke nchi kwenye madalali..
Katiba mpya Haina maana kama majority ya population ni ignorant na poor .. watauzwa mchana kweupe
 
Hakuna mfumo utakuwa perfect 100% kila siku tutakuwa na Kazi ya kuuboresha ila ugatuzi utayapeleka maamuzi ya maisha ya watu kwa watu na context yao zaidi.
Mnazungumziaga Maendeleo ya nchi kama Marekani halafu mnataka copy and paste Kwa Tanzania. ..
Marekani utajiri unamilikiwa na asilimia moja Tu ya population..
Wamarekani Hadi Leo wanalia na mifumo kama electrol college n.k...
Media zina influence Sana .kuna bado wale madalali wanaitwa lobbyists ambao ndo wanaamua Nani awe senetors au Rais na policy ipi ipite ipi ikwame n.k....

Mtakuja kudanganya watu waingie mkenge washindwe kutoka tupeleke nchi kwenye madalali..
Katiba mpya Haina maana kama majority ya population ni ignorant na poor .. watauzwa mchana kweupe
 
Katiba ya Tanzania haikuandikwa vizuri, ina makosa mengi sana ambayo yanaweza kucost nchi. Kwa mfano Katiba ina kifungu kinachosema CAG ataendelea kuwa ofisini hadi afikisha umri wa kustaafu sijui miaka 65; ni kifungu kimeandikwa kimakosa na mwandishi hakuwa na maana hiyo, lakini sasa kiko ndani ya Katiba na tumeona juzi kimetumika vibaya. Kuna haja ya kunyoosha lugha iliyotumika ndani ya katiba

Pili muundo wa serikali kikatiba pia uko skewed sana kwa kumwachia Rais madaraka mengi mno. Rais anaweza kuyatumia madaraka hayo kwa manufaa ya umma au kwa manufaa ya watu wake tu; kwa mfano katiba inampa raisi mamlaka ya kuteuwa watu wengi sana bila kuingiliwa; hivyo anaweza kuteua watu wa Sukuma Gang tu, au watu wa Msoga connection tu bila kuulizwa lolote. Kuna haja ya kumpunguzia madaraka kwa mfano kutaka mawaziri na wakuu wa mikoa wote wathibitishwe na bunge, na pia bunge liwe na mamlaka ya kuwafukuza. Halafu wakuu wa wilaya ama wafutwe au wachaguliwe na wananchi huko huko wilayani kwao.

Tatu Kwenye Uchaguzi wa Rais, Katiba imetoa madaraka makubwa sana kwa Tume ya uchaguzi kuwa ikishatamka rais mteule basi tangazo lao haliwezi kupingwa au kutenguliwa na mahakama yoyote na inabidi mteule huyu aapishwe mara moja. Hilo ni kosa.

Kuna mambo kadhaa ambayo Katiba ya sasa ina mapungufu. Lakini Katiba mpya siyo kuwa itafanya CHADEMA au CUF au ACT washinde uchaguzi. Hivyo ni vyama vya kibabaishaji sana ambavyo vimeonyesha kutokuwa na msimamo wa kisiasa. Wamekuwa wanatumia Katiba kama kisingizio cha kushindwa huku vyama vya wenzao kama Kenya, Zambia na Malawi vilishinda bila katiba mpya.
 
Hapana, mimi ndiyo nimetoka kazini sasa nasubiri kupata dinner. Dunia ni mduara; wewe unapokuwa umelala, wengine wanakuwa maofisini wanafanya kazi.

GettyImages-1137035544-88df2b9-scaled.jpg
 
Wananchi % kubwa hawajui umuhimu wa Katiba Mpya hata hii iliyopo hawaelewi so Mimi naomba Serikali itenge fungu la kuwapa watu MAARIFA waelewe hata maana ya katiba Mpya
 
Wananchi % kubwa hawajui umuhimu wa Katiba Mpya hata hii iliyopo hawaelewi so Mimi naomba Serikali itenge fungu la kuwapa watu MAARIFA waelewe hata maana ya katiba Mpya
Wananchi walishatoa maoni yao yapo kwenye rasimu ya Warioba. Kwa kuwa inawabana watawala wanataka kuichakachua ikidhi matakwa yao. Hakuna haja kuanza upya ni matimizi mabaya ya rasilmali zetu. Watayapinga Tena maoni yetu na hela italiwa lakini hakutakuwa na jipya. Danadana itaendelea, wataendelea kujimegea keki ya taifa na maisha yaendelea kama jana.
 
Katiba ya Tanzania haikuandikwa vizuri, ina makosa mengi sana ambayo yanaweza kucost nchi. Kwa mfano Katiba ina kifungu kinachosema CAG ataendelea kuwa ofisini hadi afikisha umri wa kustaafu sijui miaka 65; ni kifungu kimeandikwa kimakosa na mwandishi hakuwa na maana hiyo, lakini sasa kiko ndani ya Katiba na tumeona juzi kimetumika vibaya. Kuna haja ya kunyoosha lugha iliyotumika ndani ya katiba

Pili muundo wa serikali kikatiba pia uko skewed sana kwa kumwachia Rais madaraka mengi mno. Rais anaweza kuyatumia madaraka hayo kwa manufaa ya umma au kwa manufaa ya watu wake tu; kwa mfano katiba inampa raisi mamlaka ya kuteuwa watu wengi sana bila kuingiliwa; hivyo anaweza kuteua watu wa Sukuma Gang tu, au watu wa Msoga connection tu bila kuulizwa lolote. Kuna haja ya kumpunguzia madaraka kwa mfano kutaka mawaziri na wakuu wa mikoa wote wathibitishwe na bunge, na pia bunge liwe na mamlaka ya kuwafukuza. Halafu wakuu wa wilaya ama wafutwe au wachaguliwe na wananchi huko huko wilayani kwao.

Tatu Kwenye Uchaguzi wa Rais, Katiba imetoa madaraka makubwa sana kwa Tume ya uchaguzi kuwa ikishatamka rais mteule basi tangazo lao haliwezi kupingwa au kutenguliwa na mahakama yoyote na inabidi mteule huyu aapishwe mara moja. Hilo ni kosa.

Kuna mambo kadhaa ambayo Katiba ya sasa ina mapungufu. Lakini Katiba mpya siyo kuwa itafanya CHADEMA au CUF au ACT washinde uchaguzi.
Hivyo ni vyama vya kibabaishaji sana ambavyo vimeonyesha kutokuwa na msimamo wa kisiasa. Wamekuwa wanatumia Katiba kama kisingizio cha kushindwa huku vyama vya wenzao kama Kenya, Zambia na Malawi vilishinda bila katiba mpya.
Hapa nilipoweka bold ndo Kwenye nyama. Hao chadema wanataka wawe na muda wa kupinga pinga matokeo kupotezeana tu muda.

Huo uhuru kautumia hata raila kaishia wapi kila siku anapinga matokeo tu anaamini wakenya wote wanamtaka
 
Katiba ya Tanzania haikuandikwa vizuri, ina makosa mengi sana ambayo yanaweza kucost nchi. Kwa mfano Katiba ina kifungu kinachosema CAG ataendelea kuwa ofisini hadi afikisha umri wa kustaafu sijui miaka 65; ni kifungu kimeandikwa kimakosa na mwandishi hakuwa na maana hiyo, lakini sasa kiko ndani ya Katiba na tumeona juzi kimetumika vibaya. Kuna haja ya kunyoosha lugha iliyotumika ndani ya katiba

Pili muundo wa serikali kikatiba pia uko skewed sana kwa kumwachia Rais madaraka mengi mno. Rais anaweza kuyatumia madaraka hayo kwa manufaa ya umma au kwa manufaa ya watu wake tu; kwa mfano katiba inampa raisi mamlaka ya kuteuwa watu wengi sana bila kuingiliwa; hivyo anaweza kuteua watu wa Sukuma Gang tu, au watu wa Msoga connection tu bila kuulizwa lolote. Kuna haja ya kumpunguzia madaraka kwa mfano kutaka mawaziri na wakuu wa mikoa wote wathibitishwe na bunge, na pia bunge liwe na mamlaka ya kuwafukuza. Halafu wakuu wa wilaya ama wafutwe au wachaguliwe na wananchi huko huko wilayani kwao.

Tatu Kwenye Uchaguzi wa Rais, Katiba imetoa madaraka makubwa sana kwa Tume ya uchaguzi kuwa ikishatamka rais mteule basi tangazo lao haliwezi kupingwa au kutenguliwa na mahakama yoyote na inabidi mteule huyu aapishwe mara moja. Hilo ni kosa.

Kuna mambo kadhaa ambayo Katiba ya sasa ina mapungufu. Lakini Katiba mpya siyo kuwa itafanya CHADEMA au CUF au ACT washinde uchaguzi. Hivyo ni vyama vya kibabaishaji sana ambavyo vimeonyesha kutokuwa na msimamo wa kisiasa. Wamekuwa wanatumia Katiba kama kisingizio cha kushindwa huku vyama vya wenzao kama Kenya, Zambia na Malawi vilishinda bila katiba mpya.

Mbona unajicontradict?. Unasema katiba imeipa mamlaka makubwa NEC kwenye uchaguzi wa Rais halafu unasema kuwa vya vya Upinzani haviwezi kushinda. Tupunguze unafiki, Mwaka 2015 Rais alishinda kwa kura asilimia 57 Ina maana alivuka asilimia 7 tu, mwaka 2020 uchaguzi ukaharibiwa kwa wapinzani kuenguliwa na ujinga mwingi, Sasa unawalaumuje wapinzani kwamba hawawezi kushinda ilihali Tume ipo upande wa CCM ?.

Kwa Tanzania hali ni tofauti na Kenya, Zambia na Malawi. Kwa Tanzania CCM imejimilikisha nchi na ipo tayari kuua watu ili iendelee kukamata dola. Mwaka 2015 uchaguzi Zanzibar ulifutwa baada ya CUF kushinda, jeshi likatumwa Zanzibar. Sasa wewe Baki unalaumu wapinzani wakati CCM wamekula yamini kuwa hawataaachia madaraka .
 
Hapa nilipoweka bold ndo Kwenye nyama. Hao chadema wanataka wawe na muda wa kupinga pinga matokeo kupotezeana tu muda.

Huo uhuru kautumia hata raila kaishia wapi kila siku anapinga matokeo tu anaamini wakenya wote wanamtaka

Tatizo lako unaiangalia katiba kwa jicho la CHADEMA ukidhani CHADEMA itakuwepo miaka yote, ukijadili katiba angalia vizazi vijavyo, maana unachokidharau Leo utakuja kukihitaji kesho. Jadili katiba kwa kuangalia manufaa sio CHADEMA.

Kuhusu Kenya, uchaguzi ulikuwa mgumu, waliachana kwa tofauti ya kura laki mbili, Sasa kura laki mbili ni eneo moja la bungoma huko magharibi ndio zilimpatia Ruto ushindi, Sasa unaweza kudispute hizo kura na Uchaguzi ukaenguliwa. Kenya wapo mbali usimuangilie odinga, Kuna vizazi vinakuja vitahitaji kupinga matokeo wakati odinga hayupo.

Nakushauri, unapojadili suala la Katiba usiingize vyama au personalities utaharibu, Bali angalia mambo ya manufaa yanayohitajoka kwenye katiba. Kwa mfano katiba yetu Ina mahakama ya katiba Constitutional Court, lakini hiyo mahakama haijawahi kufanya kazi kwa sababu haitoi locus standi na procedures za kufungua mashauri kwenye hiyo mahakama. Hivyo unaweza kupendekeza katiba mpya iweke hayo mambo muhimu kwenye mahakama ya katiba, lakini kuanza kudai CHADEMA haitashika madaraka au odinga nk, haitasaidia.
 
Mbona unajicontradict?. Unasema katiba imeipa mamlaka makubwa NEC kwenye uchaguzi wa Rais halafu unasema kuwa vya vya Upinzani haviwezi kushinda. Tupunguze unafiki, Mwaka 2015 Rais alishinda kwa kura asilimia 57 Ina maana alivuka asilimia 7 tu, mwaka 2020 uchaguzi ukaharibiwa kwa wapinzani kuenguliwa na ujinga mwingi, Sasa unawalaumuje wapinzani kwamba hawawezi kushinda ilihali Tume ipo upande wa CCM ?.

Kwa Tanzania hali ni tofauti na Kenya, Zambia na Malawi. Kwa Tanzania CCM imejimilikisha nchi na ipo tayari kuua watu ili iendelee kukamata dola. Mwaka 2015 uchaguzi Zanzibar ulifutwa baada ya CUF kushinda, jeshi likatumwa Zanzibar. Sasa wewe Baki unalaumu wapinzani wakati CCM wamekula yamini kuwa hawataaachia madaraka .
Unazungumza shortcut sana. Ninachopinga ni kusema kuwa tamko la ushindi wa Rais, lakini siyo ushindi wa viti vingine kama wabunge na madiwani. Ni vigumu sana kwa chama chochote kushinda urais bila kushinda ubunge. Mambo hayo yangekuwa rahisi sana iwapo kuna chama kilipata wabunge wengi sana lakini kikakosa kiti cha urais ndipo unapoweza kutumia kifungu hicho ninachosema kina makosa.
 
Unazungumza shortcut sana. Ninachopinga ni kusema kuwa tamko la ushindi wa Rais, lakini siyo ushindi wa viti vingine kama wabunge na madiwani. Ni vigumu sana kwa chama chochote kushinda urais bila kushinda ubunge. Mambo hayo yangekuwa rahisi sana iwapo kuna chama kilipata wabunge wengi sana lakini kikakosa kiti cha urais ndipo unapoweza kutumia kifungu hicho ninachosema kina makosa.

Ubunge upi? Mwaka 2020 wagombea ubunge 180 wa CHADEMA walienguliwa ila baadaye 89 wakarudishwa wengine wakafutiliwa mbali na NEC. Fahamu Kura za ubunge zinasimamiwa na Mkurugenzi anayeteuliwa na Rais unategemea Nini?. Na hiki kilidhibitika mwaka 2020 ambapo wakurugenzi na hata wakuu wa mikoa waliingilia uchaguzi na kulazimisha kila mgombea ubunge wa CCM ashinde. Ili upinzani utangazwe umeshinda lazima wafuasi waandamane au mgombea aungwe mkono na zaidi ya asilimia 70 ya wapiga kura la sivyo hatangazei.
 
Hapa nilipoweka bold ndo Kwenye nyama. Hao chadema wanataka wawe na muda wa kupinga pinga matokeo kupotezeana tu muda.

Huo uhuru kautumia hata raila kaishia wapi kila siku anapinga matokeo tu anaamini wakenya wote wanamtaka
Demokrasi ina gharama zake, na mojawapo ni hiyo ya kurudia uchaguzi ili yule aliyeshindwa ajue kuwa alishindwa kiuhalali. Kenya waliwahi kurudia Uchaguzi wa rais, na najua Marekani kati ya Al-Gore na Bush ilichukua miezi miwili kabla ya ya uchaguzi kuamuliwa ingawa uliamuliwa kiitikadi lakini upande ulioshindwa ulielewa umeshindiwa wapi kikatiba.
 
Ubunge upi? Mwaka 2020 wagombea ubunge 180 wa CHADEMA walienguliwa ila baadaye 89 wakarudishwa wengine wakafutiliwa mbali na NEC. Fahamu Kura za ubunge zinasimamiwa na Mkurugenzi anayeteuliwa na Rais unategemea Nini?. Na hiki kilidhibitika mwaka 2020 ambapo wakurugenzi na hata wakuu wa mikoa waliingilia uchaguzi na kulazimisha kila mgombea ubunge wa CCM ashinde. Ili upinzani utangazwe umeshinda lazima wafuasi waandamane au mgombea aungwe mkono na zaidi ya asilimia 70 ya wapiga kura la sivyo hatangazei.
Unarudia yale yale. Katiba haizuii wabunge kupinga matokeo, inauia kupinga matokea ya urais tu. Kama kuna wagombea ubunge walionewa walikuwa na haki ya kikatiba kupinga matokeo, na kama hawakufanya hivyo ni lazima walijua kuwa walishindwa kihalali ila labda walitaka kupiga ngoma kwa wafuasi.

Jana au majuzi niliskiliza Zito Kabwe pale Wasafi akihojiwa. Mtu huyu alishindwa ubunge na alikuwa na uadui mkubwa sana dhidi ya Magufuli, lakini alikiri kuwa Magufuli alinyoosha nchi na wala hakupinga kupoteza ubunge. Kwa jinsi alivyokuwa vocal, asingeshindwa kwenda mahakamani.
 
Wananchi % kubwa hawajui umuhimu wa Katiba Mpya hata hii iliyopo hawaelewi so Mimi naomba Serikali itenge fungu la kuwapa watu MAARIFA waelewe hata maana ya katiba Mpya

Hii "itenge fungu" ina lengo ovu la kuonyesha wanaotaka katiba mpya wanataka ulaji. Usisahau tulishafikia kwenye katiba ya Warioba miaka 10 iliyopita.
 
Hii "itenge fungu" ina lengo ovu la kuonyesha wanaotaka katiba mpya wanataka ulaji. Usisahau tulishafikia kwenye katiba ya Warioba miaka 10 iliyopita.
Sawa huu mchakato wa Katiba Mpya unahitaji fungu Tena kubwa that way Mama kasema anajipanga , tunahitaji katiba yenye maoni ya wananchi wa Muda huu na sio 2014 hiyo hapana .
 
Sawa huu mchakato wa Katiba Mpya unahitaji fungu Tena kubwa that way Mama kasema anajipanga , tunahitaji katiba yenye maoni ya wananchi wa Muda huu na sio 2014 hiyo hapana .

Kwa hivyo 2014 wananchi walielewa umuhimu wa katiba mpya wakati huo ila leo 2023? Kwa sababu hiyo leo linatakiwa fungu (tena kubwa) la kutoa elimu?

Danganyaneni wenyewe Lumumba huko.

Hapa chini ni Uzi wako:

Rais Samia, kuhusu Katiba Mpya sisi wasomi tupo tayari kukusaidia kazi ili tupate Katiba nzuri na bora

Huku si ndiko kutega kunguru Kwa maharage makavu mjomba?

Wananchi wanataka katiba mpya wala hawatachuuzwa na wenye nia ovu nyie.
 
Back
Top Bottom