Mangatara,
Mwalimu JK Nyerere (Baba wa taifa lako) aliwahi kusema katika moja ya hotba zake akanena Wazanaki wanasema UBUBISUBISU OBUWERE EKIRO KIRIMBURA akiwa na maana ya MFICHAFICHA MARADHI KILIO KITAMFICHUA.
Labda nikuulize lile suala walilogombana kule Kanda ya Ziwa la NANI MWENYE HAKHI YA KUCHINJA, JE LIMEMALIZWA VIPI NA NANI ANA HAKI HIYO? Au ndo mumefunika kombe ...?
Kuuwa vikongwe na kunjofoa viungo vya albino, na kuchuna ngozi mtazimaliza kwa fast truck ipi hiyo? Kwani sasa ni miaka mingapi mumeshindwa ?
Kumbuka alipolifungua Bunge 2010 Kikwete alisema wazi suala la UDINI katika uchaguzi, Na juzi tu hapa Mbatia katika mkutano mkuu wa chama chake NCCR Mageuzi alilisema hilo, je hujui tu kama lipo au ndo unasubiri kifo kikuumbue.
Kifupi haa mambo yanafichwa na Muungano nje ya muungano ni changamoto kubwa sana kwa Tanganyika.
Pole sana
Barubaru,
Kama ni maudhi unayajua kweli kweli, Hivi huo udini unaousema kuwa JK aliusema, nikuulize tu kama weye ni Mwislam saafi, mwenye hofu ya Mnyazi Mungu SW, Huo udini kauanzisha nani? Si mwislam mwenzako? Jamani, Tanganyika siye hatuna ujinga huo wala hautapata upenyo. Si uliishia huko hukooo ulikotokea?
Kuhusu kuchinja, uchochezi ulitokea tu kwa wenzako hao hao wa ile dini. Baada ya kwenda kwenye mazishi. Unafika kwenye mazishi, unatamani pilao na minofu mikubwa mikubwa, ndo unaanza, kachinja nani. Kufiwa nimefiwa miye weye umekuja kulia au kula? Kama ukiona dhamira inakusuta si uache kula? kwani lazima? Mnaua Mchungaji kwa hasira ya kuchinja nyama? Tunahitaji kuzipima akili zetu. Ni nyama tu au kulikuwa na kingine?
Nasema tena, kama mambo haya yanafichwa na Muungano, nadhani basi hao Wazenj ni zaidi ya chumvi. Watu hawafiki laki saba, yaani population ya Zenj yoote haifikii ile ya Mji wa Morogoro, unasema ndio imeshikilia Tanganyia tukawa na amani! Nasema wanaousaka huo Muungano wanayajua wanayo yafaidi.
Kila mtaa Zanziba ni Jimbo la uchaguzi, upate hapo mwakilishi wa BWZ na mbunge wa Muungano. Upate hapo Mkuu wa mkoa, DC, Diwani, Waziri wa Muungano na wa Zanziba; na nanii, na nanii. Nasema kilio mtakachokuwa nacho, ni siku hilo limuungano litavunjika sijui mtapata wapi malipo ya hao viongozi utitiri.