Ni nini kinachosumbua Maalim Seif?

Ni nini kinachosumbua Maalim Seif?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
15,147
Reaction score
28,740
Kila ninaposikia kauli za Maalim Seif juu ya Muungano, ninapata picha kwamba zinazotelwa na mtu mwenye hasira sana dhidi ya serikali ya Tanzania, hususa Tanzania Bara. Sizioni kauli za Seif kama zinazotolewa na mzalendo wa Zanzibar, bali kama zinazotolewa na mtu mwenye hasira ya kisasi dhidi ya watu fulani. Katika kauli zake nyingi zimejaa "exaggeration" za hali ya juu, za aina ya mtu ambaye anataka kuwakomoa watu au kikundi fulani.

Sasa najiuliza, ni nini kinachomsumbua Maalim Seifu hadi kuwa na hasira ya namna hii?

Ni wazi kwamba si uzalendo wa kuwa M-Zanzibar. Kumbuka kwamba Seifu alitoa mchango mkubwa kwenye kuwajibishwa kwa Abdu Jumbe. Sefu alimchukulia Jumbe kuwa msaliti wa Muungano. Seifu ni mojawapo ya Wazanzibar waliofaidi na kuneemeka sana na Muungano. Bila muungano Seifu asingekuwa hapo alipo. Sasa ni nini kilimbadili Seifu? Je ni hasira baada ya kugundua ndoto yake ya kuwa Raisi wa Zanzibar isingetimia kupitia CCM? Au ni baada ya mashitaka na tuhuma alivyofanyiwa huko nyuma na sasa anataka kisasi?

Kuna mambo Seifu anataja kama faida za Zanzibar kujitoa kwenye Muungano ambayo ukifikiria utaona kwamba anawadanganya WaZanzibar kwa kuwa hayatawezekana, hata kama kweli watajitenga na muungano, kwa kuwa ni ndoto za alinacha, hayako "realistic". Sasa je, Maalimu Seifu anaona kwamba anaingia uzeeni na sasa kuna dalili kwamba kamwe hatakuwa raisi wa Zanzibar na hivyo anaona ni bora tu alivuruge?

Ni nini kinachompa hasira hii Maalim Seifu, na lengo lake ni nini hasa?
 
Mbona kama umeuliza swali alafu ukatoa majibu mwenyewe? anaway yote hapo juu ni sahihi bila kusahau udini na uharabu.
 
My friend, I think you are biting around the Bush here!! Ingekuwa vizuri kama ungetutolea mifano ya hizo kauri zake, jinsi gani anawadanganya Wazanzibar na hizo ndoto zake.
 
Ndugu yangu MADARAKA matamu,angekuwa Rais leo usingemsikia.
 
Mataifa ya magharibi yanamdanganya ili yaje yanyonye mafuta kirahisi. hasa uingereza.
 
hata zanzibar ikijitenga na muungano bado uchumi wake utaimarika tu tena hata zaidi kuliko ilivyokuwa ndani ya muungano. Lakini hili la maalim sifu limetokana na roho ya uchoyo na ubinafsi. Chimbuko kumbwa na hayo mafuta yao waliyogundua huko pemba. Maalim anafikiri kuwepo kwa muungano kutawafanya wapemba wasifaidike na mafuta hayo. Pengine ana ajenda yake ya siri kwenye hayo mafuta. Anasahau kwamba mafuta yanweza kuwepo hata bara. Ndio maana immediately baada ya mafuta kugunduliwa alihakikisha anapigania mafuta kuondolewa kwenye muungano.

Hata hivyo kama kuvunja muungano ni azma ya wazanzibar wote ama walio wengi, ni kwa nini sisi wabara tulalamike. Hatuwezi kulazimisha penzi la upande mmoja.
 
Dhambi ya usaliti kamwe haita kuacha salama. kama kweli alimsaliti huyo mzee ata tapatapa asipate huo urais mpk kufa. Knz ni tamaa tu apumzike aone new genaration kasi yake.
 
Zanzibar ina hadithi nyingi na siri nyingi!, za mapokeo, nikimaanisha ni maneno na vijineno vya mitaani ambavyo hayana uthibitisho Wala having uthibitisho ila ni hadithi tuu za mapokeo

Moja ya mapokeo haya, eti kwenye ile milingoti ya Bait Al Ajab, kila mlingoti ndani ni hollow, katikati aliwekwa mtu hai mtumwa akiwa amesinama!.

Kuna kisa cha Sultan fulani na mjakazi wa mkewe. Zamani toka enzi za Utumwa, Watumwa wanaume walihasiwa, ili wasizaliane, na watumwa wa kike wengi walifanya kazi ya ujaakazi, Miongoni mwa majukumu ya mjakazi, ni kumsaidia mama kazi zake zote!. Mila za Kiarabu ni za ya wake wengi. Miongoni mwa kanuni za uendeshaji wa ndoa za wake wengi, ni kuwatendea haki bin haki hao wake wote sawa sawa, ikiwemo kupangwa kwa zamu sawa za kulala kwenye nyumba za wake hao, kama ni kulala siku 3, then ni siku tatu kila nyumba.

Sasa inapofika zamu ya mume kulala nyumbani fulani, ikitokea mke hawezi, ili mume asikose haki yake, ilimbidi mke huyo kumtoa mjakazi wake, amuhudumie mumewe kwa zamu hiyo. ( Hili lilifanyika hata kwa Nabii Ibrahim, mkewe Sarah umri ulivuka bila kujaaliwa kupata mtoto, hivyo akamtoa mjakazi wake, mtumwa wa Kimisri, Hagir, ndipo akazaliwa Ismail).

Ikitoke huyu mjakazi akashika mimba, kuna mawili, mke akiridhia, yule mjakazi nae anaolewa akiitwa suria, na mtoto akizaliwa anakuwa ni mwana Sultani!. Mke asiporidhia, mjakazi yule anauwawa.

Kukatokea kisa cha Sultani fulani, alipoletewa mjaakazi, Sultani akapendezewa zaidi na mjaakazi akanogewa akafika jumla!. Ikawa ikifika zamu ya mke yule, Sultani anapewa chakula chake rasmi na mkewe, lakini anadai hajashiba, hivyo kulazimisha kushibishwa na chakula cha mjakazi!.

Hii hali ikasababisha husda kubwa na ugomvi mkubwa kati ya mke na mjakazi!. Kikawaida mke akitofautiana na mjakazi, mke huomba mjakazi yule auwawe, mke alipoomba mjaakazi auwawe, Sultani aligoma, hivyo ili kuepusha shari, mjakazi yule akahamishwa na kuwekwa eneo la masuria wa Sultani wasio na ndoa (concubines), masuria hawa huwa hawapati zamu za Sultani, bali Sultan huja kwao kujipumzikia wakati wowote wa asubuhi, mchana au jioni Sultani anapojisikia kujipumzisha kupooza tuu njaa na kiu haswa wakati wa mchana, akisubiria mlo wa usiku.

Huku na kule, huku na kule, mara yule mkakazi akanasa!, hapa sasa Sultani akawa hawa jinsi, siri lazima itafichuka, na mjakazi itambidi auwawe Kwa vile Sultani alimpenda kwa dhati yule mjakazi yule, aliamua kuificha siri na kuyanusuru maisha ya mjakazi yule kwa kufanya mipango wa siri, huyo mjakazi kupelekwa mahali pasipo julikana kabla siri haijafumka, na huko kuendelea na maisha yake kama mtumwa huru.

Mjaakazi yule alijuja kuposwa akaolewa na kuendelea na maisha mapya!. Familia hiyo ni top secret ila tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Oman, Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, Utapata majibu!.

Kwa taarifa tuu, kwa msiojua, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote huko, wanashinda lakini hawapewi ushindi, kwa sababu!. Ila pia amini usiamini uchaguzi wa 2015, CUF itashinda tena Zanzibar, lakini bado haitapewa ushindi, kwa sababu fulani very genuine!, kwa vile hizo sababu zinazopelekea CUF ishinde siku zote na isipewe ushindi, zingalipo zipo, CUF wasipojishughulisha kuzijua, ni sababu gani, wataendelea kushiiki uchaguzi wa rais kwa kufanya kazi bure, ni kama kukimbiza tuu upepo au kutwanga maji kwenye kinu, lakini mwisho wa siku, hawapati Kitu .Ningekuwa mimi CUF, kwanza ningedeal na kuzijua hizo sababu za kwa nini huwa nashinda lakini kwa nini hawanipi ushindi wangu halali?!, nikijiridhisha kuwa this time sababu za kutopewa sasa hazipo tena, ndipo niingie kwenye uchaguzi wa urais, vinginevyo uchaguzi urais wa Zanzibar ni just a wastage of time, money and resources!.

Visa vya Zanzibar heveshi, kuna kisa kingine tena cha ndugu wawili wa tumbo moja, watoto wa kiume wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. Baba yao alifanya makubwa, Chama fulani cha siasa kikaamua kumzawadia nafasi ya urais kaka miubwa kati ya hawa wanadugu wawili. Sababu ya kumzawadia uais mtoto huyo, ni ili kuuenzi mchango wa baba yao, aliyekuwa rais na kuifia nchi yake kishujaa. Japo baba yao alitokea nchini nyingine, licha ya kutokuwa mzaliwa wala mwenye asili yoyote ya Zanzibar, lakini aliifanyia makubwa Zanzibar, hadi kujitoa uhai wake kuifia Zanzibar. Hivyo ile zawadi ya urais kwa mwanaye ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ushujaa wa baba yao!. Ni kweli kaka mtu akaupata urais kwa mtindo ule ule wa bao la mkono, baada ya mshindi halisi kutotangazwa. Kaka mtu huyo akahudumu urais wa kipindi chote cha miaka 10!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, kitu cha ajabu sana, eti mdogo mtu naye akaibuka, akachukua fomu kutaka kumrithi kaka mtu akijua kuwa eti urais wa Zanzibar nao uendeshwe kama usultani!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza muda wa urais ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, kumrithi kaka mtu, itaonekana kuwa chama chao kinaufanya urais kama usultani!, mdogo mtu, akaelezwa kakaye kapewa tuu urais kwa hishma ya baba yao, lakini bado akagoma na kusisitiza kugombea kwa hoja kuwa eti kama urais ni wa zawadi kwa mtoto wa yule Mzee Shujaa, waliomuheshimu na kumuenzi, then "mtoto halisi aliyestahili urais ule ni yeye!", Kiukweli Zanzibar haieshi vituko!,

Nataka niwashauri wajumbe wa Bunge la Katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa huu muungano wetu adhimu kwa kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco
 
Synthesizer nimekupata vizuri. Najua hukuandika kwa kirefu sana sababu unajua wengi wetu tunaielewa vizuri HISTORIA ya Zanzibar, na mtafaruku uliokuwepo mpaka Abdu Jumbe kusimamishwa, pamoja na hekaheka za Maalim Seif kutoka CCM (akiwa na nguvu kisiasa) na baadaye kupigania Urais kupitia CUF kwa "miongo" kadhaa bila mafanikio. Binafsi nilijua baada ya huyu kiongozi kukubaliana na CCM Zanzibar kuunda serikali ya mseto (rejea hotuba nzuri aliyoitoa kipindi wanamaliza uchaguzi), ni wazi tulijua ameshapozwa ili amalize upinzani Zanzibar. CCM walimtafuta siku nyingi, wakaanza kumlipa pension ya kuwahi kuwa Waziri Kiongozi, akalainika kidogo na baadaye umakamu wa Rais wa bendera anaoushikilia hadi sasa. Kitu hiki kimewaudhi sana ndugu zake WAPEMBA ambao walimuamini sana, na nia yao kubwa ilikuwa PEMBA ijitenge na UNGUJA "huu ndiyo mziki mzito kule", hili swala la SERIKALI 2 ama 3 halipo kwenye mishipa yao, maana wengi hawautaki huu muungano si wa BARA na VISIWANI tu, bali hata wa PEMBA na UNGUJA. Kama tume ya Jaji Warioba ingetoa takwimu kulingana na visiwa hivi viwili, basi ungeona picha tofauti kabisa kati ya PEMBA na UNGUJA. Sasa turudi kwa mh. Maalim Seif, yeye baada ya kuvimbiwa, imebidi awarudie wenzake wa PEMBA ili wapunguze hasira naye, maana huyu jamaa ameuwa upinzani kabisaaa na hata kumpoteza RASHID HAMAD kwenye siasa za mikikimikiki ambaye ni ndugu yake kabisa wa kutoka PEMBA. Kwa hiyo lazima awe na maluweluwe mengi tu maana hajui anachosimamia hivi sasa......


Kwakifupi: Huyu jamaa ni mtu wa fitna tu ili ajitengenezee shibe, tazama hii picha utapata majibu mengi tu.
Seif na Hamad.jpg
 
Synthesizer nimekupata vizuri. Najua hukuandika kwa kirefu sana sababu unajua wengi wetu tunaielewa vizuri HISTORIA ya Zanzibar, na mtafaruku uliokuwepo mpaka Abdu Jumbe kusimamishwa, pamoja na hekaheka za Maalim Seif kutoka CCM (akiwa na nguvu kisiasa) na baadaye kupigania Urais kupitia CUF kwa "miongo" kadhaa bila mafanikio. Binafsi nilijua baada ya huyu kiongozi kukubaliana na CCM Zanzibar kuunda serikali ya mseto (rejea hotuba nzuri aliyoitoa kipindi wanamaliza uchaguzi), ni wazi tulijua ameshapozwa ili amalize upinzani Zanzibar. CCM walimtafuta siku nyingi, wakaanza kumlipa pension ya kuwahi kuwa Waziri Kiongozi, akalainika kidogo na baadaye umakamu wa Rais wa bendera anaoushikilia hadi sasa. Kitu hiki kimewaudhi sana ndugu zake WAPEMBA ambao walimuamini sana, na nia yao kubwa ilikuwa PEMBA ijitenge na UNGUJA "huu ndiyo mziki mzito kule", hili swala la SERIKALI 2 ama 3 halipo kwenye mishipa yao, maana wengi hawautaki huu muungano si wa BARA na VISIWANI tu, bali hata wa PEMBA na UNGUJA. Kama tume ya Jaji Warioba ingetoa takwimu kulingana na visiwa hivi viwili, basi ungeona picha tofauti kabisa kati ya PEMBA na UNGUJA. Sasa turudi kwa mh. Maalim Seif, yeye baada ya kuvimbiwa, imebidi awarudie wenzake wa PEMBA ili wapunguze hasira naye, maana huyu jamaa ameuwa upinzani kabisaaa na hata kumpoteza RASHID HAMAD kwenye siasa za mikikimikiki ambaye ni ndugu yake kabisa wa kutoka PEMBA. Kwa hiyo lazima awe na maluweluwe mengi tu maana hajui anachosimamia hivi sasa......


Kwakifupi: Huyu jamaa ni mtu wa fitna tu ili ajitengenezee shibe, tazama hii picha utapata majibu mengi tu.
View attachment 140221

Aiseeeeee.........!!
 
Zanzibar in a siri nyingi!, tafuta kisa cha Sultan kumpachika ujauzoto mjakazi wa mkewe, ili kuficha siri, huyo mjakazi alikwenda kuozeshwa mahali mbali chap chap!, baadaye, mwana sulatan alizaliwa huko mjakazi alikoolewa!. Find out huyo mwana sulatan ni nani?!, tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, find out who funds CUF and why?!.

Kwa taarifa tuu, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote kwa nini hawampi ushindi?!.

Visa vya Zanzibar havikuishia hapo, kuna ndugu tena wengine wawili, watoto wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. CCM ikaamua kumzawadia urais kaka mkubwa, kisa ni kumuenzi baba yao aliyoifanyia makubwa Zanzibar, hivyo ule urais ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ya marehemu babsa yao!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, mdogo mtu akachukua fomu kumrithi kaka mtu!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, itaonekana kama usultani!, mdogo mtu akagoma na kuibuka na madai mazito!, kuwa eti kama urais ni zawadi kwa mtoto wa yule Mzee waliomuheshimu, then "mtoto halisi aliyestahili ni yeye!".

Zanzibar haieshi vituko!, nataka niwashauri wajumbe wa bunge la katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa muungano na kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco

Pamoja na ugamba wako hapa kuna kitu nimejifinza
 
Zanzibar in a siri nyingi!, tafuta kisa cha Sultan kumpachika ujauzoto mjakazi wa mkewe, ili kuficha siri, huyo mjakazi alikwenda kuozeshwa mahali mbali chap chap!, baadaye, mwana sulatan alizaliwa huko mjakazi alikoolewa!. Find out huyo mwana sulatan ni nani?!, tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, find out who funds CUF and why?!.

Kwa taarifa tuu, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote kwa nini hawampi ushindi?!.

Visa vya Zanzibar havikuishia hapo, kuna ndugu tena wengine wawili, watoto wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. CCM ikaamua kumzawadia urais kaka mkubwa, kisa ni kumuenzi baba yao aliyoifanyia makubwa Zanzibar, hivyo ule urais ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ya marehemu babsa yao!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, mdogo mtu akachukua fomu kumrithi kaka mtu!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, itaonekana kama usultani!, mdogo mtu akagoma na kuibuka na madai mazito!, kuwa eti kama urais ni zawadi kwa mtoto wa yule Mzee waliomuheshimu, then "mtoto halisi aliyestahili ni yeye!".

Zanzibar haieshi vituko!, nataka niwashauri wajumbe wa bunge la katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa muungano na kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco

unajua pasco nakuheshim sana ktkana na weled wko wkucomment bt at the some time cc wasomi unatuboa ktkn sijui unafanya kusudi au una udhaif some where ,hutofautishi baina ya theory na propaganda japokuwa vinakaribiana ila sishangai sana hzo kw 70% ndvyo baba wenu wa taifa alivyopropagate na akawalisha sumu ,sasa ndugu yangu jirekebishe hasa unapoongelea znz coz huijui history yake nd hvy blah blah tu sijui okello...... sijui ...........,nliskiliza mada yako moja nlichoka wallah ,sincerely nimekuelewa ni mtu wa aina gn ktk hyo comment yko mwisho
 
Zanzibar in a siri nyingi!, tafuta kisa cha Sultan kumpachika ujauzoto mjakazi wa mkewe, ili kuficha siri, huyo mjakazi alikwenda kuozeshwa mahali mbali chap chap!, baadaye, mwana sulatan alizaliwa huko mjakazi alikoolewa!. Find out huyo mwana sulatan ni nani?!, tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, find out who funds CUF and why?!.

Kwa taarifa tuu, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote kwa nini hawampi ushindi?!.

Visa vya Zanzibar havikuishia hapo, kuna ndugu tena wengine wawili, watoto wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. CCM ikaamua kumzawadia urais kaka mkubwa, kisa ni kumuenzi baba yao aliyoifanyia makubwa Zanzibar, hivyo ule urais ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ya marehemu babsa yao!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, mdogo mtu akachukua fomu kumrithi kaka mtu!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, itaonekana kama usultani!, mdogo mtu akagoma na kuibuka na madai mazito!, kuwa eti kama urais ni zawadi kwa mtoto wa yule Mzee waliomuheshimu, then "mtoto halisi aliyestahili ni yeye!".

Zanzibar haieshi vituko!, nataka niwashauri wajumbe wa bunge la katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa muungano na kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco

Hadithi njoo!uongo njoo!utam kolea!
 
unajua pasco nakuheshim sana ktkana na weled wko wkucomment bt at the some time cc wasomi unatuboa ktkn sijui unafanya kusudi au una udhaif some where ,hutofautishi baina ya theory na propaganda japokuwa vinakaribiana ila sishangai sana hzo kw 70% ndvyo baba wenu wa taifa alivyopropagate na akawalisha sumu ,sasa ndugu yangu jirekebishe hasa unapoongelea znz coz huijui history yake nd hvy blah blah tu sijui okello...... sijui ...........,nliskiliza mada yako moja nlichoka wallah ,sincerely nimekuelewa ni mtu wa aina gn ktk hyo comment yko mwisho

Loh......maajabu haya......eti msomi....mh??????
 
Kila ninaposikia kauli za Maalim Seif juu ya Muungano, ninapata picha kwamba zinazotelwa na mtu mwenye hasira sana dhidi ya serikali ya Tanzania, hususa Tanzania Bara. Sizioni kauli za Seif kama zinazotolewa na mzalendo wa oZanzibar, bali kama zinazotolewa na mtu mwenye hasira ya kisasi dhidi ya watu fulani. Katika kauli zake nyingi zimejaa "exaggeration" za hali ya juu, za aina ya mtu ambaye anataka kuwakomoa watu au kikundi fulani.

Sasa najiuliza, ni nini kinachomsumbua Maalim Seifu hadi kuwa na hasira ya namna hii?

Ni wazi kwamba si uzalendo wa kuwa M-Zanzibar. Kumbuka kwamba Seifu alitoa mchango mkubwa kwenye kuwajibishwa kwa Abdu Jumbe. Sefu alimchukulia Jumbe kuwa msaliti wa Muungano. Seifu ni mojawapo ya Wazanzibar waliofaidi na kuneemeka sana na Muungano. Bila muungano Seifu asingekuwa hapo alipo. Sasa ni nini kilimbadili Seifu? Je ni hasira baada ya kugundua ndoto yake ya kuwa Raisi wa Zanzibar isingetimia kupitia CCM? Au ni baada ya mashitaka na tuhuma alivyofanyiwa huko nyuma na sasa anataka kisasi?

Kuna mambo Seifu anataja kama faida za Zanzibar kujitoa kwenye Muungano ambayo ukifikiria utaona kwamba anawadanganya WaZanzibar kwa kuwa hayatawezekana, hata kama kweli watajitenga na muungano, kwa kuwa ni ndoto za alinacha, hayako "realistic". Sasa je, Maalimu Seifu anaona kwamba anaingia uzeeni na sasa kuna dalili kwamba kamwe hatakuwa raisi wa Zanzibar na hivyo anaona ni bora tu alivuruge?

Ni nini kinachompa hasira hii Maalim Seifu, na lengo lake ni nini hasa?


Hebu tuacheni tupumue, hatulitaki hili dubwasha liitwalo muungano, Watanganyika mnachekesha, nyinyi mmejaaliwa ukubwa wa ardhi lakini badi mnaingangania Zanzibar. Kaeni na Tanganyika yenu tuachieni Zanzubar yetu tuchachoka na chokochoko zenu
 
Back
Top Bottom