Ni nini kinachosumbua Maalim Seif?

Ni nini kinachosumbua Maalim Seif?

hivi jaman kwani kuna kitabu gani cha dini kimeandika lazima Tanganyika na Zanzibar tuungane?? tuwaacheni hawa wazanzibar kanchi kao tuone watakavyoauana na hasira zao na umwinyi.., maana wanajiona kama wao ndio wajuaji wa kila jambo..., mara waseme hatujui Kiswahili,mawa waseme hatuna maadili.., yaani kwa mzanzibari mwanaume shoga ni bora kuliko mwanaume mlevi..,kifupi we have different culture so kwann tulazimishe muungani na watu wasiofika hata million 2..,

Hivi Hayo Maneno Ya Uchochezi Na Chuki Kiasi Hiki Yanatoka Wapi!!?? Jmn Kuna Maisha Yanaendelea Baada Ya CHAGUZI!! Maalim Kama Ameshinda Apewe KITI CHAKE, Kama Ilivyokuwa Kwa Magufuli!! Historia Ya CHAGUZI Za Miaka Ya Huko Nyuma Watanganyika Na Wazanzibar Wanaijua Vizuri Saana!!!
 
Synthesizer nimekupata vizuri. Najua hukuandika kwa kirefu sana sababu unajua wengi wetu tunaielewa vizuri HISTORIA ya Zanzibar, na mtafaruku uliokuwepo mpaka Abdu Jumbe kusimamishwa, pamoja na hekaheka za Maalim Seif kutoka CCM (akiwa na nguvu kisiasa) na baadaye kupigania Urais kupitia CUF kwa "miongo" kadhaa bila mafanikio. Binafsi nilijua baada ya huyu kiongozi kukubaliana na CCM Zanzibar kuunda serikali ya mseto (rejea hotuba nzuri aliyoitoa kipindi wanamaliza uchaguzi), ni wazi tulijua ameshapozwa ili amalize upinzani Zanzibar. CCM walimtafuta siku nyingi, wakaanza kumlipa pension ya kuwahi kuwa Waziri Kiongozi, akalainika kidogo na baadaye umakamu wa Rais wa bendera anaoushikilia hadi sasa. Kitu hiki kimewaudhi sana ndugu zake WAPEMBA ambao walimuamini sana, na nia yao kubwa ilikuwa PEMBA ijitenge na UNGUJA "huu ndiyo mziki mzito kule", hili swala la SERIKALI 2 ama 3 halipo kwenye mishipa yao, maana wengi hawautaki huu muungano si wa BARA na VISIWANI tu, bali hata wa PEMBA na UNGUJA. Kama tume ya Jaji Warioba ingetoa takwimu kulingana na visiwa hivi viwili, basi ungeona picha tofauti kabisa kati ya PEMBA na UNGUJA. Sasa turudi kwa mh. Maalim Seif, yeye baada ya kuvimbiwa, imebidi awarudie wenzake wa PEMBA ili wapunguze hasira naye, maana huyu jamaa ameuwa upinzani kabisaaa na hata kumpoteza RASHID HAMAD kwenye siasa za mikikimikiki ambaye ni ndugu yake kabisa wa kutoka PEMBA. Kwa hiyo lazima awe na maluweluwe mengi tu maana hajui anachosimamia hivi sasa......


Kwakifupi: Huyu jamaa ni mtu wa fitna tu ili ajitengenezee shibe, tazama hii picha utapata majibu mengi tu.
attachment.php

Elections zote ana shinda lakini hapewi ushindi and that is a BIG PROBLEM, na kwa nini anashinda ? sababu waZanzibari hawataki muungano. Kwa nin vigumu kuwaachia waZanzibari wajiamulie wenyewe THAT IS THE BIG QUESTION TO BE ASKED.
My opinion is : time has come to let Zanzibar go for the sake of humanity and peace.
 
Naona wakuda mmehamia zanzibar,sasa mnaanza propaganda ili uchaguzi ukirudiwa watu wasimchague Seif!Wapuuzi sana
 
Naona wakuda mmehamia zanzibar,sasa mnaanza propaganda ili uchaguzi ukirudiwa watu wasimchague Seif!Wapuuzi sana

Pale uchaguzi hata ukirudiwa Mara 100, haki mungu seif anashinda, na hilo ccm wanalijua, tatizo linakuja kutoa nchi tu, ndio shuhuli mwenyewe. Wamekula yamini hawatoi kwa karatasi nchi.
 
Pale uchaguzi hata ukirudiwa Mara 100, haki mungu seif anashinda, na hilo ccm wanalijua, tatizo linakuja kutoa nchi tu, ndio shuhuli mwenyewe. Wamekula yamini hawatoi kwa karatasi nchi.

Watalegea tu ,hamna namna. HAKI!
 
Kinachomsumbua Seif ni kutaka haki itendeke na upande ulioshinda utangazwe mshindi. HICHO NDICHO KINACHOMSUMBUA!
 
mr.London, niliuliza kama ni kweli kila siku huwa anashinda lakini hapewi,
  1. Kwa nini huwa hapewi?.
  2. Jee hizo sababu zinazofanya hapewi ni justifiable?.
  3. Kama ameshinda tena na safari hii, nini kitafanya apewe?!.
Pasco
Haka ni kaswali ambacho kila tukikaribia uchaguzi Mkuu kwa upande wa Zanzibar huwa nikauliza.

Kama akiwa CUF, siku zote huwa anashinda lakini hapewi, nini huwa kinafanya asipewe?.

Kama amekuwa hapewi akiwa CUF, jee sasa akiwa ACT, anaweza kupewa?.

Uthibitisho kuwa huwa anashinda ni huu
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda - JamiiForums
P
 
Haka ni kaswali ambacho kila tukikaribia uchaguzi Mkuu kwa upande wa Zanzibar huwa nikauliza.

Kama akiwa CUF, siku zote huwa anashinda lakini hapewi, nini huwa kinafanya asipewe?.

Kama amekuwa hapewi akiwa CUF, jee sasa akiwa ACT, anaweza kupewa?.

Uthibitisho kuwa huwa anashinda ni huu
Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda - JamiiForums
P
Nimependa kwa kuweka kumbukumbu nini hasa kilitokea kule Zanzibar..

CCM sio kwamba hawampi Seif Sharifu tu bali hawatampa yeyote yule,hawakumpa Lowassa, na wataendelea kuwanyima wengine...

UROHO,UCHU,na UNG'ANG'ANIZI wa madaraka ndio sera za CCM,hichi chama kimelewa madaraka,CCM ni janga la Taifa
 
Kila ninaposikia kauli za Maalim Seif juu ya Muungano, ninapata picha kwamba zinazotelwa na mtu mwenye hasira sana dhidi ya serikali ya Tanzania, hususa Tanzania Bara. Sizioni kauli za Seif kama zinazotolewa na mzalendo wa Zanzibar, bali kama zinazotolewa na mtu mwenye hasira ya kisasi dhidi ya watu fulani. Katika kauli zake nyingi zimejaa "exaggeration" za hali ya juu, za aina ya mtu ambaye anataka kuwakomoa watu au kikundi fulani.

Sasa najiuliza, ni nini kinachomsumbua Maalim Seifu hadi kuwa na hasira ya namna hii?

Ni wazi kwamba si uzalendo wa kuwa M-Zanzibar. Kumbuka kwamba Seifu alitoa mchango mkubwa kwenye kuwajibishwa kwa Abdu Jumbe. Sefu alimchukulia Jumbe kuwa msaliti wa Muungano. Seifu ni mojawapo ya Wazanzibar waliofaidi na kuneemeka sana na Muungano. Bila muungano Seifu asingekuwa hapo alipo. Sasa ni nini kilimbadili Seifu? Je ni hasira baada ya kugundua ndoto yake ya kuwa Raisi wa Zanzibar isingetimia kupitia CCM? Au ni baada ya mashitaka na tuhuma alivyofanyiwa huko nyuma na sasa anataka kisasi?

Kuna mambo Seifu anataja kama faida za Zanzibar kujitoa kwenye Muungano ambayo ukifikiria utaona kwamba anawadanganya WaZanzibar kwa kuwa hayatawezekana, hata kama kweli watajitenga na muungano, kwa kuwa ni ndoto za alinacha, hayako "realistic". Sasa je, Maalimu Seifu anaona kwamba anaingia uzeeni na sasa kuna dalili kwamba kamwe hatakuwa raisi wa Zanzibar na hivyo anaona ni bora tu alivuruge?

Ni nini kinachompa hasira hii Maalim Seifu, na lengo lake ni nini hasa?
Mzalendo wa Zanzibar ni yule anaepigania haki za msingi za Zanzibar na Wazanzibari wenywewe

Binafsi sioni kama Seif ana hasira na mtu au kikundi cha watu,Niomacho ni kuwa Seif ana hasira na uongo na dhulma wanazofanyiwa Wazanzibari na CCM..

Unachotakiwa ujuwe kuwa sio Seif tu ndie mwenye hasira na CCM bali nii Wanzibari kwa ujumla...

Wakati wazanzibari wanachukua Nchi kutoka kwa Sultan 1964,Zanzibar kiuchumi ilikuwa kama unavyoiona Dubai sasa

Zanzibar ilikuwa tayari imepiga hatua za maendeleo kwa wakati ule..iko wapi Zanzibar kiuchumi hivi sasa?

Inasemekana Karume alipoamua kuungana na Nyerere kisiasa,waliunganisha mambo 12,hivi sasa kuna zaidi ya mambo 22,mengi yao yakiwa yameingizwa kinyemela,ki ulaghai laghai..

Uongo,Ulaghai,Ubabe wa CCM kwenye huu Mungano ndio kinachowafanya Wazanzibar wauchukie Muungano na wamuunge mkono Seif..

Kumbuka kuwa kabla ya huu Muungano wa Kisiasa ambao umeasisiwa na Nyerere na mwenzake Karume,Wazanzibari na Watanganyika walikuwa wameshaungana,kiitikadi,kimila,kifamilia nk

Wazanzibari walikuwa wanaowana na kufurahia maisha na ndungu zao wa Mrima(Tanganyika) bila ya hofu,..

Mungano wa kisiasa umefanya watu wa nchi hizi mbili wachukiane,wasiowane na kudharauliana..

Wakati umefika Wazanzibari wapewe wanachotaka ili waendelee na maisha yao ya kila siku..
 
Inasemekana Karume alipoamua kuungana na Nyerere kisiasa,waliunganisha mambo 12,hivi sasa kuna zaidi ya mambo 22,mengi yao yakiwa yameingizwa kinyemela,ki ulaghai laghai..

Uongo,Ulaghai,Ubabe wa CCM kwenye huu Mungano ndio kinachowafanya Wazanzibar wauchukie Muungano na wamuunge mkono Seif.
Mkuu Chabuso, mimi naamini msimamo wa Maalim kuhusu Muungano, ndicho kinamfanya anashinda lakini hapewi.
P.
 
Mkuu Chabuso, mimi naamini msimamo wa Maalim kuhusu Muungano, ndicho kinamfanya anashinda lakini hapewi.
P.
P,..Mungano wa kisiasa unaweza kupungua kwa baadhi ya mambo lakini hauwezi kuvunjika,Seif hawezi kuvunja Muungano kabisa kabisa,Wazanzibari hawatomruhusu..

Kumbuka kuna Muungano uliokomaa baina ya watu wa pande hizi mbili yaani Mrima na Zanzibar,makabila ya Pwani na mengine kutoka Bara nyengine ndio yaliyounda Utamaduni wa Zanzibar..

Wazanzibari waachiwe wafanye kile wanachokitaka,kile wanachokiamini
 
Kila ninaposikia kauli za Maalim Seif juu ya Muungano, ninapata picha kwamba zinazotelwa na mtu mwenye hasira sana dhidi ya serikali ya Tanzania, hususa Tanzania Bara. Sizioni kauli za Seif kama zinazotolewa na mzalendo wa Zanzibar, bali kama zinazotolewa na mtu mwenye hasira ya kisasi dhidi ya watu fulani. Katika kauli zake nyingi zimejaa "exaggeration" za hali ya juu, za aina ya mtu ambaye anataka kuwakomoa watu au kikundi fulani.

Sasa najiuliza, ni nini kinachomsumbua Maalim Seifu hadi kuwa na hasira ya namna hii?

Ni wazi kwamba si uzalendo wa kuwa M-Zanzibar. Kumbuka kwamba Seifu alitoa mchango mkubwa kwenye kuwajibishwa kwa Abdu Jumbe. Sefu alimchukulia Jumbe kuwa msaliti wa Muungano. Seifu ni mojawapo ya Wazanzibar waliofaidi na kuneemeka sana na Muungano. Bila muungano Seifu asingekuwa hapo alipo. Sasa ni nini kilimbadili Seifu? Je ni hasira baada ya kugundua ndoto yake ya kuwa Raisi wa Zanzibar isingetimia kupitia CCM? Au ni baada ya mashitaka na tuhuma alivyofanyiwa huko nyuma na sasa anataka kisasi?

Kuna mambo Seifu anataja kama faida za Zanzibar kujitoa kwenye Muungano ambayo ukifikiria utaona kwamba anawadanganya WaZanzibar kwa kuwa hayatawezekana, hata kama kweli watajitenga na muungano, kwa kuwa ni ndoto za alinacha, hayako "realistic". Sasa je, Maalimu Seifu anaona kwamba anaingia uzeeni na sasa kuna dalili kwamba kamwe hatakuwa raisi wa Zanzibar na hivyo anaona ni bora tu alivuruge?

Ni nini kinachompa hasira hii Maalim Seifu, na lengo lake ni nini hasa?
Utujibu kwanza wewe ni nini hasa kinachokusumbua juu yake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Taratibu tumeanza kuelewa ni nini kinachomsumbua Maalim Seif
 
Kuna kauli, kuna mambo, ana hasira, kauli zake zimejaa exaggeration, anataka kuwakomoa watu Fulani... mkuu unataka kuongea nini hasa? mbona huweleweki na huwi muwazi? na kaka yangu Pascal Mayalla bado tu unatumia kumtaja muarabu muarabu muaraba hadi eo kaka? Muandishi mwenye kaliba kama yako bado unasiasa za Uarabu Zanzibar hadi sasa kaka? kweli!!! kuna ukanda umeenea Tanganyika, kuna upendeleo wa Dhahiri kwenye ajira mbona hulizungumzi hili kaka? inahuzunisha sana mnapopindisha ukweli na hasa wa nini kinachotokea Zanzibar wakati ni mwendo wa dakika 90 tu kwa boti. Wakuu ulimwengu wa sasa huwezi kutumia cheap politics kama hizi za uarabu, watu wamesoma, wanatembea ulimwenguni kila leo na wana excess mitandao kila uchwao, na kwamba eti sefu anakuwa na kauli za exaggeration, unajaribu kuunda hoja bila ya kutoa mfano hata mmoja. Ifike mahala wakuu mukue kiakili angalau kidogo, mnajidhalilisha sana mbele ya watoto wenu.
 
Zanzibar ina siri nyingi!, watatafute Wanzanzibar wa enzi zile, wakuhadithie kisa cha Sultan fulani kumpachika ujauzito mjakazi wa mkewe. Zamani toka enzi za Utumwa, wanaume watumwa, walihasiwa, ili wasizaliane, ila watumwa wa kike wengi walifanya kazi ya ujaakazi, kwa wanawake wa Kiarabu. Miongoni mwa majukumu ya mjakazi, ni kumsaidia mama kazi zake zote!. Mila za Kiarabu zinafuata misingi ya Dini ya Kiislamu, ya wake wengi. Miongoni mwa kanuni za uendeshaji wa ndoa za wake wengi, ni kuwatendea haki bin haki wake wote sawa sawa, hivyo kupangwa kwa zamu za kulala kwa wake hao, kama ni kulala siku 3 tatu, then mume analala kwa kila mke siku tatu tatu za zamu yake.

Kila mke anakuwa na wajakazi wake, wanaopangiwa majukumu mbalimbali, wengine kumuogesha, wengine kumpikia, wengine kumtandikia kitanda, wengine kumpepea tuu, enzi hizo kilikuwa hakuna feni, etc. Sasa inapofika zamu ya mume kulala nyumbani kwa mke huyu, ikitokea ni zile "siku" ambazo mke huyo hawezi, ili yule mke asipoteze zamu zake, ilimbidi mke huyo ambaye hawezi, kumtoa mjakazi wake, amuhudumie mumewe kwa siku ambazo zamu yake imefika lakini yeye mke hawezi!. Ikitoke huyu mjakazi akashika mimba, kuna mawili, mke akiridhia, yule mjakazi nae anaolewa akiitwa suria, na mtoto akizaliwa anakuwa ni mwana Sultani!. Mke asiporidhia, mjakazi yule anauwawa kwa kutumbuliwa tumbo kiumbe kinaondolewa, mjakazi anazikwa kama mbwa, kiumbe kinazikwa makaburi za "si rizki" ya ukoo wa kisultani.

Kukatokea kisa cha Sultani fulani, alipoletewa mjaakazi, Sultani akakuta mjakazi anakolea kuliko mke, hivyo Sultani akanogewa akafika jumla!. Ikawa ikifika zamu ya mke yule, Sultani anapewa chakula chake rasmi na mkewe, lakini anadai hajashiba, hivyo kulazimisha kushibishwa na chakula cha mjakazi!. Mara zamu za mke zikaanza kubadilishwa, kwa siku mbili chakula cha mke, na siku moja chakula cha mjakazi, siku za cha mke zikaanza kupunguzwa huku za mjakazi zikiongezeka, ikawa hata zile siku mbazo mkewe anaweza sulatani anataka mjaakazi!. Kadri siku zilivyokwenda, zamu za mke huyu zikifika siku mbili mke, siko moja mjakazi, siku zikawa zinabadilika, mara siku mbili mjakazi siku moja mke, mara ikaja siku zote tatu mjakazi, mke hapati kitu, ili hali yuko fiti! (sijui mjakazi huyu alichukuliwa utumwani kutoka Tanga?!).

Hii hali ikasababisha husda kubwa na ugomvi mkubwa kati ya mke na mjakazi!. Kikawaida mke akitofautiana na mjakazi, mke huomba mjakazi yule auwawe, mke alipoomba mjaakazi auwawe, Sultani aligoma, hivyo ili kuepusha shari, mjakazi yule akahamishwa na kuwekwa eneo la masuria wa Sultani wasio na ndoa (concubines), masuria hawa huwa hawapati zamu za Sultani, hula kwao wakati wowote sultani anapojisikia kwa lengo la kupooza tuu njaa na kiu haswa wakati wa mchana!.

Huku na kule, huku na kule, mara yule mkakazi akanasa!, ujauzito wa sultani, na hapa sasa Sultani akawa hawa jinsi, siri ya ujauzito ikifumuka lazima mkakazi yule auwawewe kwa kutobolewa tumbo!. Kwa vile Sultani alimpenda kwa dhati yule mjakazi yule, aliamua kuificha siri na kuyanusuru maisha ya mjakazi yule kwa kufanya mipango wa siri, huyo mjakazi kupelekwa mahali na kuozeshwa kwa ndoa ya mkeka mahali mbali chap chap kabla siri haijafumka!. Yule mjakazi alikwenda kuolewa chap chap bila muoaji kujua kuwa muolewaji ana mizigo ya watu!.

Baadaye, mwana Sultani alizaliwa huko mjakazi alikoolewa na kulelewa kama mtoto wa kawaida kwenye familia hiyo, ila familia ile ilipata preferential treatments kwa mwana Sultani yule kulelewa vizuri ilmu duniya!. Find out huyo mwana Sultan ni nani?!, tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Oman, Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, find out who funds kiongozi wa chama fulani cha siasa ambaye siku zote huishi hotelini tuu, and why?!. Utapata majibu!.

Kwa taarifa tuu, kwa msiojua, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote huko, hawakuipa ushindi, kwa sababu!. Ila pia amini usiamini uchaguzi wa 2015, CUF itashinda tena Zanzibar, lakini bado haitapewa ushindi, kwa sababu fulani genuine!, kwa vile hizo sababu zinazopelekea CUF ishinde siku zote na isipewe ushindi, zingalipo zipo, CUF wasipojishughulisha kuzijua, wataendelea kushiiki uchaguzi wa rais kwa kukimbiza upepo!. Ningekuwa mimi CUF, kwanza ningedeal na kuzijua hizo sababu za kwa nini huwa nashinda lakini kwa nini hawanipi ushindi wangu halali?!, nikijiridhisha kuwa this time sababu za kutopewa sasa hazipo tena, ndipo niingie kwenye uchaguzi wa urais, vinginevyo uchaguzi urais wa Zanzibar ni just a wastage of time, money and resources!.

Visa vya Zanzibar havikuishia hapo, kuna kisa kingine tena cha ndugu wawili, watoto wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. Chama fulani kikaamua kumzawadia nafasi ya urais mtoto mmoja kati ya hawa wanadugu wawili, uamuzi ukafikiwa, wa kuzawadiwa urais ule apewe kaka mkubwa. Sababu ya kumzawadia uais mtoto huyo, ni ili kuuenzi mchango wa marehemu baba yao, aliyekuwa rais wa Zanzibar, akitokea nchini Malawi!, licha ya Mmalawi huyu kutokuwa mzaliwa wala mwenye asili yoyote ya Zanzibar, lakini aliifanyia makubwa Zanzibar, hadi kujitoa uhai wake kuifia Zanzibar. Hivyo ule urais ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ya marehemu baba yao!. Ni kweli kaka mtu akaupata urais wa Zanzibar kwa mtindo ule ule wa bao la mkono, baada ya mshindi halisi kutotangazwa. Kaka mtu huyo akahudumu urais wa Zanzibar kipindi chote cha miaka 10!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, mdogo mtu naye akachukua fomu kumrithi kaka mtu akijua kuwa eti urais wa Zanzibar nao uendeshwe kama usultani!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza muda wa urais ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, itaonekana kuwa ni kweli chama chao kinaufanya urais wa Zanzibar ni sawa na usultani!, mdogo mtu akagoma na kuibuka na madai mazito!, kuwa eti kama urais ni wa zawadi kwa mtoto wa yule Mzee waliomuheshimu na kumuenzi, then "mtoto halisi aliyestahili urais ule ni yeye!", kwa hoja kuwa eti kaka yeke, ni mtoto tuu wa kufikia wa yule Mzee wao, akimaanisha mama alipokuja kuolewa baba yake, alikuja na mizigo ya watu wengine, ila baba alikubali yote kwa moyo mmoja na roho moja na ndio maana hata wakati alipoamua kuwasomesha wanae nchi kwao Malawi, aliwasomesha wote wawili bila ubaguzi wowote!.

Zanzibar haieshi vituko!, nataka niwashauri wajumbe wa bunge la katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa muungano na kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.

Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco
Pasco Mayalla unajidhalilisha, naanza kuwa na mashaka na mahala ulipopatia taaluma yako ya uandishi wa habari. Napata mashaka huenda wewe ni zao la makanjanja kwenye tasnia ya uandishi! Sielewi tafiti zako unafanyia wapi, kuna uwezekano huna weledi wa kuchagua relevant material kwa ajili ya kukusaidia kusupport fikra zako. Unakosa dira kila unapojitahidi kutaka kujenga hoja zako dhaifu kwa kuusingiza uislam!

Uislam na utamaduni wa kiislam huwezi kuufahamu bila kuusoma uislam wenyewe. Kosa mnalolifanya msiokua waislam ni kuzichukua kasumba mlizonazo dhidi ya uislam kupotoshana miongoni mwenu. Sio lazima kwamba mila za kiarabu ndio mila za kiislam.

Kwa kukusaidia tu, Waarabu baadhi yao mila zao ni kuabudu masanamu, katika imani ya kiislam kuabudu sanamu ni ushirikina. Asilimia kubwa ya uliyoandika juu ndoa ya kiislam ni uzushi na uongo ambao msingi wake ni ule ule kukashifu imani za watu kwa kutumia daraja la siasa. Kama huna facts kuhusu uislam ndugu Mayalla there are so many issues you can write about bila kuathiri imani za wengine
 
Back
Top Bottom