Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
- Thread starter
- #101
Jinsia zote mbili zina matatizo na matamanio yasiyo na mipaka. Hakuna kinachomridhisha mwanadamu na akaganda nacho mwanzo wa uhai wake hata mwisho. Binadamu ni mtu wa adventures bila kujali ubaya na uzuri wake. Ila kwa kuwa tuna akili na dhamira, mambo mengine tunayaonea haya, na wakati mwingine tunayafanya kwa uficho ili walimwengu wasitubaini.
Sijui kama kuna mtu ambaye yuko kwenye mapenzi kapata chaguo lake kwa asilimia mia kama alivyotaka iwe. Hakuna. Hapo ndio mwanzo wa matatizo. Kupewa mahitaji yote ya kibinadamu sio tiketi ya kumpenda mtu. Mwanamke anahitaji ulinzi. Sio ulinzi kama wa Ultimate security. Ulinzi wa kihisia, kimali, kimwili, n.k. Ulinzi wa kiroho atatoa Mungu. Mwanaume mmoja kutimiza yote hayo ni ngumu sana. Wapo ambao watakosa baadhi ya mambo fulani na watatulia kwa kuwa hawana jinsi. Wapo wanaotaka kila kitu na ndio maana unashangaa mwanamke anachapwa nje ya mahusiano.
La msingi ni ni kukubali kuwa si kila kitu unaweza kupata. Pia si kila kitu mwenza wako anaweza kukupatia. Gharama ya kupata hicho ulichokosa yaweza kuwa kubwa kuliko gharama ya kutokuwa nacho. Ni hayo tu
Well said mkuu.