Haya matabaka ya watawala na watwana ni mtaji mkubwa sana .
Vijijini ni mtaji mkubwa sana kwa politicians..Lakini mambo haya (ambayo tukiita ya kijinga hatujakosea) huwa yanatokea kutoka maeneo yenye umasikini mkubwa?
Angalia kwa mfano mkoa kama Kilimanjaro ambako huduma za kijamii mfano maji, barabara, mashule na hospitali zimetapakaa hadi vijijini hatuoni ujinga kama huu wakati wao ndio kama ni kuonyesha furaha ndio walipaswa?
Umasikini wa sehemu kama Lindi na Mtwara ambao ukiufatilia kwa undani miaka hii 60 tokea uhuru waweza KULIA MACHOZI kwa nini CCM ndiko inatumia propaganda hizi mfu?
Ila upande mwingine UBWEGE katika hili unarudi kwa waandaaji wa hilo onyesho. Kwani huyo mama hajui kuwa hapo watu wanalipwa kuigiza mbele yake? Kwamba anadanganywa yeye kuwa wanafuraha kumbe wanafurahia kupata hivyo vitenge na hela ya sukari siku mbili tatu?
Anajua yote na alipaswa kuyakataa, kupakwa mafuta na mgongo wa chupa na unachekelea na kupiga makofi ni aina fulani ambayo jina lake halipendezi!



