Hiyo nafasi siku zote ni lazima ishikiliwe mtu ambaye kwanza ni kada mtiifu wa CCM; manbo ya umahiri katika usimamizi wa utoaji taaluma na kufanya tafiti siyo muhimu sana.
Baada ya Pius Msekwa kutoka UDSM (kama VC) katikati ya miaka ya 70, aliteuliwa kuwa katibu mtendaji wa CCM na nafasi yake ikachukuliwa na Ibrahim Kaduma ambaye kabla alikuwa waziri wa mambo ya nje. Kaduma alifuatiliwa na Nicolaos Kuhanga ambaye kabla alikuwa waziri wa elimu. Prof Goefrey Mmari alimrithi kwa muda mfupi sana Kuhanga kabla hajaondolewa kutokana na "kutokuweka maslahi ya chama mbele chuoni".
Mmari alifuatiwa na "makada shupavu" Prof Mettew Luhanga na hatimaye Mukandala. Miaka ya 80 mwanzoni Mukandala alikuwa mwenyekiti wa CCM tawi la UDSM.
Wakati Pius Msekwa akiwa bado VC UDSM, ndipo alipoandika kitabu "Towards Party Supremacy"; na mawazo yake kwenye hiki kitabu yalitumika sana katika kuandaa mpango wa kuifanya CCM ishike hatamu za dola na uongozi wa nchi (chama dola). Huu uchama dola wa CCM ulihalalishwa kikatiba na bado unaendelezwa chini ya katiba ya sasa.
Baada ya Pius Msekwa kutoka UDSM (kama VC) katikati ya miaka ya 70, aliteuliwa kuwa katibu mtendaji wa CCM na nafasi yake ikachukuliwa na Ibrahim Kaduma ambaye kabla alikuwa waziri wa mambo ya nje. Kaduma alifuatiliwa na Nicolaos Kuhanga ambaye kabla alikuwa waziri wa elimu. Prof Goefrey Mmari alimrithi kwa muda mfupi sana Kuhanga kabla hajaondolewa kutokana na "kutokuweka maslahi ya chama mbele chuoni".
Mmari alifuatiwa na "makada shupavu" Prof Mettew Luhanga na hatimaye Mukandala. Miaka ya 80 mwanzoni Mukandala alikuwa mwenyekiti wa CCM tawi la UDSM.
Wakati Pius Msekwa akiwa bado VC UDSM, ndipo alipoandika kitabu "Towards Party Supremacy"; na mawazo yake kwenye hiki kitabu yalitumika sana katika kuandaa mpango wa kuifanya CCM ishike hatamu za dola na uongozi wa nchi (chama dola). Huu uchama dola wa CCM ulihalalishwa kikatiba na bado unaendelezwa chini ya katiba ya sasa.