Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Mkuu, nakubaliana na wewe kuwa serikali haitaanguka, lakini kinachoendelea hapa Dodoma si mchezo wa kuigiza hata kidogo. Nilichokibaini baada ya kufuatilia kwa karibu kuwa tunayoyashuhudia ni matokeo ya makundi ambayo CCM ilishindwa kuyazika. Wapo wabunge ambao kwa dhati kabisa wamedhamiria kuliangusha baraza la mawaziri na serikali nayo, ikiongozwa na Lukuvi, inahaha kuhakikisha hilo halitokei. Tatizo wanalokumbana nalo hao wanaotaka kuiwajibisha serikali ni kuwa mpaka hivi sasa hajapatikana mwenye ujasiri wa kuleta hoja binafsi ya kutokuwa na imani ya baraza la mawazi.Tupunguze hisia wakuu, mbona tunakuwa kama hatuijui nchi yetu!?
Kinachoendelea dodoma ni igizo la wabunge wa ccm kutaka kuwahadaa wananchi wajinga ili waone bado ccm ni chama chao na kwamba wabunge wa ccm pia wanajua kubwata!
Hamna wa kuangusha serikali pale, tunachokitaka toka kwa wabunge wa ccm ni kikubwa kuliko uwezo wao wa kutenda kwa mazoea!
Sisi tulioelevuka japo kidogo tukianza kulewa hisia utafikiri kinachotokea bungeni ni kipya sana ndo tutawayumbisha masikini wengine kuona uh kumbe hata wabunge wa ccm wanafanya kazi wakati hamna chochote walichofanya mpaka sasa.
Tuwaangalie mwisho wao kwanza
Lakini hata hivyo, kwa kuona kuwa wasipochukua hatua lolote linaweza kutokea, mchana huu CCM imewaita wabunge wake wote kwenye kikao chao. Huko ndani nasikia wamemwambia Pinda amwambie JK afukuze mawaziri kadhaa na mtendaji wa TRA. Kama haiwezekani, basi Pinda ajiuzulu, serikali ivunjike ili iundwe upya. Kikao chao bado kinaendelea na tupo hapa tunafuatilia