Kwahiyo unataka kusema tukate BibliaKutoa fungu la kumi ni agizo la agano la kale ikumbukwe hili lilikuwa sharti la kila mwenye kupata zao au mfugo alete sehemu ya kumi ya pato hekaluni (mambo ya walawi 27:30; hesabu 18:26; kumbukumbu la torati 14;24; mambo ya nyakati ya pili 31:5).
Agano jipya halina pahala linazungumzia fungu la kumi. Ila fahamu tu 10th ni biblical
Hata wale wanafunzi walileta 'sehemu' ya walichokuwa nacho...rejea simulizi ya Anania na Safila...nk nk
Unamdanganya mwenzio! Hiyo itakuwa ni sadaka! Fungu la kumi au Zaka hupelekwa kanisani!Mkuu hata ukitoa kwa wahitaji ambao wasiojiweza ni sawa tuu.
Habari zenu wakuu, hongera kwa kila anayewajibika muda huu pia kwa wanaopumzika katika staili zao wajuazo wao.
Naomba nisivute muda na wakati muhimu kama huu.Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naomba mjadiliane ni namna gani nzuri ya kutoa fungu la kumi?
Je, ni lazima kanisani, au hata kusaidia watu kwa ile asilimia kumi ni sawa? Na kwanini tunatakiwa kutoa fungu la kumi kanisani.
Sina ushahidi wa namna yoyote ya kutoa fungu la kumi kwa kutumia maandiko ya biblia ila nataka kujua kwa wanaojua tujuzane umuhimu katika kujua namna sahihi ya kumtolea bwana fungu la kumi.
Karibuni wote.
Kwani fungu la kumi sio sadaka??Unamdanganya mwenzio! Hiyo itakuwa ni sadaka! Fungu la kumi au Zaka hupelekwa kanisani!
EXACTLY..... there you are MkuuSomo la matoleo au sadaka limerugwa sana maana ndipo zilipo ofisi za wahusika hapo.
Kifupi kabisa ni kuwa, Mungu amefanya kazi na wanadamu kwa namna nyingi na amekuwa akibadili utaratibu mara kwa mara.
Hapo zamani kabla ya Yesu, wayahudi waliamriwa kutoa matoleo ya namna mbalimbali na kila matoleo yalikuwa na kazi mahususi. Yalikuwepo fungu la kumi, ahadi, malimbuko(mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu, mnyama, ndege na mazao) sadaka za unga, za dhabihu na mengine mengi.
Waisrael waliamriwa kutoa yote na ilikuwa amri kutoa yote hayo.
Lakini mara baada ya Yesu kuja, Mungu alimtoa mwanae kuwa sadaka ya pekee ili kuzifuta sadaka nyingi zilizotolewa na waisrael nyakati zile.
Hivyo ni kusema, nyakati za Yesu hakuna fungu la kumi, hakuna zaka, hakuna ahadi, hakuna malimbuko, hakuna sadaka za dhabihu n.k.
Kitu pekee kilichosalia ni michango/sadaka kwa kadri mtu alivyofanikiwa kwa ajili ya kusogeza mbele injili ya Kristo. Imeandikwa katika 1kor16:1-3. Changizo ni kwa ajili ya watakatifu na si vinginevyo.
Na watakatifu inafanyika kwa namna mbili.
1. Wapo tayari watakatifu ambao lazima hukutana kwa ajili ya Bwana. Ili shuguuli mbalimbali za kumwabudu Mungu zifanikiwe, ni changizo ndiyo hutumika. Lakini pia, miongoni mwa watakatifu, iwapo yeyote ana shida, basi kanisa kupitia changizo lapaswa kumsaidia.
2. Namna ya pili ni ya kitume zaidi. Kuwatafta watakatifu zaidi. Kutoa kwa yatima na wajane au yeyote mwenye kuhitaji ni kuhubiri na ni chanzo cha watu kumrudia Mungu. Kufadhili shughuli za uinjilist ndio kazi kubwa tuliyoachiwa.
Kifupi ni kuwa, sisi sote tu makuhani wa Bwana Yesu. Iwapo wote ni makuhani, haipaswi mtu yeyote aishi kwa jasho la mtu mwingine. Inatakiwa kila mtu afanye kazi ya kumpatia kipato ili awe na uwezo wa kumtumikia Mungu kwa nguvu, akili na moyo pia. Siyo kusubiri michango ya waumini kujilipa posho au mishahara.
Imeandikwa, mchungaji wa mshahara, huyo si mchungaji.
"Kupata riziki kwa njia ya Injili" ni lazima iwe kwenye fungu la kumi?Yachunguze maandiko mkuu upate maarifa sahihi .
1 Corintho 9:13,14
"Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekaluni, na wale wahudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?, Na Bwana vivyohivyo ameamuru (COMMAND) wale waihubirio injili wapate riziki kwa hiyo injili"
Ni agizo la Yesu (Bwana aliyemuamuru paul) hao watu wa injili wale katika injili.
Peleka zaka kanisani, watumishi wapate chakula cha kututumikia mkuu.
Hii inawahusu wale ambao maisha yao 100% wameyatoa kwa ajili ya injili na sio kazi nyingine.
Ikiwa wapo matapeli Mungu ndiiye Muhukumu atawashughulikia.
Mmelishwa matangopori makali Sana mpaka mnatia hurumaWakristo hawapendi kujifunza Neno, yaan shetan kabana Fikra ktk hili,
Tunapenda kubishana kuliko kukaa na kusikiliza.
Kumbuka huwez jua kila kitu, unachojua wewe mwingine hajui, na anachojua mwingine wewe hujui
Tuwe tunatafuta muda wa utulivu na kusoma Maandiko hii mikanganyiko ya sadaka isingekuwepo
Fungu la 10, ni la walawi waliambiwa watakula madhabahuni.
Huko yatima wajane tafuta sadaka nyingine upeleke na sio fungu la kumi
Na katika fungu la kumi hakikisha hutoi hata sent moja ukaila ukasema nitairudisha
MUNGU anasema leteni zaka kamili ghalani mwangu
Kamili na sio nusu, ukipeleka nusu sawa sawa na zero
Shida tumeweka watumishi wanakula na hii ni kwasababu ya wachache wanao tumia mlango wa dini vibaya
Lakin ukikaa na Mungu vzr utajua hapa ni sahihi ama la?
Sipo kuhukumu watumishi wa Mungu, Mungu ndio atawahukumu kwakuwa nI watu wake
Lakin ukitoa sadaka usiitupe ipeleke na Neno ndani yake iombee hutoona hasara ya kumrudishia Mungu alichokupa
Zaka ni sadaka yenye ahadi
Katk zaka ndipo ambapo Mungu anasema nijaribu uone kama sitofungua madirisha
Ktk baraka kuna baraka nyingi
Katika zaka Mungu analinda hata ulicho nacho kisipukutike kisiharibike
Wala muharibu asiharibu unachopatia pesa
Soma malaki 3
Ukila fungu la 10 ni laana, tena inatoka kwa Mungu
Unaweza ukapigwa kwenye uchumi sana
Utamkemea shetan kumbe hausiki
Ktk fungu la kumi usipo itoa Mungu anakuita mwizi umemuibia
Fungu la 10 sio lako haijalishi ni sh ngapi
Hata kama ni sh 10, usiseme ndogo
Tii peleka kwa Mungu, ni bora uzidishe kuliko kupunguza
Mungu awabariki
peleka fungu la kumi kanisani, watumishi wapate cha kula.
fungu la kumi ni tofauti na sadaka, hiyo unatoa popote.
hata kama wanafuja, Mungu anajua jinsi atakavyowashughulikia ila wewe baraka zao ziko palepale.
malaki 3:10
Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
Zaka ni sawa na fungu la 10, huwekewi kiwango cha kutoa zaka sababu vipato vinatofautianaZaka na fungu la kumi ni sawa/kitu kimoja?
Kiwango kilipangwa na watu au kimetoka kwenye maandiko?
Naomba kujuzwa
mkuu hiyo unatowaga sadaka siyo fungu la kumi, fungu la kumi ni sehemu ya MUNGU kwenye mapato yako hivyo ni lazima uipeleke kanisani.Binafsi napenda na ninajisikia faraja pale ninapo toa fungu la kumi kwa wasio jiweza, wagonjwa, walemavu napia watoto yatima. Zaidi ya hapo, nadhani imani ya dini yako (Msahaf/biblia) pamoja na utashi ni jambo kubwa na muhimu ili kukuongoza kwenye kile unacho kiamini.
pole Sana mkuu, MUNGU akusaidie.Namna nzuri ni kufungua account na kusave kwaajili ya watoto wako au kununua usafiri...ni fungu la 10 tosha, mengine ni watu wazima wanataka uwalishe familia zao kisa tu wamekariri mistari ya biblia.
changizo sio zaka. kama mkiamua kufanya changizo ni jambo jema zaidi."Kupata riziki kwa njia ya Injili" ni lazima iwe kwenye fungu la kumi?
Kwani mchungaji hawezi kupata Hiyo riziki kupitia Changizo /Sadaka za kawaida?
Unaweza kunionesha POPOTE PALE mitume wa Yesu including Paulo walipopokea Zaka?
Nilivyosema kiwango nilimaanisha 1/10.Zaka ni sawa na fungu la 10, huwekewi kiwango cha kutoa zaka sababu vipato vinatofautiana
Anayepata elf1, na elf 10 kwa siku huwez waambia watoe kiasi kinacho fanana
Mmoja atatoa sh 100, mwingine 1000
Anayepata laki kwa mwez ni tofauti na anayepata milion kwa mwezi
Ukipangiwa kiasi cha kutoa huo ni mchango na utaratibu wa sehemu husika unayo abudu
Ili wafikie malengo waliyo yaweka kutokana na taratibu za mahali husika
Na ukifika ktk mchango usitoe pia kama unatupa semea neno