mi nilianza kutumia mwaka 2002, zilikuwa computer za shule, shule nzima tulikuwa watu 9 tu ndo tuliokuwa tunasoma somo hilo na mwaka huo huo ndo nikaanza kutumia internet, nilifungua email nyingi, moja ilikuwa ya hotmail moja ya ganja na nyingine ya yohoo, internet nilikuwa naenda kuchati maana miaka ile yahoo massanger ndo ilikuwa inabamba sana, unaenda kwenye chating room then unachagua room unayoipenda, ukimkuta yoyote online unaanza kuchati naye, story kama kawa, pale ndo vifupisho vya maneno vilianza kutumika, ASL PLZ manaake ilikuwa age sex and location, tulikuwa tunaenjoy, kuna wakati nilikuwa nafungua ID za kike afu nawachokoza watu walikuwa wanajielezaje, ilikuwa raha sana