Ni mwaka gani ulitumia computer kwa mara ya kwanza?

Ni mwaka gani ulitumia computer kwa mara ya kwanza?

Mimi nilianza kutumia Computer 1999 nilikuwa interested tu kujua Computer,kuna jamaa alifungua chuo chake mtaani mie nikawa mwanafunzi wa kwanza,ilikuwa ni desktpo aina ya Compaq windows 98.
 
Yeah, i guess ilikuwa windows 3.1 or 3.11 maana windows 95 ilikuja late 1997/8 ni karibu na kipindi kile ambacho lazima uvue viatu kuingia kwenye chumba cha computer na mikono iwe misafi.....computers zisipate vumbi au virus, ha ha ha. tumetoka mbali sana, what i have been doing those days and ninachofanya sasa kwenye hii field no tofauti kabisaaa:tape:
aise hata uelewa wa window miaka hiyo haukuwepo kabisa.
 
ulinizidi mwaka mmoja tu mm nilianza kutumia DOS mwaka 1996 nilisoma shule ya sanaa na ndipo tulipofundishwa kutumia hapo na tulijifunza kwa kufungua WINDOW kwa DIR/US/............... hapo nimesahau kidogo kwani ndo iilikuwa njia pekee ya kustart dos

Hiyo command ndio njia pekee ya kustart DOS? aisee.
 
2004 enz hzo hata kula nilikuwa sil kwa ajil ya game.
 
Nilianza 2008 ==> OS ya Win XP ==> Computer ya Desktop (Chogo) ==> Tulikuwa ukiingia kwenye "'COMPUTER ROOM'" ni kuchora kwenye 'PAINT', Ku_change settings kama za wallpaper, creating user accounts n.k, Hahahah!
 
Ilikuwa mwaka 1998 rafiki yangu 5Dalikuwa anasoma uganda alipokuja likizo akanipeleka sayansi na technologia kulikuwa na cafe na ilikuwa mara ya kwanza kuona computer na akanifungulia email wakati sikuwa najua nini maana yake
 
Nilianza 2008 ==> OS ya Win XP ==> Computer ya Desktop (Chogo) ==> Tulikuwa ukiingia kwenye "'COMPUTER ROOM'" ni kuchora kwenye 'PAINT', Ku_change settings kama za wallpaper, creating user accounts n.k, Hahahah!

computer ya desktop (chogo) ndio ipi iyo
 
ukiangalia movie za fbi, cia nikawa nawaza hawa jamaa windo zao sijui zikoje, mtu akigusa tu button unaona yanatokea ma code yanapanda juu fasta

hv Ile Nikitu Gan?? mm Mpaka Leo Sjuiii


via Ushamba Wangu
 
2007, kumiliki ya kwangu kabisa ilikuwa 2010
 
2003
Prince of persia na arrows
Na disket 1.4 mb..ajabu kwel kwel..
Mwalim wa compter anatuonyesha flash tunaona ajaabuuu
 
Ni mwaka gani ulitumia computer kwa mara ya kwanza?

1990 lakini sana sana nilikua nacheza gemu tu (snakers, pacmen, n.k) Kipindi hicho tulikua tunatumia DOS kwenda mbele..
 
2003
Prince of persia na arrows
Na disket 1.4 mb..ajabu kwel kwel..
Mwalim wa compter anatuonyesha flash tunaona ajaabuuu



Hivi hili game ujaligusa kabisa? maana ndilo lilikuwa likibamba kinoma kushinda hilo la kupasua maputo
 
Last edited by a moderator:
1999 nilikuwa napiga game tu za magari na pikipiki. enzi za floppy disc,tumetoka mbali.flopy disc zilikuwa noma unaweza kusave kazi yako ukienda kuiprint inagoma kufunguka!ukishika flopy na optical disc mkononi unaonekana matawi ya juu, ndio zilikuwa swaga za kitaaa
 
Ni mwaka gani ulitumia computer kwa mara ya kwanza?

Mara yangu ya kwanza kutumia computer ilikuwa mwaka 1989 pale UDSM faculty of Commerce. Computer ilikuwa mojawapo ya subject wakati huo tukifundishwa na Marehemu Mgaya. Alitufundisha computer programming na wengi tulikuwa tunamshangaa.
Wakati ule kuingia computer laboratory ilikuwa lazima kuvua viatu, sijui ilkuwa ni kwa nini tulikuwa tunalazimishwa kuvua viatu.

Tiba
 
Basi wakati huo tulikuwa tunavua viatu, mara ya kwanza hata kuigusa mouse sikuruhusiwa. Nilikuwa natazama tu. Jamaa alikuwa hataki niguse ntaharibu. Leo naikorokochoa iyo iyo pc kama sina akili vile, kaazi kwelikweli
 
Back
Top Bottom