Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 2,786
- 7,567
Wakuu,
Ni miezi mitatu sasa (siku 92 tukiwa precise) toka Samia afanye uteuzi wa Tume ya Kuchunguza 'matukio' ya Oktoba 29, 2025, akisema hajui kwanini tuliandamana kugomea uchaguzi, wa kina nani waliua watu vile na kwa amri ya nani
Dunia ina mambo, anyhu....
Hii inamaanisha wakati wowote kutoka sasa tume itakuja mbele kutueleza nini kilitokea pamoja na kutoa mapendekezo yao, ili "KULIPONYA TAIFA".
Toka uchaguzi ufanyike, kesi ya Lissu inayoendelea, viongozi 'wa mchongo' kuapishwa, comments za Samia na viongozi wengine juu ya hali ya usalama nchini, mashambulizi kwa viongozi wa dini hasa Wakatoliki, figisu zinazoendelea kwa CHADEMA, matukio ya polisi kuendelea kukamata watu bila kufuata taratibu na sheria, viongozi kusema "Maridhiano ni Hiyari" huku wakisema hatuwezi kusonga mbele kuridhiana, "WHO ARE YOU"......
Unadhani Tume ya Chande itakuja na matokeo gani? Kutakuwa na mwangaza wa maridhiano na kuponya majeraha ya Watanganyika kutokana na mauaji ya raia? Usalama utarejea nchini hata waliokimbia makazi yao kwa kuhofia usalama wao waweze kurejea nchini bila wasiwasi? Vipi kuhusu waliokamatwa mpaka sasa wakishikiliwa kwa kosa la "Uchochezi"? Viongozi watapata legitimacy ya kuendelea kutawala? Polisi kukamata raia ovyo bila kufuata utaratibu itakoma? Lissu ataachiliwa huru na CHADEMA kuendelea na shughuli zao? Kubwa zaidi Polisi WALIOUA raia watawajibishwa?
Nini matarajio yako juu ya Tume hii ya Uchunguzi?
Ni miezi mitatu sasa (siku 92 tukiwa precise) toka Samia afanye uteuzi wa Tume ya Kuchunguza 'matukio' ya Oktoba 29, 2025, akisema hajui kwanini tuliandamana kugomea uchaguzi, wa kina nani waliua watu vile na kwa amri ya nani

Dunia ina mambo, anyhu....Hii inamaanisha wakati wowote kutoka sasa tume itakuja mbele kutueleza nini kilitokea pamoja na kutoa mapendekezo yao, ili "KULIPONYA TAIFA".
Toka uchaguzi ufanyike, kesi ya Lissu inayoendelea, viongozi 'wa mchongo' kuapishwa, comments za Samia na viongozi wengine juu ya hali ya usalama nchini, mashambulizi kwa viongozi wa dini hasa Wakatoliki, figisu zinazoendelea kwa CHADEMA, matukio ya polisi kuendelea kukamata watu bila kufuata taratibu na sheria, viongozi kusema "Maridhiano ni Hiyari" huku wakisema hatuwezi kusonga mbele kuridhiana, "WHO ARE YOU"......
Unadhani Tume ya Chande itakuja na matokeo gani? Kutakuwa na mwangaza wa maridhiano na kuponya majeraha ya Watanganyika kutokana na mauaji ya raia? Usalama utarejea nchini hata waliokimbia makazi yao kwa kuhofia usalama wao waweze kurejea nchini bila wasiwasi? Vipi kuhusu waliokamatwa mpaka sasa wakishikiliwa kwa kosa la "Uchochezi"? Viongozi watapata legitimacy ya kuendelea kutawala? Polisi kukamata raia ovyo bila kufuata utaratibu itakoma? Lissu ataachiliwa huru na CHADEMA kuendelea na shughuli zao? Kubwa zaidi Polisi WALIOUA raia watawajibishwa?
Nini matarajio yako juu ya Tume hii ya Uchunguzi?

