Ni mapema mno kumnyooshea kidole mheshimiwa Rais, Tumpe muda!

Vipi kuhusu bei ya mbolea, bei ya Petrol?

Unajua Rais wa Zanzibar amefanya mengi kwa muda mfupi. Maelewano na Cuf, kaiunganisha Zanzibar. Ana sera zinazoeleweka (Blue Economy) mikakati ya ukweli kuwavutia wawekezaji na Wazanzibari diaspora na kuweka mazingira mazuri wafanyabiashara, utalii, kilimo cha kisasa, miundombinu, utalii.

Mchapa kazi mwenye maono, malengo,dira, uthubutu na kasi. Watu wanawajibishwa wasipowajibika.

Matokeo yanaonekana wazi.

Lakini Huku bara dah?
Usisahau kuwa na Mama anamuunga mkono au niseme anaig'arisha sana Zanzibar. Si umesikia kero zaidi ya 10 zimepata ufumbuzi ndani ya muda mfupi
 
ACHEN KUMDEKEZA

MPE MUDA MPE MUDA NN???

HUYO NI MTI MZIMA ANA AKILI TIMAMU.


HAFAI, HAFAI NA HAJAWAHI KUFAA KUA RAIS.



2025, VYOMBO VYA DOLA, KAMA MMESHINDWA SANA KUACHA WANANCHI WACHAGUE, BASI MSITULETEE MTU WA AINA HII KUPITIA CCM.
Shangwe la wakulima wa mazao mbalimbali baada ya bei kupaa ni kwa mama tu.Hayo ya ujinga wa kina Mbowe bakini nayo nyinyi washikiwa akili.
 
Usisahau kuwa na Mama anamuunga mkono au niseme anaig'arisha sana Zanzibar. Si umesikia kero zaidi ya 10 zimepata ufumbuzi ndani ya muda mfupi

Ni kweli, lakini tangu wakati wa JPM mentality, speed yake ilikuwa hiyo hiyo. Mchaka mchaka. Hata angekuwepo JPM sidhani kama angekuwa tofauti, labda speed zaidi.

Yale yanayofanyika Zenji yangeweza na yanaweza kufanywa bara kama Mwinyi angekuwepo huku.

It should be win-win situation for both countries. Kuna keki kubwa tu ya kutosha na maslahi, rasilimali, interests, na uchumi unaotegemeana.
 
Kodi ya majengo imewalenga wanaotumia umeme kupitia TANESCO, je wale wanaotumia solar na wale wa karabai, vibatari, kandiri n.k. wanalipiaje majengo yao?
 
UPUUZI MTUPU!
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

Suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
 
Namuelewa sana MAMA, ila anahitaji kufumua safu ya juu ya uongozi kwa baadhi ya vyombo vyetu vya ulinzi...wanamuangusha na hajui
Hana ubavu huo. Hao ndiyo wanamfanya aendelee kubakia madarakani. Akiwagusa itakula kwake
 
Kuna msemo usemao "mvinyo mpwa kwenye chupa ya zamani"."New wine in old bottle".hicho ndiyo kinachoendelea awamu sita Hawa wasaidizi wa Rais ni vigegeu,bendera fuata upepo na hawana misimamo, watamuangusha. Mama awe mwangalifu Sana,hawamtakii mema.
Ambao wanakwamishwa awaweke pembeni ili kazi iendelee.
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

Suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
Huu ni upuuzi wa kiwango cha juu sana.
 
Kuna msemo usemao "mvinyo mpwa kwenye chupa ya zamani"."New wine in old bottle".hicho ndiyo kinachoendelea awamu sita Hawa wasaidizi wa Rais ni vigegeu,bendera fuata upepo na hawana misimamo, watamuangusha. Mama awe mwangalifu Sana,hawamtakii mema.
Ambao wanakwamishw awaweke pembeni ili kazi iendelee.


Wewe ndio President, Commander in Chief, final decision maker with tremendous exucutive power. Kwahiyo unatakiwa uwe na uwezo wa kuamua ushauri gani uuchukue, upi uuache.

Unapokea ushauri, mapendekezo. Kazi yako uliojiriwa na Watanzania ni kutoa maamuzi ya mwisho. Hicho ndicho kitu kikubwa, kuisimamia serikali yako, kuamua.

Sasa kila siku unasikia wasaidizi wanamkwamisha, wanamuhujumu, wanamyumbisha,hawana msimamo.

Wao wanafuata msimamo wa Rais wao. Kama ya Rais amesimama na wao watasimama au kusimamishwa.

Kama anayumba na wenyewe watayumba. Unafikiria wanafanyaje maamuzi kama haya kodi na tozo mpya nne kwa kipindi cha miezi miwili zinazogusa directly vitu na huduma muhimu kwa Jamii.

Kweli hatuna ubunifu, wa kuongeza mazao tunayolima, kutumia vifaa na mbinu za kisasa, kuzifanya balozi zetu kazi yao kubwa kabisa kuwa kutangaza utalii, bidhaa zetu, madini, kutafuta masoko, fursa zinazopatikana nchini za kibiashara, uwekezaji.

Hapo naona balozi wa China na Comoro wanajitahidi wengine hatusikii chochote. Inabidi kuchagua Mabalozi wemye weledi na kuwapa maelekezo kazi zao ni zaidi ya kuimarisha mahusiano.
 
Kodi ya majengo imewalenga wanaotumia umeme kupitia TANESCO, je wale wanaotumia solar na wale wa karabai, vibatari, kandiri n.k. wanalipiaje majengo yao?
Wanaotumia solar wanalipa kupitia benki au kwa njia ya mtandao kama m-pesa, tigo-pesa n.k
 
Nianze na suala la kukamatwa kwa kiongozi wa upinzani bw. Freeman Aikael mbowe

kukamatwa kwa kiongozi huyo wa upinzani kwa tafsiri ya kisiasa inaweza kuonekana ni agizo kutoka juu ili kudhoofisha upinzani au kukwamisha mapambano ya kudai katiba mpya.

Lakini ukweli ni kuwa kukamatwa kwa mbowe ni uamzi wa jeshi la polisi chini ya IGP sirro ndio maana kwenye hotuba ya juzi mheshimiwa Rais alimsisitiza sana pamoja na mifumo ya utoaji haki yaani 'mahakama' na 'DPP' kufuta kesi na mashauri yote ambayo hayana ushahidi wa kutosha kwani haya mambo yote kwa ujumla wake yanaidhalilisha serikali na kumchafua Rais na kwakuwa jambo lenyewe limeshafika mahakamani, Rais hawezi kuliingilia kwahiyo tuiache mahakama ifanye kazi yake na haki itatendeka.

Suala la kodi ya majengo
kodi ya majengo huwa ipo wala haijaanzishwa na mheshimiwa Samia. Kilichobadilika ni namna tu ya kufanya malipo. kwamba badala ya kulipa kwa mkono 'cash' kwa sasa tunailipa kidigitali kwa mfumo wa LUKU. Na, huu mfumo wa LUKU ni mzuri kwa sababu unasaidia kupunguzia wananchi mzigo kwamba badala ya kulipa 12, 000 au 60, 000 kwa mkupuo kwa sasa tuna lipa kwa kukatwa kidogo kidogo kwa mwezi. Pia mfumo huu unasaidia kupunguza hadha ya watu kusafiri umbali mrefu kwenda ofisi za TRA kufanya malipo. Vilevile unasaidia kudhibiti ukwepaji kodi kwa watu ambao sio waaminifu na wazalendo.

Tozo ya miamala ya simu
Mheshimiwa Rais anajua kazi nzito iliyoko mbele yake. Anajua kuna miradi mikubwa iliyoanzishwa inahitaji kuendelezwa, anajua watumishi wa umma wamenyimwa haki yao ya kupandishiwa mishahara kwa kipindi kirefu, anajua kuna changamoto katika huduma za afya na elimu, anajua kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira kwa vijana. Lakini changamoto zote hizi atazitatuaje bila ya kuwa na pesa?

Ndio maana kwa mapenzi mema, mheshimiwa Rais pamoja na serikali yake wakaamua kuanzisha kodi ya kizalendo 'solidarity fund' kupitia miamala ya simu ili pesa itakayopatikana ikasaidie kutatua changamoto hizo lakini bado watu wanalaumu? HAPANA tumpeni muda Rais afanye kazi na matokeo tutayaona.
Bonge la pambaf
 
Kodi ya majengo imewalenga wanaotumia umeme kupitia TANESCO, je wale wanaotumia solar na wale wa karabai, vibatari, kandiri n.k. wanalipiaje majengo yao?

Watatumia mfumo wa zamani obviously. Naipongezwe hii mbinu ya ukusanyaji kodi, kinachotakiwa ni maboreshe na kuhakishi mpangaji asiye na nyumba na wenye exception wazee halipishwi, hivyo tu.
 
Back
Top Bottom