Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Tanzania inashindwa kuendelea kwa sababu ya kuweka madarakani viongozi wenye damu ya Utumishi wa umma na kushindwa kuweka mchanganyiko wa Watumishi wa umma na wafanyabiashara. Ntatoa mfano kwa awamu zote sita zilizowahi kuwepo kwenye utawala
Historia ya Mwalimu alikuwa Mtumishi wa Umma kwenda kwenye siasa na baada ya Urais, wasaidizi wake nao hivyohivyo. Akaja Mzee Mwinyi na safu yake nayo ikawa Watumishi wa umma
Mzee mkapa alipoingia akaja na Watumishi wa umma akina Mhe.Sumaye na Mhe Gharab Bilal, akakabidhi nchi kwa JK naye pure civil servant pamoja na Mzee Lowasa na Pinda.
JPM akaingia na safu accademician kila sekta na hivyo kila jambo kwao likawa linahitaji principles na urasimu mwingi wakiamini wanaibiwa. Hakuna mindset za kujua risk Ni sehemu ya mfumo wa uendeshaji nchi.
Mhe. Samia ameingia ukiangali safu yake yote Ni wanasiasa na wanataalumu hakuna wafanyabiashara. Na hakuna mtu anashtuka kwanini nivigumu sisi kusonga mbele.
Watumishi wa umma Ni watu wenye mindset za kimaskini (sory to say but that is reality). Watumishi wa umma Ni watu Wana mawazo yakuingia nakutoka ofisini kulingana na muda uliowekwa lakini siyo watu wakuingia kazini kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya mwajiri wake. Ni watu wanaoweza kukata kufanya Jambo flani bila sababu na hakuna wakuwalazimisha kufanya. Kauli mbiu ya Watumishi wa umma Duniani kote ni " HIZI KAZI ZIPO TU NA TUMEZIKUTA CHAKUFIA NINI?" Hii Ni kauli ambayo utolewa na viongozi wa kitaifa wanapokuwa faragha au wanapokaa na watendaji wao wa chini. Kauli namba mbili ya Watumishi wa umma ni USILIE KULIKO MFIWA, kwamba fanya usifanye almradi hakuna athari kwenye mshahara wako Basi nyamaza usipomhudumia atahudumiwa na wengine.
Kinyume chake wafanyabiashara ni watu wameumbwa kutafuta fursa mpya kila siku na kuchukua risk kama sehemu ya kazi yake. Mfanyabiashara anajitathimini amefanikiwa vipi na namna gani anaweza kuvuka hatua kwenda mbele
Sisi Tanzania kukosa wafanyabiashara kwenye mfumo wa uongozi madhara yake nikudumaa kwa akili. Mtu anastaafu katika nafasi kubw nchini lakini uoni mradi wake binafsi anaosimamia, anachoweza nikusubiri Mhe. Rais amteue mwenyekiti wa bodi au mkuu wa taasisi flani Basi. Tungekuwa na wafanyabiashara Leo hii wasingekaa nyumbani baada ya kustaafu wasubiri kuonewa huruma.
Tubadili mfumo tuchanganye wenye mawazo tegemezi (Watumishi) na wasio na mawazo tegemezi wenye uwezo wa kujisimamia (wafanyabiashara)
Historia ya Mwalimu alikuwa Mtumishi wa Umma kwenda kwenye siasa na baada ya Urais, wasaidizi wake nao hivyohivyo. Akaja Mzee Mwinyi na safu yake nayo ikawa Watumishi wa umma
Mzee mkapa alipoingia akaja na Watumishi wa umma akina Mhe.Sumaye na Mhe Gharab Bilal, akakabidhi nchi kwa JK naye pure civil servant pamoja na Mzee Lowasa na Pinda.
JPM akaingia na safu accademician kila sekta na hivyo kila jambo kwao likawa linahitaji principles na urasimu mwingi wakiamini wanaibiwa. Hakuna mindset za kujua risk Ni sehemu ya mfumo wa uendeshaji nchi.
Mhe. Samia ameingia ukiangali safu yake yote Ni wanasiasa na wanataalumu hakuna wafanyabiashara. Na hakuna mtu anashtuka kwanini nivigumu sisi kusonga mbele.
Watumishi wa umma Ni watu wenye mindset za kimaskini (sory to say but that is reality). Watumishi wa umma Ni watu Wana mawazo yakuingia nakutoka ofisini kulingana na muda uliowekwa lakini siyo watu wakuingia kazini kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya mwajiri wake. Ni watu wanaoweza kukata kufanya Jambo flani bila sababu na hakuna wakuwalazimisha kufanya. Kauli mbiu ya Watumishi wa umma Duniani kote ni " HIZI KAZI ZIPO TU NA TUMEZIKUTA CHAKUFIA NINI?" Hii Ni kauli ambayo utolewa na viongozi wa kitaifa wanapokuwa faragha au wanapokaa na watendaji wao wa chini. Kauli namba mbili ya Watumishi wa umma ni USILIE KULIKO MFIWA, kwamba fanya usifanye almradi hakuna athari kwenye mshahara wako Basi nyamaza usipomhudumia atahudumiwa na wengine.
Kinyume chake wafanyabiashara ni watu wameumbwa kutafuta fursa mpya kila siku na kuchukua risk kama sehemu ya kazi yake. Mfanyabiashara anajitathimini amefanikiwa vipi na namna gani anaweza kuvuka hatua kwenda mbele
Sisi Tanzania kukosa wafanyabiashara kwenye mfumo wa uongozi madhara yake nikudumaa kwa akili. Mtu anastaafu katika nafasi kubw nchini lakini uoni mradi wake binafsi anaosimamia, anachoweza nikusubiri Mhe. Rais amteue mwenyekiti wa bodi au mkuu wa taasisi flani Basi. Tungekuwa na wafanyabiashara Leo hii wasingekaa nyumbani baada ya kustaafu wasubiri kuonewa huruma.
Tubadili mfumo tuchanganye wenye mawazo tegemezi (Watumishi) na wasio na mawazo tegemezi wenye uwezo wa kujisimamia (wafanyabiashara)