Ni lini Marekani itaacha mchezo wa kigeugeu?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111420725265.jpg

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani Patrick Ryder hivi majuzi alisema imethibitishwa kuwa puto lililogunduliwa miezi minne iliyopita "halikukusanya taarifa za kijasusi wakati wa safari yake kwenye anga za Marekani." Mara tu taarifa hii kutolewa, vyombo vya habari vya Marekani vilijitokeza kusuluhisha mambo: kauli hii ilipunguza "wasiwasi" wa pande zote nchini Marekani kuhusu “tukio la puto”.

Mwezi Februari mwaka huu, wakati puto la kiraia la China lilipoingia kwenye anga ya Marekani kwa makosa yasiyoweza kuepukika, Wizara ya Ulinzi ya Marekani ilisema wazi kuwa lilikuwa "puto la kukusanya taarifa za kijasusi" na kupaza sauti ya "tishio la China"; Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken naye aliahirisha ziara yake nchini China, na jeshi la anga lilitumia ndege ya kivita aina ya F22 kuliangusha puto hilo kwa kombora lililogharimu mamia ya maelfu ya dola.

Ni Marekani iliyotuma ndege ya kivita kuangusha puto, na pia ni Marekani ilisema puto hilo halikukusanya taarifa za kijasusi, basi puto hilo la China ni la kijasusi au la "utafiti wa kisayansi na matumizi ya kiraia", msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani yeye anakurupuka na kutoa jibu tofauti kabisa.

Kwa bahati mbaya, Marekani hivi karibuni ilijisuta yenyewe tena. Ripoti iliyoainishwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Kitaifa wa Marekani ODNI, ilisema kwamba "haikupata ushahidi wowote kwamba virusi vya COVID-19 vilitoka kwenye Taasisi ya Utafiti wa Virusi ya Wuhan nchini China."

Tangu kuzuka kwa janga la COVID-19 mwaka 2019, wanasiasa na vyombo vya habari vya Marekani vimekuwa vikieneza hoja kwamba "virusi hivyo vilitoka kwenye maabara huko Wuhan, China". Baada ya wataalam kutoka Shirika la Afya Duniani WHO kutoa hitimisho wazi kwamba "haiwezekani kabisa kwa virusi vya COVID-19 kutoka kwenye maabara" baada ya kufanya matembezi halisi na utafiti mwaka 2021, serikali ya Marekani bado ilitumia kauli kama "labda" na "inawezakana". kubainisha chanzo cha virusi ili kuchafua sura ya China. Lakini kama ilivyokiri ripoti hiyo kutoka ODNI, "Shirika la Upelelezi la Marekani CIA na wakala mwingine bado hawawezi kubaini chanzo halisi cha virusi hivyo kwa sababu mahitimisho yote yanategemea uwezekano au ripoti zinazokinzana."

Iwe ni kuelezea puto la kiraia la China kama "la kijasusi" au kusema virusi vya COVID-19 "vimevujishwa na binadamu", hizi zote ni njama za Marekani za kukandamiza na kuchafua sura za China, na kufanya China kuwa "adui wa wengi" ili kuzuia maendeleo ya China. Vilevile kufanya hivyo kunalenga masuala ya kisiasa ya ndani ya Marekani, hasa kwa kuwa uchaguzi mkuu unakaribia nchi humo, na chama chochote kitakachokuwa na msimamo mkali zaidi dhidi ya China kitapata kura nyingi.

Sasa, serikali ya Marekani inajitokeza na kuonesha mchezo wake wa kigeugeu, sababu sio vigumu kuelewa. Siku hizi, maafisa wa ngazi ya juu wa Marekani wameitembelea China mmoja baada ya mwingine. Ikulu ya White House inatarajia " kudhibiti ipasavyo tofauti kati yake na China ili isije ikawa makabiliano na migogoro halisi. Lakini hii sio nia ya dhati, kwani Marekani haijaacha kuitendea China vibaya. Kwa mfano, Antony Blinken, aliyemaliza ziara yake nchini China, alisema kuwa "Marekani itaendelea kufanya na kusema mambo ambayo China haiyapendi." Je, ni "vitu gani ambavyo China haipendi"? Kulingana na shirika la habari la Bloomberg, serikali ya Marekani inatarajiwa kupitisha amri ya kiutendaji inayolenga kuzuia uwekezaji kabisa nchini China kwenye akili bandia na sekta nyingine za kiteknolojia.

Waswahili husema “unapomnyooshea mwenzako kidole kimoja elewa kwamba vidole vilivyobaki vimekuelekea mwenyewe”. Hadi leo hii, Marekani bado inaamini kimakosa kuwa inaweza kufanya mazungumzo na China huku ikiikandamiza China. Lakini kwa kweli, kitendo hicho sio tu hakisaidii uhusiano kati ya nchi hizo mbili, lakini pia kinadhoofisha sana sifa ya Marekani kimataifa. Makala ya tahariri iliyopewa kichwa cha "Marekani inakosa heshima" iliyochapishwa hivi karibuni na jarida la "Modern Diplomacy" la Ulaya ilisema kwamba kwa muda mrefu Marekani imetumia vigezo viwili kwenye masuala makubwa ya kimataifa, na hii imepunguza sana uaminifu wa Marekani. Kwa mujibu wa matokeo ya hivi punde ya kura za maoni ya watu wa nchi za kiarabu yaliyotolewa na Chuo Kikuu cha Prince nchini Marekani, uaminifu wa Marekani unapungua sana, lakini watu wengi wanaamini kuwa China ndiyo “nchi yenye nguvu” inayopendwa zaidi.
 
Sera ya marekani hana rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu ila ana maslai ya kudumu , ata mtu binafsi ukiwa hivi lazima utoboe .
 
View attachment 2678124

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani Patrick Ryder hivi majuzi alisema imethibitishwa kuwa puto lililogunduliwa miezi minne iliyopita "halikukusanya taarifa za kijasusi wakati wa safari yake kwenye anga za Marekani." Mara tu taarifa hii kutolewa, vyombo vya habari vya Marekani vilijitokeza kusuluhisha mambo: kauli hii ilipunguza "wasiwasi" wa pande zote nchini Marekani kuhusu “tukio la puto”.



Mwezi Februari mwaka huu, wakati puto la kiraia la China lilipoingia kwenye anga ya Marekani kwa makosa yasiyoweza kuepukika, Wizara ya Ulinzi ya Marekani ilisema wazi kuwa lilikuwa "puto la kukusanya taarifa za kijasusi" na kupaza sauti ya "tishio la China"; Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken naye aliahirisha ziara yake nchini China, na jeshi la anga lilitumia ndege ya kivita aina ya F22 kuliangusha puto hilo kwa kombora lililogharimu mamia ya maelfu ya dola.



Ni Marekani iliyotuma ndege ya kivita kuangusha puto, na pia ni Marekani ilisema puto hilo halikukusanya taarifa za kijasusi, basi puto hilo la China ni la kijasusi au la "utafiti wa kisayansi na matumizi ya kiraia", msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani yeye anakurupuka na kutoa jibu tofauti kabisa.



Kwa bahati mbaya, Marekani hivi karibuni ilijisuta yenyewe tena. Ripoti iliyoainishwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Kitaifa wa Marekani ODNI, ilisema kwamba "haikupata ushahidi wowote kwamba virusi vya COVID-19 vilitoka kwenye Taasisi ya Utafiti wa Virusi ya Wuhan nchini China."



Tangu kuzuka kwa janga la COVID-19 mwaka 2019, wanasiasa na vyombo vya habari vya Marekani vimekuwa vikieneza hoja kwamba "virusi hivyo vilitoka kwenye maabara huko Wuhan, China". Baada ya wataalam kutoka Shirika la Afya Duniani WHO kutoa hitimisho wazi kwamba "haiwezekani kabisa kwa virusi vya COVID-19 kutoka kwenye maabara" baada ya kufanya matembezi halisi na utafiti mwaka 2021, serikali ya Marekani bado ilitumia kauli kama "labda" na "inawezakana". kubainisha chanzo cha virusi ili kuchafua sura ya China. Lakini kama ilivyokiri ripoti hiyo kutoka ODNI, "Shirika la Upelelezi la Marekani CIA na wakala mwingine bado hawawezi kubaini chanzo halisi cha virusi hivyo kwa sababu mahitimisho yote yanategemea uwezekano au ripoti zinazokinzana."



Iwe ni kuelezea puto la kiraia la China kama "la kijasusi" au kusema virusi vya COVID-19 "vimevujishwa na binadamu", hizi zote ni njama za Marekani za kukandamiza na kuchafua sura za China, na kufanya China kuwa "adui wa wengi" ili kuzuia maendeleo ya China. Vilevile kufanya hivyo kunalenga masuala ya kisiasa ya ndani ya Marekani, hasa kwa kuwa uchaguzi mkuu unakaribia nchi humo, na chama chochote kitakachokuwa na msimamo mkali zaidi dhidi ya China kitapata kura nyingi.



Sasa, serikali ya Marekani inajitokeza na kuonesha mchezo wake wa kigeugeu, sababu sio vigumu kuelewa. Siku hizi, maafisa wa ngazi ya juu wa Marekani wameitembelea China mmoja baada ya mwingine. Ikulu ya White House inatarajia " kudhibiti ipasavyo tofauti kati yake na China ili isije ikawa makabiliano na migogoro halisi. Lakini hii sio nia ya dhati, kwani Marekani haijaacha kuitendea China vibaya. Kwa mfano, Antony Blinken, aliyemaliza ziara yake nchini China, alisema kuwa "Marekani itaendelea kufanya na kusema mambo ambayo China haiyapendi." Je, ni "vitu gani ambavyo China haipendi"? Kulingana na shirika la habari la Bloomberg, serikali ya Marekani inatarajiwa kupitisha amri ya kiutendaji inayolenga kuzuia uwekezaji kabisa nchini China kwenye akili bandia na sekta nyingine za kiteknolojia.



Waswahili husema “unapomnyooshea mwenzako kidole kimoja elewa kwamba vidole vilivyobaki vimekuelekea mwenyewe”. Hadi leo hii, Marekani bado inaamini kimakosa kuwa inaweza kufanya mazungumzo na China huku ikiikandamiza China. Lakini kwa kweli, kitendo hicho sio tu hakisaidii uhusiano kati ya nchi hizo mbili, lakini pia kinadhoofisha sana sifa ya Marekani kimataifa. Makala ya tahariri iliyopewa kichwa cha "Marekani inakosa heshima" iliyochapishwa hivi karibuni na jarida la "Modern Diplomacy" la Ulaya ilisema kwamba kwa muda mrefu Marekani imetumia vigezo viwili kwenye masuala makubwa ya kimataifa, na hii imepunguza sana uaminifu wa Marekani. Kwa mujibu wa matokeo ya hivi punde ya kura za maoni ya watu wa nchi za kiarabu yaliyotolewa na Chuo Kikuu cha Prince nchini Marekani, uaminifu wa Marekani unapungua sana, lakini watu wengi wanaamini kuwa China ndiyo “nchi yenye nguvu” inayopendwa zaidi.
Wakala wa shetani,waharibu kwenye dunia
 
Back
Top Bottom