Mpango wa uwongo wa Marekani wenye thamani ya dola milioni 300 wafichuliwa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111437104227.jpg


Kwa miaka mitano mfululizo, kila mwaka dola za Marekani milioni 300 zimekuwa zikitengwa, hivi karibuni msomi wa Ulaya Bw. Jan Oberg alifichua katika mahojiano kuwa Marekani imetoa mswada wa kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari ili watoe ripoti mbaya kuhusu China. Inadaiwa kwamba kile alichokitaja Bw. Oberg ndio "Sheria ya Ushindani wa Kimkakati ya mwaka 2021" iliyopitishwa na Kamati ya Masuala ya Kigeni ya Baraza la Seneti la Bunge la Marekani mwezi Aprili mwaka 2021. Sheria hiyo imelenga kukabiliana na ushawishi wa China duniani.

Hali halisi ni kwamba, kumekuwa na taarifa zinazoonesha Marekani inaanzisha vita vya maoni ya umma dhidi ya China kwa muda mrefu. Mapema mwishoni mwa mwaka 2021, vyombo vya habari vya Zimbabwe viliripoti kuwa serikali ya Marekani kupitia ubalozi wake nchini humo imewahonga wanahabari wa vyombo binafsi, dola za kimarekani elfu moja ili kuandika makala moja ya kuchafua sura ya kampuni za China nchini Zimbabwe. Inaonekana kuwa hii ilikuwa ni hatua ya mapema iliyochukuliwa na serikali ya Marekani kwa mpango wake huu mbaya wa miaka mitano dhidi ya China.

Katika miaka ya hivi karibuni, kadri ushirikiano kati ya China na Afrika unavyozidi kuwa mzuri, Marekani inaona kuwa ushawishi wake barani Afrika unapungua sana. Katika hali hii, serikali ya Marekani inatumia pesa kidogo kuwafadhili watu waliotoa ripoti kuchafua sura ya China kwa kisingizio cha “kuunga mkono uhuru wa vyombo vya habari”, jambo ambalo linatajwa kama ni mbinu yenye hasara ndogo na faida kubwa. Lakini jaribio hili haliwezi kuharibu msingi wa ushirikiano kati ya China na Afrika, wala kubadilisha hali ya sasa ya China kuwa na ushawishi mkubwa barani Afrika kuliko ule wa Marekani.

Kwa mujibu wa Wizara ya Biashara ya China, China imedumisha nafasi ya mwenzi mkubwa wa kibiashara wa Afrika kwa miaka 14 iliyopita, haswa katika miaka ya hivi karibuni, uagizaji bidhaa za Afrika umeongezeka sana, ambapo mauzo ya mazao ya kilimo ya Afrika nchini China yanaongezeka kwa wastani wa asilimia 11.4 kwa mwaka; chini ya utaratibu wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC na ujenzi wa pamoja wa “Ukanda Mmoja, Njia Moja” BRI, China imekuwa mwekezaji mkubwa zaidi wa miundombinu barani Afrika, na jengo la makao makuu ya Afrika CDC na Reli ya SGR ya Kenya imekuwa miradi mikubwa zaidi inayosikika mara kwa mara; na wakati huohuo, China imekuwa nchi inayopokea kwa wingi wanafunzi wa kigeni kutoka Afrika, ambapo idadi ya wanafunzi wa Afrika wanaokuja China ni mara mbili ya watu wanaoenda kusoma Marekani……

Tafiti nyingi pia zimekanusha kauli kama eti China inatoa “mikopo yenye hila”, kufanya “ukoloni mambo leo” au kupeleka wafanyakazi wa China barani Afrika. Shirika la Fedha la Kimataifa IMF mwishoni mwa mwaka jana lilitoa ripoti ya mtazamo wa uchumi wa Afrika ikikiri kuwa China sio chanzo kikuu cha mzigo wa madeni katika Afrika Kusini mwa Sahara, na kwamba asilimia 80 ya madeni yanayozikabili nchi za Afrika yanatokana na taasisi za fedha za kimataifa na wakopeshaji wa kibiashara wa nchi za Magharibi, ambapo Marekani ina nafasi kubwa. Uchunguzi huru nao pia umegundua kuwa asilimia 89 ya wafanyakazi wa kawaida na asilimia 44 ya wasimamizi katika kampuni za China barani Afrika ni wenyeji, na uwekezaji wa serikali ya China barani Afrika unaangalia maendeleo, na sekta zinazowekezwa ni pamoja na afya, elimu, mafunzo, na kilimo.

Ni hatari kwa Marekani kuleta mtazamo wa “vita vipya vya baridi” barani Afrika, China haishiriki kwenye mashindano ya kimataifa ya kujitangazia umwamba barani Afrika, sembuse kuitawala Afrika. Maendeleo ya kasi ya uhusiano kati ya China na Afrika yanatokana na sera ya China yenye moyo wa dhati. Kama alivyosema Peter Kagwanja, mkurugenzi wa Taasisi ya Sera ya Afrika ya Kenya, katika miaka 20 iliyopita, China imeibuka kama mwezi mkubwa zaidi wa Afrika, cha muhimu ni kwamba wakati nchi za Magharibi ziliichukulia Afrika kama "bara lisilo na matumaini," China tangu mwanzo imeiangalia Afrika kama ni fursa badala ya changamoto. Kwa hivyo, hadi sasa jaribio lolote la kuvunja ushirikiano wa kirafiki kati ya China na Afrika, kupitia kutoa habari zenye uwongo halijafanikiwa, na pia halitafanikiwa katika siku za baadaye.
 
Ushawishi wa China ni pamoja na kuitaifisha airport ya Lusaka, na Wachina kuingia mpaka kwenye Jeshi la Polisi Zambia.

Huu ni ukichaa, sihitaji hata dollar moja ya hao Wamarekani kuusema ukweli ubaya wa Wachina.

Ukiona makamari ya madubu mtaani basi ujuwe ni Mchina huyo, ukiona tembo wanatekea basi ujuwe ni Mchina huyo.

Mifuko yote ya Wildlife conservation inachangiwa na wazungu hasa Wamarekani kutunza wildlife yetu.
 
Back
Top Bottom