Ni kweli waliouawa Mwanza walitoka Kibiti?

Ni kweli waliouawa Mwanza walitoka Kibiti?

Unabisha nn juu ya hili na unavosema kwamba mtu yeyote akihamia sehem pasipo kujitambulisha kwa serikal ya kijiji anauwawa hv kweli watu wamekutwa na silaha wameuliwa as long as ni majambazi haijarishi wapi wametokea bado unapinga tu daah alieturoga kafa
Achana naye bwege huyo hajielewi na haelewi anachokiandika ..
 
Intelijensia Ipi unayoizungumzia wewe????
Ni hii hii ambayo imeshindwa kudhibiti mauaji ya kibiti kwa kipindi chote hiki???

Ni intelijensia ipi unayotakabkuiaminisha kwayo????
Ni hii hii ambayo mpaka Leo haijui kwanini mauaji yatokee KIBITI????

Div 1 na div 5 za bongo hazi reflect uwezo wa mtu wa ubongo
Mtalalamika sana na bado mpaka mtandao wenu utaisha wote mtakamatwa popote mlipo..
Na lazma mfe wote roho mnazoziua zisizo na hatia znawalilia nyuma ndio maana kila mnapokimbilia mnadakwa..

Itaeleweka tu
 
Kaulize kenya wamefikia wapi na wawekezaji wa kisomali. Tusifanye mchezo na mambo ya msingi. Unahakika hawa wendawazimu wako kibiti muda wote? Nchi inaingia kwenye janga la upotevu wa amani wewe unaleta itani wa kisiasa?Kumbuka kesho wataua bila kuchagua na hili ni janga la nchi yote! Swali lako ni la kitoto na halina hata chembe ya utanzania!Polisi wanajua wafanyalo ili kesho tuwe salama!
Achana na kahaba huyo akili yake imechoka
 
Kna wtu sidhani km niwazma maana kuingili kz ya Polic bac nenda ww ukatoe ushahdi km hawa siwo halafu na ww modoreta acha kushikwa akili co kla ktu unaruhu kpoctiwe hm
 
Mkuu
Usipanic
Twende taratibu...
Hakuna anayetamani haya yanayotokea yaendee...
Yanatuumiza sisi sote,lakini hii miereka ya Serikali yako hii inaturudisha nyuma sana kifikra.
Kama mlihamishia Jeshi la Polisi huko na bado watu wakaendelea kuuwawa iweje uone tuko salama.
Sina hakika sana kama ni Kweli SERIKALI imeshindwa kudhibiti mauaji hayo la sivyo basi iko siri kubwa sana serikali inaijua kuhusu mauaji haya
Wewe mheshimiwa,
ulitaka hayo mauaji yakome lini ?
Kwani iliwekwa deadline ya mwisho kwa wauaji kukamatwa wote
huko Kibiti ?
Au hujui kua vita ya wahalifu, magaidi na majambazi ni endelevu ?
Huko Ulaya unakoamini kumejiimarisha kiulinzi bado wahalifu
wanasumbua.
Wewe ulitakiwa uwahakiki hao waliouliwa, upate ushahidi kuwa sio wahalifu bali walionewa, ndio uje ulalamike hapa na upeleke ushahidi kwenye vyombo husika ili wachukue sheria.
Au nenda ulisaidie jeshi la polisi kuwakamata wauaji halisi kwa muda unaodhani unastahili.
Jitahidi kuandika habari ulizozifanyia utafiti na sio kuleta mihemko ya mitaani.

Vita ya uhalifu ni endelevu.
 
MUNGU NIPE HEKIMA NIONGEE KIDOGO KUHUSU WAUWAJI WA KIBITI.

Zipo taarifa kwamba kwamba wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza baada ya majibizano ya risasi na askari wetu.

Pia ziko taarifa kwamba akipatikana mtu mgeni kwenye eneo fulani kwa maana ya kwamba serikali ya eneo Hilo kutokumtambua basi atauwawa.

Kama taarifa hizi ndivyo zilivyo basi tunazo sababu za kujiuliza maswali mengi.

Kwamba, kama wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza kwenye majibizano ya risasi na askari, ni nani alitoa taarifa za uwepo wa watu hao Mwanza wakitokea KIBITI?

Je, aliyetoa taarifa ya watu hao kuwa wametoka KIBITI alizithibitihaje taarifa hizo na yuko wapi mpaka sasa?

Jeshi la Polisi linasema nini juu ya mtoa taarifa huyo ambaye kimsingi atalisaidia sana Jeshi letu la Polisi kufanya upelelezi?

Je, ni sahihi kwamba mtu yeyote mgeni kwenye eneo fulani anatakiwa kuuwawa? Na kama ndivyo mbona serikali yetu imekuwa na uoga wa kiwango hiki kwa wahalifu?

Je, hakuna namna nyingine ya kushughulika na wanaodaiwa kuwa ni wageni kwenye maeneo fulani zaidi ya kuwauwa?

Hii ni Tanzania ile ile tunayoisifia kwamba inaongozwa kwa misingi ya sheria?

KIBITI KIBITI KIBITI
MCHEZO WA SINEMA USIOTABIRIKA.
Haya ni mawazo tu lakini ya mjinga mmoja.
Angalia miwani ya RPC ndio utajua ukweli
 
kama majambazi waliouawa ni ndugu zako unakaribishwa katika postmortem halafu ukawazike kwa heshima.

Polisi ikishatangaza vita maana yake hakuna majadiliano ni action tu.

Hapa mtaani kwangu kuna wageni kibao sijaona wakiuawa na Polisi.

Wanaouawa ni Majambazi...na waendelee kuawa tu.
Kuwa mkweli usifuate mkumbo. Fikiria kidogo tu
 
Sidhani Kama kuna agizo la kuua mgeni kwenye eneo Fulani huo ni upotoshaji na pili taifa lina intelijensia hivo kuwa trace Hao watu kuwa wametoka kibiti ni kazi ya intelijensia
Hii intelijensia kwann isipelekwe na Kibiti??
 
Si malengo yangu...
Lakini hili suala la KIBITI lina ukakasi sana
Rose, usalama wa RAIA hauko hivo unavosema. Ww ulishawahi kuwa mbunge tungetegemea uwe na uelewa mpana wa mambo lakin sio hivo.

Ukiangalia hali ilivokuwa kipindi cha kikwete utagundua kuwa waovu wengi walijijenga kipindi hicho. Na hapo namaanisha waovu wa kila aina. Wezi, mafisad wajambazi magaid nakadhalika nakadhalika.

Vita ya kupambana nao sio lelemama kama akili yako inavokutuma. Kule kibiti ni kama kulikuwa na kikosi kabisa cha majambazi au magaid. Ukikisambaratisha kile nacho kinasambaa kila kona ya nchi. Na ndo maana wengine wamekamatwa kule songea, wengine nachingwea, wengine mwanza, of course wengine watakuwa apo apo kibiti na hata dar na mikoa mingine.

Ni suala la kutumia tu akili ili uelewe kuwa hawa magaid sio wajinga kama nyie wapinzan mnavotaka ieleweke. Sasa kwa taarifa yenu hawa wote watakamatwa na kupotezwa wote. Jeshi letu sio la mzaha mzaha.
 
Aliyetoa taarifa za wahalifu waliohusika na mauaji MKIRU apewe milioni kumi zake...!
 
Hebu tuache unazi kidogo tujadili jambo hili maana kesho ni jingalao au Chakaza anaweza kushambuliwa na hao magaidi/majambazi.
Nachoshindwa kuelewa ni kuwa Polisi walizingira hiyo Nyumba na mapambano yakaanza. Wakaua sita na "wanasema" wawili wamekimbia. Wamekimbiaje toka Nyumba iliyozingirwa? Wamejuaje kuwa ni wawili tuu waliokimbia wakati wenzao hawakuweza kusema kwani wamewaua?
Ndio hapo woga unapotuzidia
Mkuu Chakaza,wanaposema "wawili wamefanikiwa kukimbia" wana maana ya "kuweka open window" kwa doubts kama zenu ikitokea kesho mauaji yameendelea. Itakuwa "labda ni wale wawili waliokimbia MZA au ni wale wawili waliokimbia Kibigi".
 
Sasa hiv kama unawajua majangil au vibaka weny bunduki ukienda kuripoti unajishindia 10 million sio mchezo kwa usawa huu, hata mm nipo chimbo natafuta walio salia nitoe taarifa nikamate mpunga wa Sirro kiulain
 
Serikali ya Tanzania imewavalisha jwtz nguo za police, Halafu wamewekwa maeneo kibiti na sasa wanauwa kila mgeni na muislamu mwenye ndevu. Lakini hawaondoi ugaidi wana recruit wapya, mtu alieuliwa baba yake, kaka yake rafiki yake ni rahisi kubandika kuwa gaidi, historia inatusomesha.
 
Mimi nilivyo msikiliza yule kamanda wa mwanza kuna sehemu alisema kuna mtu walimkamata siku 6 kabla hao jamaa kubainika so yawezekana ndo aliye saidia mambo yote hayo,

Kuhusu mharifu kukamatwa sehemu/mkoa mwingine hiyo sio hoja mkuu labda kama una hoja nyingine, unakumbuka nadhani ni 2013 mwishoni au mwanzoni mwa 2014 kuna jamaa alikuwa anaua watu wasio na hatia kule Tarime alikamatiwa Tanga so unaweza ukaona ni kwa kiasi vyombo vya ulinzi na usalama vina mkono mrefu.
 
Back
Top Bottom