Ni kweli waliouawa Mwanza walitoka Kibiti?

Ni kweli waliouawa Mwanza walitoka Kibiti?

Kama unatishika endelea kuwapa ushirikiano taarifa muhimu kama unazo ili waweze kuuawa!
Hebu tuache unazi kidogo tujadili jambo hili maana kesho ni jingalao au Chakaza anaweza kushambuliwa na hao magaidi/majambazi.
Nachoshindwa kuelewa ni kuwa Polisi walizingira hiyo Nyumba na mapambano yakaanza. Wakaua sita na "wanasema" wawili wamekimbia. Wamekimbiaje toka Nyumba iliyozingirwa? Wamejuaje kuwa ni wawili tuu waliokimbia wakati wenzao hawakuweza kusema kwani wamewaua?
Ndio hapo woga unapotuzidia
 
Next tym watakuambia tumeua majitu matatu yanayosadikiwa kuwa ni majamb mkoani mbeya. Hawa walinz wetu wapo vizur kwa intelejensia
 
Yaani sasa tunataka Polisi kabla hawajafanya kazi yao watueleze kuwa wanakusudia kupambana?
Au Intelijensia yao au ya TISS ikishagundua wauaji wako wapi pia wajekutueleza na sisi wananchi?
Au kwamba kama TISS ndo ilitoa taarifa kwa polisi kuwa wauaji wapo Mwanza basi na sisi wananchi tuelezwe?

Naamini una nia njema lakini hii hoja yako haijakaa sawa.
 
Hebu tuache unazi kidogo tujadili jambo hili maana kesho ni jingalao au Chakaza anaweza kushambuliwa na hao magaidi/majambazi.
Nachoshindwa kuelewa ni kuwa Polisi walizingira hiyo Nyumba na mapambano yakaanza. Wakaua sita na "wanasema" wawili wamekimbia. Wamekimbiaje toka Nyumba iliyozingirwa? Wamejuaje kuwa ni wawili tuu waliokimbia wakati wenzao hawakuweza kusema kwani wamewaua?
Ndio hapo woga unapotuzidia
Hakuna cha unazi wala nini...!
kinachokushangaza ni nini?yaani kukimbia kwa majambazi wawili sio jambo la kawaida?
Unaongea as if hayo ni mapambano ya kwanza baina ya polisi na majambazi.

Kwa mantiki yako unataka kusema polisi wametudanganya?
 
Kuna jambo haliko sawa mahali na ni vema statements zao ziwe zinaandaliwa kwa umakini.
Kama wale wa Kibiti wapo mpaka Mwanza, wengine wanashikwa Tunduru jee Dar jiji kubwa na lililo karibu na Kibiti watakuwepo wangapi?
WANATUTISHA SANA NA HIZI TAARIFA
Tunahitaji serikali iwe na ukweli sana katika hili...si vema tukileta maigizo kwenye masuala ya msingi
 
hv umemwelewa alichokuliza [HASHTAG]#rose[/HASHTAG] mayemba?mbn unajibu kisiasa sana ww! huenda hufatilii haya!
Sababu anauliza ujinga ujinga mtupu tena kwa kejeli kabisa, mbona kina Upendo Peneza wanajiheshimu na kufanya siasa za kistaarabu. Hivi unategemea Polisi watasema hadharani walithibitisha vipi taarifa zao ? Yeye inamuuma sana kwa hao majambazi kuuliwa ila polisi na raia wema wakiuliwa ni furaha kwake ?

Sasa naelewa kwa nini Mbowe alimtosa viti maalum, kichwani hamna kitu zaidi ya kujua kuropoka tu. Mtu yoyote timamu hawezi kuja kutetea wauaji hapa.
 
kama majambazi waliouawa ni ndugu zako unakaribishwa katika postmortem halafu ukawazike kwa heshima.

Polisi ikishatangaza vita maana yake hakuna majadiliano ni action tu.

Hapa mtaani kwangu kuna wageni kibao sijaona wakiuawa na Polisi.

Wanaouawa ni Majambazi...na waendelee kuawa tu.
Hujaelewa hoja yangu...nisome vizuri kwanza
 
Mjumbe Rose ni wazi kuwa hujui usemalo. Mwulize mtu yeyote hata mtoto atakwambia kuwa mambo kama hayo hayaulizwi wala kujibiwa hazarani labda kama unanusanusa upate fununu uwasaidie wahusika. Endelea kuamini unachoamini, kuwaliwaza magaidi na maadui wa Taifa hili. Uyakapojazinduka utakuta meli ilishaondoka zamani.
Sidhani kama hii ilikuwa ndiyo maana halisi ya andiko langu
 
Sidhani Kama kuna agizo la kuua mgeni kwenye eneo Fulani huo ni upotoshaji na pili taifa lina intelijensia hivo kuwa trace Hao watu kuwa wametoka kibiti ni kazi ya intelijensia
Na ukiwa mgeni mahali sidhani Kama utapigwa risasi tu hapana utasimamishwa utahojiwa na kuulizwa vitambulisho Ndio utaratibu ila wewe ukisimamishwa ukaanza kukimbia na kurusha risasi lazima utauawa
Hii ni nchi ya UDIKITEITA, hayo unayoyasema ya kusimamishwa kuhojiwa ni nchi zenye demokrasia, siyo hii! Unatetea udikiteita kama siyo wewe wajukuu zako wahalia
 
Police wetu wajuvi sana ujue. Huenda waliwahoji wale jamaa kabla hawajakata roho na wakathibitisha bila shaka kuwa ni kweli wao ndo walikuwa wanaiterrorize Kibiti kabla ya kuhamia Mwanza. Heko Kamanda wa Mwanza🙂
Hahaaaaaaaaaaaaa.....lakini inaweza kuwa Kweli....umewaza vema
 
Jeshi la polisi lifanye kazi yake kwa ueledi.Lisianze kututia hofu, hao watu wa kibiti walijipanga muda mrefu kwa hiyo jeshi letu na vyombo vya usalama viende kisomi zaidi.Hizi taarifa mara tumeua wanne, mara tumeua Mwanza hazitusaidii..Tunachohitaji mauaji ya Kibiti yakomeshwe!
Umenena vema mkuu
 
Huyu kamanda msangi ana kimbele mbele sana ,natamani apelekwe kibiti atacheza na media mpaka wauaji waishe kabisa,kila anachofanya media anao mkononi.
Ile ya ya magaidi wa mapango ya amboni tanga. KAMANDA MSANGI yeye alikuja na yake ya mwanza , Mizinga ya kuvunjia mawe na mahandaki kuuwa majambazi mwanza(polisi tangu lini watumie mizinga ). advertisement yake tu mtu unajua leo ama zetu ama zao.
naamini akipelekwa kibiti urafiki wake na vyombo vya habari utawamaliza nguvu magaidi.
Jambo zito hili
 
MUNGU NIPE HEKIMA NIONGEE KIDOGO KUHUSU WAUWAJI WA KIBITI.

Zipo taarifa kwamba kwamba wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza baada ya majibizano ya risasi na askari wetu...

Pia ziko taarifa kwamba akipatikana mtu mgeni kwenye eneo fulani kwa maana ya kwamba serikali ya eneo Hilo kutokumtambua basi atauwawa...

Kama taarifa hizi ndivyo zilivyo basi tunazo sababu za kujiuliza maswali mengi.

Kwamba, kama wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza kwenye majibizano ya risasi na askari, ni nani alitoa taarifa za uwepo wa watu hao Mwanza wakitokea KIBITI????

Je aliyetoa taarifa ya watu hao kuwa wametoka KIBITI alizithibitihaje taarifa hizo na yuko wapi mpaka sasa?

Jeshi la Polisi linasema nini juu ya mtoa taarifa huyo ambaye kimsingi atalisaidia sana Jeshi letu la Polisi kufanya upelelezi?

Je ni sahihi kwamba mtu yeyote mgeni kwenye eneo fulani anatakiwa kuuwawa? Na kama ndivyo mbona serikali yetu imekuwa na uoga wa kiwango hiki kwa wahalifu?

Je hakuna namna nyingine ya kushughulika na wanaodaiwa kuwa ni wageni kwenye maeneo fulani zaidi ya kuwauwa?
Hii ni Tanzania ileile tunayoisifia kwamba inaongozwa kwa misingi ya sheria?

KIBITI KIBITI KIBITI
MCHEZO WA SINEMA USIOTABIRIKA.
Haya ni mawazo tu lakini ya mjinga mmoja....
Afadhali umejisema mwenyewe mjinga,hatusikilizagi wajinga sisi
 
sasa hivi wanasakwa vibaya mno majuzi kuna mtu alikuja kutafutwa maeneo ya Nachingwea ikaonekana alitokea kibiti na alikuwa ameomba kibarua sehemu ya fenicha ambapo alikaa kama wiki 3 huku wenyeji hawakujua ametokea wapi na alikuwa anepanga vyumba viwili katika maeneo tofauti, wakati wenyeji walipokamatwa alikuwa aneshatoroka siku moja kabla na hata alivyotafutwa hakupatikana so ni kweli hao watu wapo na tayari wamenasa mawasiliano yao yote so hata uende wapi utakamatwa tu.
 
MUNGU NIPE HEKIMA NIONGEE KIDOGO KUHUSU WAUWAJI WA KIBITI.

Zipo taarifa kwamba kwamba wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza baada ya majibizano ya risasi na askari wetu...

Pia ziko taarifa kwamba akipatikana mtu mgeni kwenye eneo fulani kwa maana ya kwamba serikali ya eneo Hilo kutokumtambua basi atauwawa...

Kama taarifa hizi ndivyo zilivyo basi tunazo sababu za kujiuliza maswali mengi.

Kwamba, kama wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza kwenye majibizano ya risasi na askari, ni nani alitoa taarifa za uwepo wa watu hao Mwanza wakitokea KIBITI????

Je aliyetoa taarifa ya watu hao kuwa wametoka KIBITI alizithibitihaje taarifa hizo na yuko wapi mpaka sasa?

Jeshi la Polisi linasema nini juu ya mtoa taarifa huyo ambaye kimsingi atalisaidia sana Jeshi letu la Polisi kufanya upelelezi?

Je ni sahihi kwamba mtu yeyote mgeni kwenye eneo fulani anatakiwa kuuwawa? Na kama ndivyo mbona serikali yetu imekuwa na uoga wa kiwango hiki kwa wahalifu?

Je hakuna namna nyingine ya kushughulika na wanaodaiwa kuwa ni wageni kwenye maeneo fulani zaidi ya kuwauwa?
Hii ni Tanzania ileile tunayoisifia kwamba inaongozwa kwa misingi ya sheria?

KIBITI KIBITI KIBITI
MCHEZO WA SINEMA USIOTABIRIKA.
Haya ni mawazo tu lakini ya mjinga mmoja....
Kama kweli wamewaua mwanza, Mbona jana kibiti kuna mtu amekula "chuma"?

RIP innocent citizens
 
Back
Top Bottom