MUNGU NIPE HEKIMA NIONGEE KIDOGO KUHUSU WAUWAJI WA KIBITI.
Zipo taarifa kwamba kwamba wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza baada ya majibizano ya risasi na askari wetu...
Pia ziko taarifa kwamba akipatikana mtu mgeni kwenye eneo fulani kwa maana ya kwamba serikali ya eneo Hilo kutokumtambua basi atauwawa...
Kama taarifa hizi ndivyo zilivyo basi tunazo sababu za kujiuliza maswali mengi.
Kwamba, kama wauwaji wa KIBITI wameuwawa Mwanza kwenye majibizano ya risasi na askari, ni nani alitoa taarifa za uwepo wa watu hao Mwanza wakitokea KIBITI????
Je aliyetoa taarifa ya watu hao kuwa wametoka KIBITI alizithibitihaje taarifa hizo na yuko wapi mpaka sasa?
Jeshi la Polisi linasema nini juu ya mtoa taarifa huyo ambaye kimsingi atalisaidia sana Jeshi letu la Polisi kufanya upelelezi?
Je ni sahihi kwamba mtu yeyote mgeni kwenye eneo fulani anatakiwa kuuwawa? Na kama ndivyo mbona serikali yetu imekuwa na uoga wa kiwango hiki kwa wahalifu?
Je hakuna namna nyingine ya kushughulika na wanaodaiwa kuwa ni wageni kwenye maeneo fulani zaidi ya kuwauwa?
Hii ni Tanzania ileile tunayoisifia kwamba inaongozwa kwa misingi ya sheria?
KIBITI KIBITI KIBITI
MCHEZO WA SINEMA USIOTABIRIKA.
Haya ni mawazo tu lakini ya mjinga mmoja....