Biggest economies in 2021 by gross domestic product
Boss, Tukiongelea interms of GDP, kufikia 2021 ushawishi wake upo juu. Labda ushawishi katika angle nyingine ila nchi nyingi hupendelea kuwa na diplomasia nzuri na nchi zenye GDP kubwa.
Labda mleta mada angetueleza hao wataalamu wa kimataifa wametumia vigezo vipi?
Ndani ya miaka ya hivi karibuni, bado naona US anazidi kwa ushawishi na nguvu zake zikizidi kuongeza. Hii agenda ya US kushuka chini haijaanza leo wala jana, toka miaka ya 70, 80 na 90, na sasa ni 2020. Zamani alikuwa akipambanishwa dhidi ya Japan, mara German na sasa China.
Ni ngumu kumshusha US kutokana na uchumi wake ulipo. Leo hii kuhusu viwanda, teknolojia, huduma n.k ni US ndo ameshika dunia, kuhusu bank ya dunia na taasisi za kifedha zinazojihusisha na mataifa huko tusiguse, hizi taasisi zote zinaendeshwa na yeye.
Kibaya zaidi ni kuwa, China ndiye anayegemewa kumpiku US, china huyu huyu? China ambaye hata kijeshi hana uthubutu dhidi ya US. China ambae uchumi wake unapaa kutokana na US kuwekeza kwake na kumruhusu mchina auze zaidi kwake, hapo tusizungumzie Ulaya ambayo ipo mifukoni mwa US. China ana pesa ambazo ni kutoka kwa hawa washirika wa US na US mwenyewe. US akiamua kupambana na mchina, ni baada ya miaka michache tu utaona China akishuka kwa kasi.
Pia unaposema US hana ushawishi, yaani ushawishi wake unapungua huwa unatazama nini????? Embu tutazame hili la Ukraine pekee.
China hajaisaidia Ukraine? China amepeleka nini kwa Russia kumpush ktk hii special op yake? Unajifunza nini kwa China kutomzingua US juu ya Taiwan, hakuna picha yoyote unayopata juu ya China kwa US?
Mataifa mangapi yamepiga kura ya kupinga op ya Russia pale Ukraine? Wale walosema hawafungamani na upande wowote maana yake pia wanapinga hii op.
Nachojaribu kusema ni kwamba, nguvu ya US sio ndogo. US sio chombo kidogo, ni heavy. Mleta mada atazame budget za US pengine atapanua ufahamu zaidi.