Mheshimiwa Anna Makinda au hafahamu sheria au anatumia vibaya kiti cha Uspika. Kusema kwamba Tanzania Bara hakuna serikari ni uongo kwani katiba iko wazi, mawaziri wanaendelea na kazi zao mpaka mawaziri wapya watakapo apishwa, na ni wao watakao kabidhi kwa hao wapya! Hata walioanguka kama Mh. Masha na Mh. Mama Mwangunga bado wanapeta kwenye maofisi yao. Kuhusu CHADEMA kutotambua ushindi wa Mh Kikwete, lazima tukumbuke kwamba kuna uraisi kama taasisi, na Kikwete kama mtu. Naamini kwamba taasisi ya uraisi haina utata kwa mtu yeyote. Mheshimiwa Makinda ukumbushwe kwamba mihimili ya nchi ni mitatu, yaani, the Executive, the Legislature na Judiciary. Hii mihimili inatakiwa isiwe tegemezi; the executive inatekeleza kwa kufuata sheria, legislature inatunga sheria, judiciary inatoa tafsiri za sheria kuona kwamba haki inatendeka. Tukumbuke kwamba CUF hawakuzitambua shindi za viongozi wawili waliopita mpaka majuzi tu, lakini waliendelea kuingia bungeni na kushiriki kikamilifu, na aidha kutumia mahakama palipobidi.