Ni kweli Anna Makinda ni 'Mbabe'?

Ni kweli Anna Makinda ni 'Mbabe'?

Dingswayo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
4,019
Reaction score
2,930
5170501743_1fe7e9bf8f_z.jpg


Sikutegemea huyu mama kusema maneno haya kwa wakati huu, hasa akiwa amechaguliwa kama speaker wa bunge. Hili linanipa shaka katika ufanisi wake wa kazi, kwani ameanza vibaya kwa kutumia siasa za maji taka.

Wote tunajua kuwa suala la kuongelea kuhusu 'wizi wa mke wa mtu' ni nini na linamlenga nani. Hizi ni siasa za maki taka. Ni maji taka hayohayo ambayo yalitumiwa na viongozi wa ccm dhidi ya Dr. Slaa wakati wa kampeni za uchaguzi. Kwa hili tunaweza kusema kweli kama atafanya kazi yake vizuri? La hasha! Leo hii hakuna haja ya kutafuta maana ya neno 'fisadi'. Kila mtu anajua hata mtoto wa darasa la 3 anajua.

Kwa kutamka hivyo hadharani, ameuhakikishia umma wa Kitanzania kuwa amewekwa pale kuetetea hoja za mafisadi, hakuna mjadala zaidi. Kama yeye alikuwa halijui hilo, basi imeliwa kwake! Sikuwa na imani na utendaji wa ccm tangu mwanzo, lakini hii imeniongezea kutokuwa na imani na Anna Makinda kama Speaker anayefaa.
 
Anafikiri watu hawana records cha alichoongea mwaka 2008 kuhusu ufisadi!
 
Sikutegemea huyu mama kusema maneno haya kwa wakati huu, hasa akiwa amechaguliwa kama speaker wa bunge. Hili linanipa shaka katika ufanisi wake wa kazi, kwani ameanza vibaya kwa kutumia siasa za maji taka.

Wote tunajua kuwa suala la kuongelea kuhusu 'wizi wa mke wa mtu' ni nini na linamlenga nani. Hizi ni siasa za maki taka. Ni maji taka hayohayo ambayo yalitumiwa na viongozi wa ccm dhidi ya Dr. Slaa wakati wa kampeni za uchaguzi. Kwa hili tunaweza kusema kweli kama atafanya kazi yake vizuri? La hasha! Leo hii hakuna haja ya kutafuta maana ya neno 'fisadi'. Kila mtu anajua hata mtoto wa darasa la 3 anajua.

Kwa kutamka hivyo hadharani, ameuhakikishia umma wa Kitanzania kuwa amewekwa pale kuetetea hoja za mafisadi, hakuna mjadala zaidi. Kama yeye alikuwa halijui hilo, basi imeliwa kwake! Sikuwa na imani na utendaji wa ccm tangu mwanzo, lakini hii imeniongezea kutokuwa na imani na Anna Makinda kama Speaker anayefaa.
.

Uelewa wake wa maana ya neno hilo ni mdogo sana na ni mtu wa vijembe na kukomoa lakini safari hii atabanwa ndani ya bunge na nje ya Wabunge na wapiganaji. Bunge lazima libanwa na waajiri wake ambao ni sisi wananchi. Hivyo kama anategemea mteremko sisi tulioko nje tutambana kukosoa kila baya atakalofanya.
 
..Mama Makinda alituhumiwa na Dr.Ndebelwa Ngunangwa ktk bunge la 1995 kuwa alivamia jimbo la Njombe na kumwaga fedha na zawadi ili achaguliwe kuwa mbunge.

..Dr.Ngunangwa alilamika kwamba ilifika wakati wananchi wa Njombe wakawa wanauliza "alikwina," kwa maana Makinda alikuwa wapi siku zote asiwamwagie misaada na mapesa kiasi hicho.

..kwa mtizamo wangu nadhani ameanza vibaya kwa kupotosha maana ya neno fisadi ktk siasa za Tanzania, na kumtupia vijembe Spika Mstaafu Samuel Sitta.
 
Anafikiri watu hawana records cha alichoongea mwaka 2008 kuhusu ufisadi!

Sijaipata, huyu mama kasemaje tena? I hate her, inabidi 2015 tukaweke kambi jimboni kwake mpaka ang'oke
 
Walishaambiwa kuwa kuchagua ccm ni kujitakia maafa, ndiyo hayo sasa. Hata baraza la mawaziri halijatangazwa tunaanza kuyaona. Poleni sana watanzania. Mwalimu Aliyaona zamani. Kwa mwendo huu tumekwishaaaa! Rais wa mafisadi, speaker wa mafisadi na soon tutaliona baraza la mawaziri wa mafisadi. Mungu Ibariki Tanzania ya Watu wako, tuondolee hawa mafisadi!!!
 
Ameanza vibaya..
Hiyo nafasi haiwezi kwa nyakati hizi..
Anyway, only time will tell
 
Wajameni, nilikuwepo kwenye hiyo press conference yake, aliposema mafisadi ni wezi wa wake za watu, hakumaanisha Dr. Slaa. Alikuwa akikanusha kutumwa na mafisadi na kusema kwanza hawajui hao mafisadi ni kina nani na kuuliza kwanza neno fisadi ni nini?. Ndipo akatoa tafsiri ya kamusi. Unachotakiwa wewe kufanya ni
kutafuta kamusi, soma neno fisadi ndipo ubishe alichokitamka mama Makinda.
 
- You know what, tutalipeleka pabaya sana hili taifa kama tutadai kujua the meaning ya neno ufisadi as we want ndio should be our litimus test ya nani kiongozi anayefaa na asiyefaa, wananchi tufike mahali tukubali kwamba somebody had to be a new Speaker baada ya Mh. Sitta,

- Na ilikuwa ni lazima atoke kwenye chama chenye majority bungeni in this case CCM, sasa tumpe nafasi Spika mpya afanye kazi yake mpya kwanza ndio tumuhukumu!



William.
 
Wajameni, nilikuwepo kwenye hiyo press conference yake, aliposema mafisadi ni wezi wa wake za watu, hakumaanisha Dr. Slaa. Alikuwa akikanusha kutumwa na mafisadi na kusema kwanza hawajui hao mafisadi ni kina nani na kuuliza kwanza neno fisadi ni nini?. Ndipo akatoa tafsiri ya kamusi. Unachotakiwa wewe kufanya ni
kutafuta kamusi, soma neno fisadi ndipo ubishe alichokitamka mama Makinda.

Wewe nawe unachekesha: mara umesema alisema (makinda) 'mafisadi ni wezi wa wake za watu' halafu tena unasema akauliza maana ya neno 'mafisadi'! Yaani alitoa maana ya neno 'fisadi' tena akataka kujua maana ya neno hilo? Hii yawezekana kweli? Ujue kitu halafu tena usikijue?
 
Kamusi gani hiyo inayotoa maana ya neno fisadi kuwa ni wezi wa wake za watu (ingawa dhana nzima naikataa)? Na wezi wa waume za watu nao wanaitwaje sasa?
 
Wajameni, nilikuwepo kwenye hiyo press conference yake, aliposema mafisadi ni wezi wa wake za watu, hakumaanisha Dr. Slaa. Alikuwa akikanusha kutumwa na mafisadi na kusema kwanza hawajui hao mafisadi ni kina nani na kuuliza kwanza neno fisadi ni nini?. Ndipo akatoa tafsiri ya kamusi. Unachotakiwa wewe kufanya ni
kutafuta kamusi, soma neno fisadi ndipo ubishe alichokitamka mama Makinda.
Unatakiwa ukiwa mwanasiasa uwe makini sana wakati unapoongea. Ukiweka kwenye context ya kisiasa nchini Tanzania kwa wakati huu, ufisadi unamaanisha ni wizi wa mali ya umma. Hiyo haina haja ya kwenda shule kujua hivyo. Kwa hiyo kusema kuwa huwajui mafisadi na kutoa tafsiri yako katika kamusi, huko ni kupoteza mwelekeo wa mazungumzo.
 
Pasco said:
Wajameni, nilikuwepo kwenye hiyo press conference yake, aliposema mafisadi ni wezi wa wake za watu, hakumaanisha Dr. Slaa. Alikuwa akikanusha kutumwa na mafisadi na kusema kwanza hawajui hao mafisadi ni kina nani na kuuliza kwanza neno fisadi ni nini?. Ndipo akatoa tafsiri ya kamusi. Unachotakiwa wewe kufanya ni
kutafuta kamusi, soma neno fisadi ndipo ubishe alichokitamka mama Makinda.

Pasco,

..Mama Makinda ameulizwa kuhusu mafisadi kulingana na tafsiri ya neno hilo ktk siasa za leo za Tanzania.

..hivi ina maana akiulizwa kuhusu "vigogo" atasema ni vipande vya miti?

..hilo lilikuwa swali la mtego na kutokana na majibu yake amekwepa mtego mmoja na kutumbukia kwenye mtego mwingine.

..huyu ndiye anayedai kwamba amekuwa mbunge "maisha yake yote" halafu anashindwa kujibu maswali mapesi kama aliyoulizwa.

..so far naona kitakachomharibia Mama Makinda ni hii tabia ya kujibu maswali kwa jazba.

NB:

..Mama Makinda hakuwa kwenye timu ya kampeni ya uraisi ya Edward Lowassa mwaka 1995??
 
Like her Party's leaders, she has no vision nor direction. May the Almighty God show her the Light.
 
Pamoja na mambo kwenda ndivyo sivyo mimi nadhani kwanza tumpe mama nafasi aanze kazi yake mpya tuone utendaji wake. Vinginevyo yote tutakayoongea itakuwa ni hisia tu.
 
Pasco,

..Mama Makinda ameulizwa kuhusu mafisadi kulingana na tafsiri ya neno hilo ktk siasa za leo za Tanzania.

..hivi ina maana akiulizwa kuhusu "vigogo" atasema ni vipande vya miti?

..hilo lilikuwa swali la mtego na kutokana na majibu yake amekwepa mtego mmoja na kutumbukia kwenye mtego mwingine.

..huyu ndiye anayedai kwamba amekuwa mbunge "maisha yake yote" halafu anashindwa kujibu maswali mapesi kama aliyoulizwa.

..so far naona kitakachomharibia Mama Makinda ni hii tabia ya kujibu maswali kwa jazba.

NB:

..Mama Makinda hakuwa kwenye timu ya kampeni ya uraisi ya Edward Lowassa mwaka 1995??

Joka kuu nina hasira sana na huyu mama kiukweli lakini imebidi nicheke tu kwamba akiulizwa kuhusu vigogo atasema ni vipande vya miti .. huu umetoa mfano mzuri sana maana nilikuwa nikijaribu kufikiria niandike kitu gani kieleweke kwa urahisi but thanx that u made it clear.
 
- You know what, tutalipeleka pabaya sana hili taifa kama tutadai kujua the meaning ya neno ufisadi as we want ndio should be our litimus test ya nani kiongozi anayefaa na asiyefaa, wananchi tufike mahali tukubali kwamba somebody had to be a new Speaker baada ya Mh. Sitta,

- Na ilikuwa ni lazima atoke kwenye chama chenye majority bungeni in this case CCM, sasa tumpe nafasi Spika mpya afanye kazi yake mpya kwanza ndio tumuhukumu!


William.

Taifa letu tayari liko mahali pabaya sana kama bado hujaelewa hivyo pole sana. Tunachojaribu sasa ni kulitoa hapa mahali pabaya tulipo. Na adui mkubwa sana aliyetupeleka hapa pabaya ni ufisadi. Sasa kama mheshimiwa Speaker mpya hajui ufisadi anatupeleka kwenye kamusi, basi hatufai kwa kazi iliyo mbele yetu. Hakuna mwenye ugomvi na ccm, kama unavyodai ni 'chama chenye majority bungeni' nikinukuu maneno yako. Lakini kauli ya mama Makinda kuhusu definition ya neno fisadi bila kuelewa context ya neno hilo katika siasa za nchi yetu inaonyesha wazi kuwa hatufai. Kazi yake ameshaanza si ameshaapishwa na kufanya press conference? Na alikuwa naibu speaker kwa kipindi kilichopita? Tumpe nafasi ipi zaidi ya hapo? Tumechoshwa na mahali pabaya tulipofikishwa, tunatafuta namna ya kutoka kwenye hii nightmare!!!
 
Huyu Speaker Mpya hana jipya bali anaturudisha nyuma badala ya kusonga mbele kama taifa, kiswahili kinakuwa kila siku. Kumbe akiulizwa maana ya neno "kuchakachua" atatafsiri kizamani kuwa ni kuchanganya ulanzi uliolala kuchachusha ulanzi mpya ili iwe pombe! Huu ni upuuzi unaofaa kupuuzwa na tusitegemee wabunge wa upinzani kupata ushirikiano toka kwake. Ameanza vibaya na lazima ata,aliza vibaya na atakisambaratisha chama chake kabla ya 2015. Kwa staili hii ni sawa na kuwasafisha mafisadi toka kwenye matope yao.
 
Back
Top Bottom