Ni kwanini Wasabato wanakataza wanawake kufundisha ama kuwa wachungaji wakati wanatumia vitabu vya Hellen G White? Iweje nyama ikataliwe mchuzi unywe?

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Sababu ya kukataza.

1Timotheo 2:12 >> Simruhusu mwanamke yeyote kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya wanaume (ibadani). Mwanamke anapaswa kukaa kimya.

Wasabato hawaruhusu mwanamke kufundisha kanisani au kuwa mchungaji cha ajabu wanatumia mafundisho ya moja wa waanzilishi wa kanisa hilo Hellen G White.

Tena utaratibu wa wasabato ni kwamba wana vitabu maalum vya mafundisho ya kila miezi mitatu, vitabu hivi vinaitwa lesoni na kila mwaka kuna lesoni 4, lesoni hizi zina mafundisho madogo ya kila wiki ambayo yamegawanywa zaidi usome kila siku, jumamosi asubuhi kabla ya ibada wanakutana kujadiliana hilo fundisho la wiki kwenye vikundi.

Sasa iweje kwamba Hellen aruhusiwe kufundishe ila wanawake wengine wakatazwe?
 
Kawailize kama umelijua Hilo basi huenda uliwaasi otherwise angalia vizuri msingi WA biblia inasemaje kuhusu wanawake kufundisha? Mbili elewa tofauti kati ya kuhubiri, kutoa seminar, na kufundisha. Mwandishi WA vitabu ni lazima awe muhubiri?
Kama wewe ni mkristo tafuta kumjua Mungu zaidi ya materialistic things.Barikiwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom