Ni ipi maana halisi ya kumkomboa Mwanamke?

Ni ipi maana halisi ya kumkomboa Mwanamke?

Kisai

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2018
Posts
29,126
Reaction score
29,345
Nawaamkia kwa maamkizi wote watoto na wavyele.

Huu ni muendelezo wa pale nilipoishia katika mada zangu kuwahusu hawa wenzetu, wenzetu ambao ni mama zetu, dada zetu, jirani zetu, watoto wetu na wake zetu pia.

Kila siku tunasikia mikutano, matamasha, makongamano na sherehe pia ya kuwa Mwanamke amekombelewa kutoka katika dhiki na manyanyaso au anaendelea kukombolewa.

Swali langu amekombelewa toka wapi na sasa yuko wapi na ipi faida ya kukombolewa Mwanamke na hasara zake ni zipi?

Tanbihi: Hamasa hasi na mihemko hapa si mahala pake, bali hoja na bayana na upole na uadilifu hapa ndiyo mahala pake.

Karibuni sana.
 
Jiulize mkeo umemfunga mpaka atake kukombolewa?

Huduma zote nyumbani anapata,upendo wote umempa,kwanini aingie huko? Kama sio kutaka madaraka zaidi,wengi wao ni wale walioshindikana kwa waume sasa ili kujifariji wanajiona bila wanaume wanaweza kumbe ni uongo.

Ukikutana mwanaharakati m1 muule kama kweli umejikomboa,na bila mwanaume unaweza tamaa ya ngono unaimaliza vipi? Kama ana hawara bado wanawake hawawez bila wanaume
Umesema kweli kabisa.
 
Binafsi sio mwanamke anaetaka kukombolewa bali naona kuna uongo ndani yake.

Mwanaume ukikubali mkeo akaingia kwenye harakati hizi nyumba yenu imekwisha.
Hivi unajua kuna mila ambazo hadi leo zinakeketa wanawake?
Unajua kuna maeneo hadi leo mwanamke ruhusiwi kusoma na anaozwa akiwa na miaka 6 kwa lizee la miaka 50?

Unajua kuwa wanawake wangapi wapo kwenye ndoa lakini wananyanyasika? Mume haachi matumizi akirudi kalewa anapiga kwanzia mke hadi watoto?

Hayo ni machache, msiwe mnajadili mambo ambayo hamyajui .
 
Kila siku tunasikia mikutano, matamasha, makongamano na sherehe pia ya kuwa Mwanamke amekombelewa kutoka katika dhiki na manyanyasho au anaendelea kukombolewa.

Swali langu amekombelewa toka wapi na sasa yuko wapi na ipi faida ya kukombolewa Mwanamke na hasara zake ni zipi?

Jibu umeshaliandika.

Anakombolewa kutoka kwenye dhiki na manyanyaso na kutokuwa na elimu, na kukeketwa na kuozwa kwa lazima.

Faida zake ni, Sasa hivi wanawake wana elimu, wanafanya kazi wanajisimamia wenyewe. Yaaani tunang'araaaaa.

Hamna hasara labda kwa wanaume wasiojiamini.
 
Every man needs a woman,
Every woman needs her man,
Sharing a world so free,
You've got your love and i've got mine and then we put them together cause they gonna work so fine.
 
Jibu umeshaliandika.
Anakombolewa kutoka kwenye dhiki na manyanyaso na kutokuwa na elimu, na kukeketwa na kuozwa kwa lazima.
Faida zake ni, Sasa hivi wanawake wana elimu, wanafanya kazi wanajisimamia wenyewe. Yaaani tunang'araaaaa.

Hamna hasara labda kwa wanaume wasiojiamini.
Umejibu vyema lakini nadhani wengi wa kimjini mjini hawajui kuwa huko vijijini bado kuna wenzao wanakeketwa, wanaachishwa shule n.k , mfumo dume uliopo mijini na vijijini ni tofauti sana huko vijijini ni kama ukoloni kabisa, hizi harakati inabidi zielekeze nguvu ziadi huko vijijini ndani ndani
 
umejibu vyema lakini nadhani wengi wa kimjini mjini hawajui kuwa huko vijijini bado kuna wenzao wanakeketwa, wanaachishwa shule n.k , mfumo dume uliopo mijini na vijijini ni tofauti sana huko vijijini ni kama ukoloni kabisa, hizi harakati inabidi zielekeze nguvu ziadi huko vijijini ndani ndani
Na hii ndio dhumuni ya hizo harakati, kufikia hayo maeneo na kumkomboa huyo mwanamke.

Mtoa mada na wenzake hawafuatilii kusudi la hizo harakati ni nini, wao wanafuatilia hawa slay kwini wa mjini wanaojificha kwenye kivuli cha hizo harakati. Ndio maana tunaona mada kama hizi.

Kitu chochote kinaanzaga vizuri ila hawakosekani watu wa kuingiza maslahi yao, sasa hiyo haimaanishi hicho kitu ni kibaya au kiachwe. Cha msingi ni mtu kujua chanzo. Kitu kilianzishwa kwa dhumuni gani.
 
Moja ya sera ya ukombozi kwa wanawake ni kuwafanya wawe 50/50 na wanaume, usawa kwa wote, wote wawe na final say , mwanamke awe 'kichwa' kama mume, kitu ambacho hakipo

Uko seminani wanajazana ujinga tu

Mwanamke siku zote yupo chini ya mwanamume, hakuna cha ukombozi wala babu yake ukombozi
 
Jibu umeshaliandika.
Anakombolewa kutoka kwenye dhiki na manyanyaso na kutokuwa na elimu, na kukeketwa na kuozwa kwa lazima.
Faida zake ni, Sasa hivi wanawake wana elimu, wanafanya kazi wanajisimamia wenyewe. Yaaani tunang'araaaaa.
Hakuna jibu nililo andika hapo, zaidi ya kuwasilisha yale tunayo yasikia katika vikao vyenu.

Ndiyo utueleze faida za kujisimamia wenyewe, kupata elimu katika kuistawisha jamii na kulea jamii? Hayo mafanikio yanu yamewasaidia katika hilo?

Ama kuhusu kung'ara,hapa unatakiwa utuambie kung'ara kwenye nini ?
Hamna hasara labda kwa wanaume wasiojiamini.
Kama huoni hasara basi wewe bado upo katika giza la harakati hizo, na si mkweli.

Hivi huwezi kuwa mwanadamu kamili bila kujilinganisha na mimi ?

Kwanini kila nachofanya mimi na wewe unataka kufanya ? Huwa mnatafuta haki sawa au kufanana kwa haki ?
 
Huu ukweli huwa hawaukubali ila kiukweli wanapoteza sana.

Ndiyo maana huko juu nimesisitiza ya kuwa wawe wakweli, lakini kwa masikitiko makubwa wanajifariji na ukweli hawausemi.
 
Anakombolewa kutoka katika sheria kandamizi za kiutamaduni na kidini, ambazo zinamnyika haki yake mfano kwenye urithi watoto wote ni sawa kwanini mwanaume achukue kingi kuliko mwanamke, mfano wa tabia kama hizi lazima zifike mwisho
 
Hivi unajua kuna mila ambazo hadi leo zinakeketa wanawake?
Unajua kuna maeneo hadi leo mwanamke ruhusiwi kusoma na anaozwa akiwa na miaka 6 kwa lizee la miaka 50?
Unajua kuwa wanawake wangapi wapo kwenye ndoa lakini wananyanyasika? Mume haachi matumizi akirudi kalewa anapiga kwanzia mke hadi watoto?

Hayo ni machache, msiwe mnajadili mambo ambayo hamyajui .
Mwanamke ni mwanamke na mwanaume ni mwanaume.

Mwanamke hawezi kuwa mwanaume na mwanaume hawezi kuwa mwanamke.

Tutaendelea kubishana lakini huo ndio uhalisia na haubadiliki unless Mungu aumbe ulimwengu mpya.
 
Ajabu ipo wapi kuwa zaidi ya mwanaume? Kama uwezo anao kumzidi mwanaume kuwa mpole
Yaan kwa kifupi ni kwamba mwanamke pia alizaliwa kwa kusudi la Mungu na ana ndoto zake za kutimiza maishani, aachwe atomize ndoto zake hata ziwe kubwa vipi asiwekewe vikwazo kama vilivyopo sasa hiv kwenye jamii kwa ujumla.

Heshima kwa mume mke anayo tuuu akiwa Hana chochote na zaidi anayo Sana akiwa ana mume anayesupport kutimiza ndoto zake.

Maisha yanakua matamu mnooo. Sio mume akiona mke anauwezo anapambana kumgandamiza kwa madai hatakiwi kuwa na uwezo ohh kisa wewe ni mwanaume, uwezo wa mke hauwi limited na uwezo wa mume.
 
Mjadala siku zote huwa ni kwa mambo ambayo hatuyajui na yenye utata. Sa jambo kama unalijua utalijadili la nini?
 
Back
Top Bottom