Kuondolewa kwa posho za semina, mambo ya salary increment, kuongezeka kwa umakini kwenye taasisi za umma kama TRA, TPA, kumefamya watu waseme pesa imekuwa ngumu.
Kukosekana kwa masoko ya mazao, ukosefu wa ajira za serekali,kubana matumizi ya serekali, kumefanya watu waseme pesa imekuwa ngumu.
Kwa mtazamo wangu nadhani mabadiliko ya kiuongozi yatasababisha mabadiliko ya sura ya uchumi.Wakati wa JK ilikuwepo dhana ya 'maisha magumu', sasa ni pesa imepotea....baadhi ya watu wanapokea kauli na kuzikuza bila kuangalia uhalisia wake.
Utamkuta mtu maisha yake yapo steady kama miaka ya nyuma ila naye anaimba pesa imepotea.