Ni hela ipi ndo imekuwa ngumu?

Ni hela ipi ndo imekuwa ngumu?

Ndo tatizo lenu... unataka kusema hizo meli hewa zilikuwepo kwavile hapakuwa na hiyo VAT?
Mkuu nianze na hili kwanza.

Uhusiano wa VAT na Meli upo na ni wa moja kwa moja.

Wafanyabiasha waliolipa mfano milioni 7 (takribani dola 2000) waliingiza mizigo mingi kupitia 'kwa mtu kariakoo' aliyekuwa na dili na bandari.

Kumbe thamani ya kontena ni milioni 40 sawa na dola 20,000.

Wafanyabiashara iwe wa ndani au jirani walitumia fursa hiyo.
Kukawa na hiyo 'multiplier effect' unayosema ikichagiza 'inflation'

Wameambiwa walipe kiwango halali wanakwenda kwingine ambapo badala ya dola 20,000 wanaweza kulipa 14,000 ikiwa ni mara 2 ya ile ya dili na wao kubaki na 6,000.

Kuondokakunapunguza mizigo na kupungua mizigo kunapunguza meli zinazotia nanga.
Hivyo uhusiano wa VAT na Meli upo

Ninachoweza kukubaliana nawe ni kimoja, kuwa lazima kuangalia masoko mengine na kuifanya bandari iwe competitive na si suala la kusema mameli yasije.

Si suala la kuacha mizigo iingie bila kodi huku wahuni wachache wakitia mifukoni

Morogoro rd, kila baada ya km 2 kuna kituo cha mafuta.
Leo tunajua walikuwa hawalipi kodi kwasababu mita zilizuiwa kufanya kazi, ilikuwa dili tu.

Hiyo ndiyo multiplier effect mnayosema?

Vituo havijaambiwa vifunge, bali vilipe kodi ya bandari. Je, hilo ni baya?

Kuhusu bandiko lako 175 nitarudi tuzungumze
 
Well, umeeleza vema. Tunajua pia hakujatokea maafa yakaua watu kwa kiasi cha kutisha. Wateja wako wapo pale pale. Ni kwanini hawatumii kama walivyokuwa wanatumia siku za nyuma?
Kwa sababu na wao kwenye sehemu yao kipato fedha imepungua,,,mkuu kuna sehemu nyingi watu wamepunguzwa kazi ,,jamaa yangu aliajili vijana 6,ila kapunguza hadi kabakiwa na wawili kwa sababu mzunguko kwenye biashara,so tusishadadie tu wakati hata raisi alikili kwamba pesa hakuna mtaani
 
Kwa sababu na wao kwenye sehemu yao kipato fedha imepungua,,,mkuu kuna sehemu nyingi watu wamepunguzwa kazi ,,jamaa yangu aliajili vijana 6,ila kapunguza hadi kabakiwa na wawili kwa sababu mzunguko kwenye biashara,so tusishadadie tu wakati hata raisi alikili kwamba pesa hakuna mtaani
sawa sawa, kupunguzwa kazi kwa watu ni kwasababu hakuna uwezo wa kuwalipa.

Swali linabaki pale pale, zile pesa zilizowezesha walipwe zilitokana na biashara, sasa kwanini watu hawanunui tena?

Hapa hakuna ushabiki tunaongelea uhalisia.
Kama mfanyakazi aliweza kujenga nyumba na wewe kukupa biashara ya hardware, mfanyakazi huyo katika wadhifa , idara na wizara ile ile nini kinamkwaza?

Pili, kama mzunguko wa pesa umepungua, unashauri nini kifanyike urudi hali ya kawaida?
 
Hili swali nimeuliza sana
Ikiwa wateja ni wale wale wakiwa wameajiriwa kule kule, nini hasa kimetokea hawatumii tena pesa?

Na wanaosema hakuna pesa, wanashauri nini kifanyike irudi mtaani?

Niliowauliza wamekimbia, mbele ya safari wataibuka tena pesa hakuna
teh teh teh hawachelewi kusema sababu ya VAT
 
Mkuu nianze na hili kwanza.

Uhusiano wa VAT na Meli upo na ni wa moja kwa moja.

Wafanyabiasha waliolipa mfano milioni 7 (takribani dola 2000) waliingiza mizigo mingi kupitia 'kwa mtu kariakoo' aliyekuwa na dili na bandari.

Kumbe thamani ya kontena ni milioni 40 sawa na dola 20,000.

Wafanyabiashara iwe wa ndani au jirani walitumia fursa hiyo.
Kukawa na hiyo 'multiplier effect' unayosema ikichagiza 'inflation'

Wameambiwa walipe kiwango halali wanakwenda kwingine ambapo badala ya dola 20,000 wanaweza kulipa 14,000 ikiwa ni mara 2 ya ile ya dili na wao kubaki na 6,000.

Kuondokakunapunguza mizigo na kupungua mizigo kunapunguza meli zinazotia nanga.
Hivyo uhusiano wa VAT na Meli upo

Ninachoweza kukubaliana nawe ni kimoja, kuwa lazima kuangalia masoko mengine na kuifanya bandari iwe competitive na si suala la kusema mameli yasije.

Si suala la kuacha mizigo iingie bila kodi huku wahuni wachache wakitia mifukoni

Morogoro rd, kila baada ya km 2 kuna kituo cha mafuta.
Leo tunajua walikuwa hawalipi kodi kwasababu mita zilizuiwa kufanya kazi, ilikuwa dili tu.

Hiyo ndiyo multiplier effect mnayosema?

Vituo havijaambiwa vifunge, bali vilipe kodi ya bandari. Je, hilo ni baya?

Kuhusu bandiko lako 175 nitarudi tuzungumze
Hapa tunachanganya mambo!!! Kuna meli 60 ambazo tunaambiwa zilitoroka bila kulipa kodi... hilo ni jambo moja! Ninachozungumzia mimi ni watu ambao wameacha kutumia bandari baada ya ku-impose VAT kwa Mawakala wa Forodha! Mawakala wa Forodha nao waka-pass VAT Burden kwa waagizaji bidhaa kutoka nje na hivyo kuongeza import costs! Walipoona hivyo, watu wakaacha kutumia Bandari ya Dar es salaam na wakakimbilia kule ambako ama no tax on transit goods au kodi hiyo ni ndogo sana!

Utetezi wa serikali ilikuwa kwamba hawaku-impose VAT to Transit Goods (kwavile haikubaliki) bali kodi hiyo ni kwa Mawakala wa Forodha but practically, kila mmoja anafahamu Tax Burden inakuwa passed from one service user to another! Sasa ingawaje ni kweli serikali haiku-impose tax on transit goods bali kwa mawakala; mawakala nao wakai-pass hiyo kodi kwa importers... meaning to transit goods! Sasa hili halina uhusiano wowote na utorokaji wa meli 60!!

Ninachokisema hapa ni kile ambacho kilipata kuripotiwa hapo kabla na The Citizen.

TRA.png


Kwahiyo TRA hapo walitaka kuaminisha watu kwamba zigo hilo VAT Mawakala wa Forodha wasingetafuta wa kumdondoshea!!!! Ni wafanyabiashara wa nchi gani hao wanaokubali kujitwisha zigo la kodi wao wenyewe na sio kutafuta wa kumtupia?!

Vituo havijaambiwa vifunge... sawa; hoja hapa ni kwamba kutokana na maamuzi ya hovyo, meli zimepungua na hivyo mzigo kupungua na matokeo yake kuathiri sekta zingine! Marine Traffics hawa hapa wanatuonesha meli zilizopo na zinazotarajiwa kuingia bandari ya Dar... kisha linganisha na nchi zingine!!
Dar.png


Mombasa hawa hapa chini:
Mombasa.png


Bandari za Msumbiji hizi hapa:
Maputo.png


Lugha nyepesi ambazo zinazungumzwa na watawala na wafuasi wao ni kwamba "wakimbie tu, walikuwa wakwepa kodi hao!" Sasa ina maana huko walikoenda nako hawalipi kodi sio? Kwenye uchumi kuna kitu kinaitwa Comparative Advantage... kwamba, mtu anaweza ku-sacrifice X in exchange for Y but net outcome ni low cost! Kwamba, fine impose VAT but you've railway network ambayo transporter atafanya comparative analysis kwamba; hawa Jamaa wana VAT but they have good railway system ambayo ina-lower transport cost na wale kule no VAT on transit goods but poor railway system ambayo ina-higher transport costs! Hapo atafanya hesabu za "on" and "off" na ikiwa mwisho wa yote atakuta total cost kupitia Dar ni ndogo hata kama kuna VAT, anaweza ku-sacrifice/ku-forgo non VAT destination! Sasa nchi yenyewe haina aina comparative advantage lakini bado una-impose ma-VAT ambayo hayakutakiwa kuwapo!!

Anyway,lakini watakuja wengine watakuambia "mbona meli zimeongezeka" "mbona mapato yameongezeka" huku wakisahau kwamba hata kama hiki na kile kimeongezeka lakini kipo chini ya kile ambacho tulistahili!
 
Naongelea upigaji bandarini in general. Kusema wamefanywa nini wakati unajua kesi zao zipo kwenye hatua mbalimbali ni kujitoa ufahamu bila ya sababu. Bakhresa bidhaa zake zilizuiliwa kwa sababu ya issue za kodi mbalimbali.
Kulipa kodi ni suala moja, wafanyabiashara hao hao wanaolipa kodi, kuweza kupatiwa ushirikiano na serikali ni suala jingine.
Akina nani ambao unasema kesi zao zipo hatua mbalimbali?! Nitajie mfanyabiashara mmoja manake naona na hapa unataka kuchanganya kati ya wafanyabiashara waliokuwa wanatorosha makontena na akina Masamaki! Nitajie hao wafanyabiashara ambao kesi zao zipo katika hatua mbalimbali!!!!

Kuhusu upigaji in general basi hoja ulileta pasipostahili manake mimi nilikuwa nazungumzia suala lingine!!!
 
Hela ngumu ni silver za 200 & 500 noti zote laini
 
sawa sawa, kupunguzwa kazi kwa watu ni kwasababu hakuna uwezo wa kuwalipa.

Swali linabaki pale pale, zile pesa zilizowezesha walipwe zilitokana na biashara, sasa kwanini watu hawanunui tena?

Hapa hakuna ushabiki tunaongelea uhalisia.
Kama mfanyakazi aliweza kujenga nyumba na wewe kukupa biashara ya hardware, mfanyakazi huyo katika wadhifa , idara na wizara ile ile nini kinamkwaza?

Pili, kama mzunguko wa pesa umepungua, unashauri nini kifanyike urudi hali ya kawaida?
Mi nadhani wale wezi waliominywa ni kwamba walikuwa wanakuja kutumia mtaani na kufanya mzunguko uongezeke,mfano mtu alikuwa akiiba huko mishahara hewa anaenda bar,kule bar anafanya muuza bia auze bia nyingi na kuajili wafanyakazi wa kutosha.....n.k mi nadhani raisi kwa kuwa kaziba ile mianya ya udokozi wa pesa ambapo hata walala hoi tulikuwa tunafaidi ,basi atafute njia mbadala
Mfano fisadi akiiba anajenga nyumb au kupaka rangi nyumba,unadhani anakuwa ametoa ajira kwa watu wangapi hapo?
 
Na Mimi nauliza tu kaswali kidogo, je kama ni kweli hela imeadimika kwa sababu zozote zile, kwa nini bei haipungui bali inazidi kupanda?
 
Na Mimi nauliza tu kaswali kidogo, je kama ni kweli hela imeadimika kwa sababu zozote zile, kwa nini bei haipungui bali inazidi kupanda?
Katika uchumi ni kawaida kuona uchumi ukidorora na hela kukosekana, kasi ya kupanda bei kupungua au bei kupungua.

Lakini katika miaka ya karibuni kuna kitu kinatokea, wataalamu wanakiita stag-flation.

Stagflation ni muungano wa economic stagnation (which normally comes with deflation) but in this case it comes with inflation.

stag·fla·tion

ˌstaɡˈflāSH(ə)n/

noun

ECONOMICS

persistent high inflation combined with high unemployment and stagnant demand in a country's economy.

Stagflation - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Katika uchumi ni kawaida kuona uchumi ukidorora na hela kukosekana, kasi ya kupanda bei kupungua au bei kupungua.

Lakini katika miaka ya karibuni kuna kitu kinatokea, wataalamu wanakiita stag-flation.

Stagflation ni muungano wa economic stagnation (which normally comes with deflation) but in this case it comes with inflation.

stag·fla·tion

ˌstaɡˈflāSH(ə)n/

noun

ECONOMICS

persistent high inflation combined with high unemployment and stagnant demand in a country's economy.

Stagflation - Wikipedia, the free encyclopedia
Nadhani chige na juvenile davis watapata majibu hapa. Key words 'the action designed to lower inflation my exacerbate unemployment or vice versa''

Kwa mtazamo wangu situation iliyopo kuna 'factor' nyingine 'Fanaticism'

Maamuzi yanalenga siasa, hayapimwi kitaalam na watalaam ni kama wameingiwa na woga
 
Hakuna kielelezo chochote cha kuonyesha hela hakuna mitaani. Ni porojo tu za kawaida.

Mnasema kulikuwa na hela? Wakati elimu bure ilipoanza primary school enrollment imeonngezeka Mara mbili. Hiyo inaonyesha nini?

Toeni vielelezo au angalia simple logic. Siyo kusema mitaani hali mbaya. Hiyo haitoshi kuelezea chochote.

Ni porojo tu, hakuna data.
 
Akina nani ambao unasema kesi zao zipo hatua mbalimbali?! Nitajie mfanyabiashara mmoja manake naona na hapa unataka kuchanganya kati ya wafanyabiashara waliokuwa wanatorosha makontena na akina Masamaki! Nitajie hao wafanyabiashara ambao kesi zao zipo katika hatua mbalimbali!!!!

Kuhusu upigaji in general basi hoja ulileta pasipostahili manake mimi nilikuwa nazungumzia suala lingine!!!
Kaka walipewa grace time na wengi wao walipambana na kutafuta pesa kila walipoweza.

Wapo wafanyabiashara ndugu yangu usipende sana ligi isiyokuwa na tija kwako wala kwangu.

Yule wa milioni saba kwa kila dakika ambaye yupo chini ya mikono salama, umemsahau?. Na hayupo peke yake mind you. Wote ambao walimtengenezea mazingira ya ukwepaji wa kodi na wao suala zima linawahusu.

Yule wa Arusha umemsahau?, issue hizi hizi za kodi.
 
Hili swali nimeuliza sana
Ikiwa wateja ni wale wale wakiwa wameajiriwa kule kule, nini hasa kimetokea hawatumii tena pesa?

Na wanaosema hakuna pesa, wanashauri nini kifanyike irudi mtaani?

Niliowauliza wamekimbia, mbele ya safari wataibuka tena pesa hakuna
Wateja wengi nchi hii ni waajiriwa hasa taasisi za umma. Wafanyakazi taasisi za umma mshahara mdogo walikuwa wanategemea posho za safari etc. Hizo posho ndio zinajenga majumba,zinanunua magari na issue nyingine.

Sasa hawa watu wanebanwa,safari hamna,vikao vya ajabu ajabu hakuna kwahio hela yao waliokuwa wanategemea haipo wanatumia mshahara tu so obvious matumizi yao yatakuwa sio kama zamani.

Wengine ni wale wapiga deal,tender za ajabu ajabu wanapata billions, hamna tena awamu hii. Sasa hawa ndio wateja wabiashara nyingi na wanatoa ajira ndogo ndogo.

Sasa kipato cha hawa kikiathirika wanaathiri hata wale wenye biashara halali kwasababu kwenye biadhara hujui mteja kapata wapi hela. In general mfanyabiashara atasema biadhara hakuna hela mtaani imepotea.
 
Kaka walipewa grace time na wengi wao walipambana na kutafuta pesa kila walipoweza.

Wapo wafanyabiashara ndugu yangu usipende sana ligi isiyokuwa na tija kwako wala kwangu.

Yule wa milioni saba kwa kila dakika ambaye yupo chini ya mikono salama, umemsahau?. Na hayupo peke yake mind you. Wote ambao walimtengenezea mazingira ya ukwepaji wa kodi na wao suala zima linawahusu.

Yule wa Arusha umemsahau?, issue hizi hizi za kodi.
Naona kiongozi unataka kuhamisha magoli! Hapa tunazungumzia watoroshaji wa makontena na sio watu wa 7 Million kwa dakika! Na wala usidhani nampinga JPM kuwaachia wale watu.... kuna cku hapa niliwahi kuongea kwamba sometimes kwenye masuala ya kiuchumi mtu unatakiwa kuchukua hata maamuzi ya kipum'bavu for the sake of net economic outcome! Kwahiyo ingawaje inaweza kuonekana ni maamuzi ya hovyo kusamehe wakwepa kodi but for the sake of microeconomic sector, ilikuwa ni busara kuwaacha ili waendelee kufanya biz.
 
Naona kiongozi unataka kuhamisha magoli! Hapa tunazungumzia watoroshaji wa makontena na sio watu wa 7 Million kwa dakika! Na wala usidhani nampinga JPM kuwaachia wale watu.... kuna cku hapa niliwahi kuongea kwamba sometimes kwenye masuala ya kiuchumi mtu unatakiwa kuchukua hata maamuzi ya kipum'bavu for the sake of net economic outcome! Kwahiyo ingawaje inaweza kuonekana ni maamuzi ya hovyo kusamehe wakwepa kodi but for the sake of microeconomic sector, ilikuwa ni busara kuwaacha ili waendelee kufanya biz.
Wenye kuhamisha magoli ni wale jamaa wa ufipa na wala sio mimi. Wenye makontena na huyu wa milioni saba kwa dakika na yule wa Arusha wote ni wafanyabiashara. Ukijenga tabia ya kusamehe watu kodi, kuna ambao kwa makusudi kabisa watataka kuwaumiza wanyonge kwa sababu hizo hizo halali za kibiashara.
Lazima uwe ni utamaduni kwa kila mtu kulipa kodi whether biashara zake zina impact kwa micro economic sectors au hazina.
Wanafungwa jela kina Wesley Snipes na wengine maarufu zaidi yake kwa sababu za ukwepaji wa kodi, why hawa wa kwetu wapewe special priorities all the time?.
 
Watu wanamlalamikia sana Magufuli katika hili, lakini Mimi binafsi wala halijanugusa kabisa.
Nafanya yao, nalipwa changu. Sema watanzania wengi ni vyuma ulete(Chuma Ulete). Wana Tabia ya kuvuna wasipopanda, ndiyo hao wanao mlalamikia Magufuli.
 
Wenye kuhamisha magoli ni wale jamaa wa ufipa na wala sio mimi. Wenye makontena na huyu wa milioni saba kwa dakika na yule wa Arusha wote ni wafanyabiashara. Ukijenga tabia ya kusamehe watu kodi, kuna ambao kwa makusudi kabisa watataka kuwaumiza wanyonge kwa sababu hizo hizo halali za kibiashara.
Lazima uwe ni utamaduni kwa kila mtu kulipa kodi whether biashara zake zina impact kwa micro economic sectors au hazina.
Wanafungwa jela kina Wesley Snipes na wengine maarufu zaidi yake kwa sababu za ukwepaji wa kodi, why hawa wa kwetu wapewe special priorities all the time?.
Mazoea ya kusamehe kodi kivipi?! For what I know hakuna aliyesamehewa kodi bali kulikuwa na wakwepa kodi ambao badala ya kupelekwa mahakamani, waliambiwa walipe pesa wanazodaiwa na yakaisha!

Hili ndilo naliunga mkono cuz' endapo pangekuwa na attempt yoyote ambayo ingesababisha wasiendelee na biashara, damage yake ingekuwa kubwa sana kv walikuwa takribani 200. Moja ya maamuzi ya JPM ambayo nimeyaunga mkono kwa 100% ni hili na ninayopinga ni VAT kwenye Utalii na Mawakala wa Forodha!

Kwenye uchumi kuna namna kuu mbili za kuongeza Revenues... mosi; by increasing sales through price reduction but second, by increasing price keeping cost constant for either practice! Mimi ni mfuasi wa kuongeza mapato by increasing sales through price reduction hususani kama sector husika ipo partially utilized!
 
Back
Top Bottom