Ni hatari sana kwa nchi kutegemea ushauri wa Legal Officer (Hamza Johari), na kuiingiza nchi kwenye mkataba

HANGAYA THE CHIEF

JF-Expert Member
Sep 10, 2021
329
947
Utangulizi:
Katika taaluma ya sheria kote dunia, na kwa kipekee hapa nchini Tanzania, ili mtu akidhi vigezo vya kuwa mshauri, au kuwakilisha watu mahakamani, au kushauri mambo msingi ya kisheria , au kuhakiki nyaraka mbalimbali ni lazima awe na taalum hiyo katika ngazi au nafasi ya uwakili.

Hivyo kwa sababu ni taaluma, ina taratibu zake kuweka kutambulikwa na jumuia wa wataaluma hao katika nchi, kwa mathalani wale waliomaliza shahada za sheria kabla ya 2007 walifanya mitihani iliyotambulika kama bar exams , na wale waliomaliza baada ya 2007 shahada zao, ilianzishwa shule ya sheria kwa vitendo (law school of Tanzania.)

Katika mifumo hiyo yote wanaofaulu wanaomba kupokelewa, na Jaji Mkuu akiwakubalia wanaapishwa na kufanywa kuwa jumuia ya mawakili, wakiwa na majukumu mbalimbali, kama mawakili, mafisa viapo, na waidhinisha nyaraka mbalimbali katika jamii; na mawakili wanaweza kuwa wakujitegemea au mawakili wa serikali.

Kama hujapitia hatua hizo hata ungekuwa una LLD (PhD), LLM. LLB, unaitwa legal officer, na chochote unachotaka kukifanya lazima uwe chini ya wakili (either private or public), kwa sababu hautambuliki kama member in professional fratenity na huna comitment za obligation ya taaluma hiyo. na hivyo ushauri wako sio ushari

Utata:
Ukifuatilia sintofahamu ya Bandari, chimbuko lake kubwa ni mkataba na wala si uwezo wa DP world kama inavyoelezwa na waunga hoja wa waarabu hao, na kimsingi mkataba ni kazi ya sheria moja kwa moja, na yeyote anayetaka kuzungumzia mkataba lazima arejee sheria, au awe na background ya sheria, aidha za mikataba mbalimbali, ikiwepo za ndani na za nje, au uwezo wa kisheria kiujumla.

Kumekuwa na mwanasheria ambaye amejinasibu kuwa alishiriki katika mchakato na kushauri, swali langu Je, "mwanasheria" huyo ni wakili? (private or public) (is he a member of professional fratenity in Tanzania? Jibu ni hapana Hamza Johari si wakili(public or private) inawezekana ni mwanasheria kwa maana labda ana LLD, LLM, LLB, lakini si wakili, na si lawyer by professional, labda ni mwanasheria kwa kumaliza degree za sheria. lakini haonekani katika kanzi data za mahakama (data base) za judiciary.

Kulijua hilo ingia kwenye (tovuti ya mahakama) www.ewakili.judiciary.go.tz. kuna sehemu ya kumjua wakili wako, (know your advocate) ingiza majina utagundua si wakili.

Wale mnaolaumu wanasheria, tujiulize kwanza, Je aliyetoa ushauri wa kisheria ni mwanasheria kwa mujibu wa taaluma yetu ya kisheria?

Na kama si hivyo, aliwezaje kufanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo?
 
Kule kwetu "KUSADIKIKA" propaganda imeshaota mizizi katika kutawala watu, na taaluma ndo ipo hatua ya miche kuja kuongoza watu, ila rutuba ya kuipalilia ndo imejaa uchawa.
Tukutane Cuba, nimeishiwa Cigar mkuu.
 
Hapo sasa ndio utajua wapigaji hawana hata haya. Ulaku tu ndio umetawala myoyo yao. Hiyo concession sijui mkataba haukustahili kupenya popote kwenye ofisi za serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kutokana na masharti ya kibeberu na kikoloni yaliyogubika waraka huo. Hicho kitu kakisema prof mzalendo mama tibaijuka. Wengi tunaona hivyo.

Awamu hii wengi wanaifananisha na awamu ya 4 iliyokua na kashfa kibao kwa mikataba ya ovyo.
 
Unamaanisha ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali haihusiki na DP world,au hukumalizwa ashki kabla hapajakucha!?
 
Utangulizi:
Katika taaluma ya sheria kote dunia, na kwa kipekee hapa nchini Tanzania, ili mtu akidhi vigezo vya kuwa mshauri, au kuwakilisha watu mahakamani, au kushauri mambo msingi ya kisheria , au kuhakiki nyaraka mbalimbali ni lazima awe na taalum hiyo katika ngazi au nafasi ya uwakili.


Na kama si hivyo, aliwezaje kufanya kazi asiyokuwa na taaluma nayo?
Nchi ilibadili sheria kwa wanasheria wa serikali si lazima a some school of law
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Nchi ilibadili sheria kwa wanasheria wa serikali si lazima a some school of law
umeji-misdirect,huyo Hamza Johari siyo State Attorney(Mwanasheria wa Serikali) kiasi cha ku-enjoy hiyo privilege iliyotolewa specifically kwa exprienced State Attorneys kwa wakati huo.Hata hivyo,ukirejea matangazo ya hivi karibuni ya Sekretariat ya Ajira Tanzania,Kusoma na kufaulu Law School ni kigezo cha msingi ili upate kuajiriwa kama Mwanasheria wa Serikali
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine ye
Usiseme hivyo
Tayari kuna MoU ya February 2022 kati DP na TPA
So hatujielewi
 
umeji-misdirect,huyo Hamza Johari siyo State Attorney(Mwanasheria wa Serikali) kiasi cha ku-enjoy hiyo privilege iliyotolewa specifically kwa exprienced State Attorneys kwa wakati huo.Hata hivyo,ukirejea matangazo ya hivi karibuni ya Sekretariat ya Ajira Tanzania,Kusoma na kufaulu Law School ni kigezo cha msingi ili upate kuajiriwa kama Mwanasheria wa Serikali
Tukubali kwenye mkataba Huu hatukuhitaji serikali pekee pia watu kutoka nje so tuwalaumu wote lakini hata tukilaumu hiyo IGA haisaniniwi upya let us cut the crap

What we can do ni kutangaza mgogoro kwa mujibu wa mkataba tusuhishe na kwenda vizuri jambo ambalo hatuongei na hatulioni ikizingatiwa hii ni saini ya pili dhidi ya DP
 
Back
Top Bottom