SACO
JF-Expert Member
- Jul 25, 2011
- 2,318
- 2,912
Niuzie hiyo hiace nina mil 2Mwaka 2019 tu hapo nilishawishiwa na rafiki yangu ninunue hiace moja ilikuwa kazini kwao inauzwa, kumbe ile gari ni kimeo mbaya mbovu, engine haieleweki kabisa, ni zile hiace za NISSAN zenye tabia kama X-Trail ikianza kuharibika....jamaa nilikuwa namuamini sana so sikuwa na haja ya kukagua kivile, alinitumia picha tu nikaridhika nikijua ni marekebisho madogo madogo ya rangi e.t.c! Kitu ambacho sikujua ni kwamba jamaa yangu huyo alikuwa anapata commission kwa kuuza hiyo gari....dah nikazama CRDB nikapewa mkopo nikachukua gari langu nikiwa na matumaini itaingia road irudishe pesa!!! Mpaka navyoandika sasa hivi nimeamua kui-park tu, garage kila siku....mkopo bado natoboka kwenye mshahara wangu na gari haijarudisha hata robo ya pesa