KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 18,143
- 32,884
Habari za muda huu ndugu zanguni.
Mwaka fulani mida ya asubuhi wakati nikiwa kwenye harakati za kuusaka ugali nilidondosha pochi yangu.
Pochi yangu wakati inadondoka ilikuwa na pesa kiasi kama 90,000/= na vitambulisho na kadi zangu za benki na wakati naangusha nilikuwa naelekea benki ya NBC, iliyokuwa njia ya kuelekea quality center mkono wa kushoto ukitokea tazara.
Nilipogundua kuwa pochi yangu haikuwa na mimi hapo hapo nikageuka zangu na kurudi kuelekea kituo cha polisi ili kupata loss report kwa ajili vitambulisho vyangu.
Wakati nipo polisi najiandaa kutoa maelezo nikasikia simu yangu inaita kuangalia ni namba ngeni.
Nikaipokea na sauti ya upande wa pili ukanisalimia kiungwana na kuniuliza kuwa wewe ndio fulani. Nikamjibu ndio akasema yeye ameokota pochi yangu lakini ameshaelekea kariakoo kwenye eneo lake la kazi kwa baadae nikipata nafasi niende kuchukua.
Ni taarifa iliyo nishtua na kunipa mshangao mkubwa sana pamoja na wasi wasi ukizingatia nyakati hizi za sasa.
Yule polisi aliyekuwa anachukua maelezo yangu akauona mshangao wangu na mashaka yangu lakini akanishauri niende Tu hivyo hivyo.
Kwa kufupisha maelezo nilifika pale kariakoo maeneo ya msimbazi nikamkuta na kunipatia pochi yangu ikiwa na vitu vyangu vyote.
Nilipojaribu kutaka kumpatia chochote kitu kama asante yangu kwake alikataa na kujibu kuwa nikiipokea hii pesa wewe utasahau wema wangu na hutawafanyia wengine wema.
Tangu siku hiyo nimekuwa nikirudisha vitu au vifaa vingi ninavyookota kwa kuwatafuta wenyewe.
Je, wewe ulishawahi kuokota mali au kitu cha mtu na kumrudishia mwenyewe?
Mwaka fulani mida ya asubuhi wakati nikiwa kwenye harakati za kuusaka ugali nilidondosha pochi yangu.
Pochi yangu wakati inadondoka ilikuwa na pesa kiasi kama 90,000/= na vitambulisho na kadi zangu za benki na wakati naangusha nilikuwa naelekea benki ya NBC, iliyokuwa njia ya kuelekea quality center mkono wa kushoto ukitokea tazara.
Nilipogundua kuwa pochi yangu haikuwa na mimi hapo hapo nikageuka zangu na kurudi kuelekea kituo cha polisi ili kupata loss report kwa ajili vitambulisho vyangu.
Wakati nipo polisi najiandaa kutoa maelezo nikasikia simu yangu inaita kuangalia ni namba ngeni.
Nikaipokea na sauti ya upande wa pili ukanisalimia kiungwana na kuniuliza kuwa wewe ndio fulani. Nikamjibu ndio akasema yeye ameokota pochi yangu lakini ameshaelekea kariakoo kwenye eneo lake la kazi kwa baadae nikipata nafasi niende kuchukua.
Ni taarifa iliyo nishtua na kunipa mshangao mkubwa sana pamoja na wasi wasi ukizingatia nyakati hizi za sasa.
Yule polisi aliyekuwa anachukua maelezo yangu akauona mshangao wangu na mashaka yangu lakini akanishauri niende Tu hivyo hivyo.
Kwa kufupisha maelezo nilifika pale kariakoo maeneo ya msimbazi nikamkuta na kunipatia pochi yangu ikiwa na vitu vyangu vyote.
Nilipojaribu kutaka kumpatia chochote kitu kama asante yangu kwake alikataa na kujibu kuwa nikiipokea hii pesa wewe utasahau wema wangu na hutawafanyia wengine wema.
Tangu siku hiyo nimekuwa nikirudisha vitu au vifaa vingi ninavyookota kwa kuwatafuta wenyewe.
Je, wewe ulishawahi kuokota mali au kitu cha mtu na kumrudishia mwenyewe?