St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,634
- 4,519
Kuna jamaa mmoja alioa mke mrembo ambaye wazazi wake waliishi kama kilomita 20 toka alipokuwa anaishi jamaa huyo.Tatizo lilijitokeza siku ya kwanza mke alipoingia ndani,ile kuandaa ugali mezani jamaa akagundua kuwa ulikuwa mbichi,ukamwagwa.Siku ya pili,vilevile na ya tatu jamaa akachoka na kuchukua chungu cha ugali kisha akakifunga kwenye baiskeli na talaka mkononi kwenda ukweni.Kufika huko akakabidhi ugali mbichi kama ushahidi na talaka juu.Sasa ndio ninajiuliza ni halali kumwacha mkeo kisa hajui kupika?