Nguvu kubwa inayotumiwa na Polisi kuwadhibiti BAWACHA bila mafanikio ni kuipaisha taasisi hiyo

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,733
218,322
Ile Taasisi bora ya akina mama barani Africa, na ambayo inatajwa kushika namba 3 kwa ubora duniani kwa sasa, BAWACHA, Imeishika Nchi kwa kiganja kimoja cha mkono wa kushoto.

Pamoja na kwamba Bawacha ni Taasisi ya wanawake, lakini nguvu kubwa inayotumiwa na Jeshi la Polisi kuwadhibiti bila kufuata PGO, tena bila Mafanikio inazidi kuipaisha Taasisi hiyo

Hii_Marathon_Kati_ya_Jeshi_la_Polisi_na_Wanawake_wa_CHADEMA_nchi_nzima%2C_Nani_atashinda%3F._I...jpg

Kwa kifupi ni kwamba hoja za Polisi za kujaribu kuhusisha Jogging za Bawacha na harakati za kisiasa HAZINA MASHIKO, BAWACHA ni Taasisi ya kisiasa, chochote watakachokifanya hauwezi kukitenganisha na siasa, kiongozi wa kisiasa hawezi kubadilika kwa mavazi, hata akiingia Kanisani au Msikitini atabaki kuwa mwanasiasa tu, hata akihudhuria msiba bado TAITO yake ya uanasiasa haitapotea, udiwani wake, ubunge au uenyekiti wake hautaondoka kwa vile yuko kwenye mazishi.

Kwahiyo kuwazuia BAWACHA kufanya mazoezi kwa vile ni viongozi wa kisiasa, au labda kutaka wanasiasa hao wafanye mazoezi yao au Jogging zao huku vyeo vyao wameviacha nyumbani ni KITUKO kisichowezekana, Polisi ni lazima iseme ni namna gani kiongozi anaweza kujitokeza kama raia huku akiacha cheo chake nyumbani, na ni wakati gani ambao anapaswa kutembea na cheo chake, kwa mfano, ni wakati gani Waziri labda Jenister Mhagama anakuwa Waziri ni wakati upi anakuwa Raia? bila shaka si rahisi.

Bali Polisi wanapaswa kulinda amani na usalama tu, wakianza kupiga ramli na kuzuia wengine kukimbia barabarani kwa Visingizio vya kichovu watajidhalilisha tu, uonevu duni kama huu hautasaidia Polisi katika lolote na wala HAUTAFANIKIWA, zaidi utatengeneza Uhasama wa Kudumu.
 
Katika kikao cha bunge kijacho ipo haja baadhi ya vifungu vikarekebishwa kwa dharura hasa kipengele kinachoruhusu watu kuandamana hovyohovyo na vikao vya hovyo hovyo ili kuwepo na muda rasmi ambao ndio utakuwa muda sahihi kwa maswala ya kisiasa mfano [MWAKA MMOJA KABLA YA UCHAGUZI] ili mambo ya kisiasa yasiweze kuingiliana na mambo ya kiujenzi wa taifa
 
''Haki ya nani nasema kwa ukwe kwa ukweli mangi yangu wakikosea tu tunauchapa bei na mlima wenyewe tunawaachia vumbi tu chalii yangu unajua ule mlima ni pesa ndefuuu sana"
 
Katika kikao cha bunge kijacho ipo haja baadhi ya vifungu vikarekebishwa kwa dharura hasa kipengele kinachoruhusu watu kuandamana hovyohovyo na vikao vya hovyo hovyo ili kuwepo na muda rasmi ambao ndio utakuwa muda sahihi kwa maswala ya kisiasa mfano [MWAKA MMOJA KABLA YA UCHAGUZI] ili mambo ya kisiasa yasiweze kuingiliana na mambo ya kiujenzi wa taifa

..tatizo ccm wakiona upande wa upinzani kumenoga na kuna mwamko wana-panic na kuanza kutuma polisi kuwahujumu wapinzani.
 
Katika kikao cha bunge kijacho ipo haja baadhi ya vifungu vikarekebishwa kwa dharura hasa kipengele kinachoruhusu watu kuandamana hovyohovyo na vikao vya hovyo hovyo ili kuwepo na muda rasmi ambao ndio utakuwa muda sahihi kwa maswala ya kisiasa mfano [MWAKA MMOJA KABLA YA UCHAGUZI] ili mambo ya kisiasa yasiweze kuingiliana na mambo ya kiujenzi wa taifa
Point safi hii watu hawafanyi kazi kisa mbowe na lissu (anayejilia pork) tu huko ughaibuni

Cha kuongeza ni kuwa viongozi nao wabanwe zaidi katika kuleta maendeleo ya wananchi ili ionekane kweli kuwa kuna kitu kimefanyika wakati huo wa utulivu, hizi kelele za kijinga jinga kila dakika zinaboa nazo.

Hawajifunzi tu, wanahangaika mwenzao akitoka na kupata dili kama lile la 2015 (ambapo inasemekana bilioni kadhaa zilihusika), ANAPIGA!
 
Katika kikao cha bunge kijacho ipo haja baadhi ya vifungu vikarekebishwa kwa dharura hasa kipengele kinachoruhusu watu kuandamana hovyohovyo na vikao vya hovyo hovyo ili kuwepo na muda rasmi ambao ndio utakuwa muda sahihi kwa maswala ya kisiasa mfano [MWAKA MMOJA KABLA YA UCHAGUZI] ili mambo ya kisiasa yasiweze kuingiliana na mambo ya kiujenzi wa taifa
Point zako ni za hovyo sana, walioziweka hizo shuguli katika katia sio wajinga kama niyi mnaotafutiza tu kila sababu ya kuwazuia wapinzani wasifanue siasa! Wakati mnajaribu kumatamata sabab eti watu wasikusanyike sababu ya corona mbona matamasha makubwa kama Yanga Day na Simba Day hamkuzuia? Au mnafikiri wapinzani ni wajin ga ety?
 
point safi hii......watu hawafanyi kazi kisa mbowe na lissu (anayejilia pork) tu huko ughaibuni

cha kuongeza ni kuwa viongozi nao wabanwe zaidi katika kuleta maendeleo ya wananchi ili ionekane kweli kuwa kuna kitu kimefanyika wakati huo wa utulivu.......hizi kelele za kijinga jinga kila dakika zinaboa nazo.
hawajifunzi tu, wanahangaika mwenzao akitoka na kupata dili kama lile la 2015 (ambapo inasemekana bilioni kadhaa zilihusika), ANAPIGA!!!!
Hao watu hata wasipofanya kazi maisha yao wewe yankyhusu nini?

Huwalishi na wala hujuwi bajeti zao unahangaika nao kutaka wafanye kazi ya nani?

Acheni kujitoa ufahamu siku mtakapokuja kuwa wapinzani hayohayo ndiyo mtakayoyalilia tena kwa kusaga na meno!
 
Hao watu hata wasipofanya kazi maisha yao wewe yankyhusu nini?
Huwalishi na wala hujuwi bajeti zao unahangaika nao kutaka wafanye kazi ya nani?
Acheni kujitoa ufahamu siku mtakapokuja kuwa wapinzani hayohayo ndiyo mtakayoyalilia tena kwa kusaga na meno!
wanapozuia barabara kwa maandamano yao mama yangu anashindwa kuweka vitumbua vyake; watoto wetu wanaosoma kwenye mashule yaliyo karibu wanaathirika; bodaboda anashindwa kumpitisha mteja wake humo kisa mnamuandamania fulani n.k.

kama ingelikuwa yanawahusu nyie tu, kama lile la kupigwa bilioni kadhaa na mh. chair huku nyie mkideki barabara, hata nisingetia neno hata moja kwani hayanihusu kabisaaa. maisha yalivyonipiga hata sina muda wa kuyaingilia ya watu.
 
Point zako ni za hovyo sana, walioziweka hizo shuguli katika katia sio wajinga kama niyi mnaotafutiza tu kila sababu ya kuwazuia wapinzani wasifanue siasa! Wakati mnajaribu kumatamata sabab eti watu wasikusanyike sababu ya corona mbona matamasha makubwa kama Yanga Day na Simba Day hamkuzuia? Au mnafikiri wapinzani ni wajin ga ety?
Mgabo,haya mawazo ni ya muhumu sana kwani ungependelea nchi kila wakati iwe kwe siasa? KILA KITU NI LAZIMA KIWE NA WAKATI WAKE NDIO MAANA KUNA WAKATI WA CHAI LUNCH NA DINNER
 
Back
Top Bottom