Ngozi ya chatu ni zaidi ya uijuavyo

Hahaa nimekaa pembezoni mwa Hifadhi ya Serengeti, nimewinda sana, hakuna kitu kama hicho, mbwa huenda kushangaa Chatu.

Kwenye kushangaa ndo hukamatwa, Chatu akikulia timing hata wewe huchomoki kwake kamwe
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ya wezi imethibitishwa wapi? Au kwa story za Mshana?

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndiomaana umeona nimetilia shaka endapo ni kweli analegea na kukosa nguvu kwa harufu, je ngozi itatoa harufu kama ya chatu aliye hai?

Ila rangi ya ngozi ya chatu na chatu mzima hazina tofauti sana. Hii ya mbwa kushangaa rangi ya ngozi ya chatu kidogo inamantiki.
 
Kiukweli mbwa hanaga uhanja kwa chatu na hata mm nimeshapoteza mbwa wangu wawili porini nilipokuwa nachunga mifugo wa babu.
Ila pona pona yangu ilibidi mbwa aliwe tu mana kuna siku ilibakia kama mita kumi tu niingie kwenye 18 za chatu na mbwa aliwahi kujipeleka akanaswa na mbwa wengine wakashindwa kumsaidia mwenzao huku mimi natetemeka sijui hata cha kufanya.
Japo nilijifunza kitu kwamba chatu akimeza kitu hawezi tena mapambano wala huwa haendi mbali kutoka pale tukio limefanyika hivyo kama unaujasiri wa kupambana nae unamkata vipande vipande tu dk sifuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha hii nimeipenda, hao wanaojishugurisha na sayansi ya giza wangekuwa wabunifu kama huyu wa Njombe hakika tungekuwa na maendeleo makubwa sana.
 
Kwakweli bado natafiti hili... Mbwa hata awe hodari vipi akishaliona lile dubwana huchanganyikiwa kabisa na kukosa ujasiri huku akijipeleka kuliwa bila utashi wake
Kwahiyo analiwa kimasikhara.??
anyways,tuachane na hayo.
Swali!
Kama mbwa anafundwa na kufunzwa mbinu mbali mbali za ulinzi, how come mtaala wa mafunzo yake haujatilia maana mbinu za kukabiliana na chatu??
Au ndio ile hata iweje somo halitakaa lielewke??
Usinikumbushe enz zangu secondary,hata aje nguli yupi wa hesabu,akiandika ubaoni neno "!probability" basi akil zote zinapotea.Sielewi hata iwaje..

May b na mbwa hawa nao wamefikia hatua kama hiyo hapo.hawataelewa.vinginevyo wafunzwe
 
Kwakweli bado natafiti hili... Mbwa hata awe hodari vipi akishaliona lile dubwana huchanganyikiwa kabisa na kukosa ujasiri huku akijipeleka kuliwa bila utashi wake


Mkuu mshana kama utajaaliwa kugundua sababu, basi haitakuwa vyema kuweka ugunduzi wako hadharani kwani watu tupo tofauti, kuna wengine wanaweza kutumia ugunduzi huo kutengeneza dawa za kuwanasa wake za watu.
 
Atleast hapa naweza kukubali
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kabisa mkuu. Nimeshudia kabisa. Sisi kwetu zamani kulikuwa na nyoka hatari. Siku tuko shule,kulikuwa na poli kubwa la shule,tumeshuhudia hayo makitu,nyoka akijivua gamba ndio unasikia harufu ya wali
Umeshuhudia nyoka akijivua magamba ama umesikia harufu ya wali...tuweke sawa hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…