Ngozi ya chatu ni zaidi ya uijuavyo

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,789
Good morning great thinkers, N sinkers.
Good morning JF. Good morning people!

Matukio ya kuvujiwa nyumba na kuibiwa hali ya kuwa tumeajiri walinzi wa asili na hata wa kisasa huku wengine wakiwa na silaha kali za moto kumesababisha wengine kutokuwa na imani nao tena.

Kufuatia hali hiyo ndio maana wenye uwezo kifedha wameamua kuongeza nguvu na mbwa wenye mafunzo. Na kwa wale wenye kipato cha kawaida wameamua kufuga mbwa kama walinzi waaminifu.

Lakini inakuwaje hata hawa walinzi waaminifu nao wanazidiwa maarifa na kujikuta nao wanalevywa ama kuibiwa kabisa? Kuna kutumia ujanja wa chakula chenye sumu ama madawa ya kulevya.

Lakini mbwa mwenye mafunzo hadanganyiki kamwe. HALI!!!

Akili ya binadamu hailali kila kitu kina mbadala wake. Wewe ukiwaza hivi. Kuna mwenzako anawaza vile. Kama mbwa wako ana mafunzo ya kutokula chochote bila idhini yako. Wenzako wamewaza zaidi ya hapo

Kuna sayansi ya nguvu ya uvutano kati ya mbwa na chatu. Mbwa akishakutana na chatu huishiwa na nguvu na kujikuta anajipeleka mwenyewe bila kupenda mpaka analiwa. Umegundua nini hapo? Kiboko ya mbwa ni chatu.

Hivyo basi siku hizi wezi wanatembea na ngozi za chatu kwenye yale majumba yenye mbwa wakali. Wakifanikiwa tu kuzama ndani na kumwoneshea mbwa wako mwenye mafunzo yote. Hupoteza nguvu zote na kujikuta anaifuata ngozi huku akitoa mate mdomoni na kutikisa tu mkia na kutoa kisauti chenye kutia huruma.

Hapo mwizi atakuwa na uchaguzi. Amuibe na mlinzi mwaminifu? Amuue? Amzimishe kwa muda? Ukiona watu wako busy mikoani kutafuta ngozi za chatu tambua zina matumizi zaidi ujuavyo

hqdefault-1.jpeg
hqdefault.jpeg
 
Kwakweli bado natafiti hili... Mbwa hata awe hodari vipi akishaliona lile dubwana huchanganyikiwa kabisa na kukosa ujasiri huku akijipeleka kuliwa bila utashi wake
Mshana Jr kwenye ubora wake,

Nini hasa kinachomponza mlinzi huyu mwaminifu kwa Chatu? Ebu tujazie jazie nyama hapo mkuu, hasa pale uliposema nguvu ya uvutano kati yao.
 
Kule kijijini mkiwa porini na mbwa ile hali ya kuhisi tu kuwa kuna joka kubwa karibu, kama mlikuwa mnatembea huku mnacheza, hachezi tena zaidi ya kulia, kufyata mkia na kuelekea aliko. Anakuwa hawezi kutii sheria tena bila shuruti. Unachofanya ni kutumia nguvu kwa kipigo au kumkamata kwa nguvu ili mbadili uelekeo.
Uzoefu wangu kutoka maeneo yenye historia ya kunukia wali porini kunakosababishwa na uwepo wa nyoka wakubwa.
 
Kule kijijini mkiwa porini na mbwa ile hali ya kuhisi tu kuwa kuna joka kubwa karibu, kama mlikuwa mnatembea huku mnacheza, hachezi tena zaidi ya kulia, kufyata mkia na kuelekea aliko. Anakuwa hawezi kutii sheria tena bila shuruti. Unachofanya ni kutumia nguvu kwa kipigo au kumkamata kwa nguvu ili mbadili uelekeo.
Uzoefu wangu kutoka maeneo yenye historia ya kunukia wali porini kunakosababishwa na uwepo wa nyoka wakubwa.
Nataka nifanye utafiti naweza kupata dawa bora sana ya mvuto hasa kwa madomo zege na akina dada wanaosaka ndoa... Shida ni kwamba inaweza kuwa zana bora kabisa kwa matapeli na machangu
 
Good morning great thinkers, N sinkers.
Good morning JF. Good morning people!!

Matukio ya kuvujiwa nyumba na kuibiwa hali ya kuwa tumeajiri walinzi wa asili na hata wa kisasa huku wengine wakiwa na silaha kali za moto kumesababisha wengine kutokuwa na imani nao tena.

Kufuatia hali hiyo ndio maana wenye uwezo kifedha wameamua kuongeza nguvu na mbwa wenye mafunzo. Na kwa wale wenye kipato cha kawaida wameamua kufuga mbwa kama walinzi waaminifu.

Lakini inakuwaje hata hawa walinzi waaminifu nao wanazidiwa maarifa na kujikuta nao wanalevywa ama kuibiwa kabisa? Kuna kutumia ujanja wa chakula chenye sumu ama madawa ya kulevya.

Lakini mbwa mwenye mafunzo hadanganyiki kamwe. HALI!!!

Akili ya binadamu hailali kila kitu kina mbadala wake. Wewe ukiwaza hivi. Kuna mwenzako anawaza vile. Kama mbwa wako ana mafunzo ya kutokula chochote bila idhini yako. Wenzako wamewaza zaidi ya hapo

Kuna sayansi ya nguvu ya uvutano kati ya mbwa na chatu. Mbwa akishakutana na chatu huishiwa na nguvu na kujikuta anajipeleka mwenyewe bila kupenda mpaka analiwa. Umegundua nini hapo? Kiboko ya mbwa ni chatu.

Hivyo basi siku hizi wezi wanatembea na ngozi za chatu kwenye yale majumba yenye mbwa wakali. Wakifanikiwa tu kuzama ndani na kumwoneshea mbwa wako mwenye mafunzo yote. Hupoteza nguvu zote na kujikuta anaifuata ngozi huku akitoa mate mdomoni na kutikisa tu mkia na kutoa kisauti chenye kutia huruma.

Hapo mwizi atakuwa na uchaguzi. Amuibe na mlinzi mwaminifu? Amuue? Amzimishe kwa muda? Ukiona watu wako busy mikoani kutafuta ngozi za chatu tambua zina matumizi zaidi ujuavyo

View attachment 1284247View attachment 1284248


Haina ukweli wowote, mbwa akiona nyoka wa aina yeyote hata mjusi lazima atamfuata na kumnusa ili ajuwe kama ni chakula au la.
 
Kule kijijini mkiwa porini na mbwa ile hali ya kuhisi tu kuwa kuna joka kubwa karibu, kama mlikuwa mnatembea huku mnacheza, hachezi tena zaidi ya kulia, kufyata mkia na kuelekea aliko. Anakuwa hawezi kutii sheria tena bila shuruti. Unachofanya ni kutumia nguvu kwa kipigo au kumkamata kwa nguvu ili mbadili uelekeo.
Uzoefu wangu kutoka maeneo yenye historia ya kunukia wali porini kunakosababishwa na uwepo wa nyoka wakubwa.
Ukisikia kunukia wali ujue ni nyoka anajitoa magamba
 
Sidhani kama ni rangi tu... Kuna kitu cha ziada kinachohusika na hormones harufu na wireless poison yenye kulevya....!!!

Nahapo ndio hoja ya rangi inapokua na nguvu sasa. Ngozi ya chatu haiwezi kuwa na harufu, au kutoa vitu kama chatu akiwa hai.
Ila hao wezi waliobuni hii sayansi inabidi watunukiwe PhD nne.

Sambamba na waliojiongeza kwenye mafuta ya transformer kutokuisha upesi kwenye chips, akili kubwa sana imetumika pale.
 
Kuna jamaa alikuwa anapasulisha mbao miaka ya 2004 kule mkoa wa njombe, ilikuwa ukienda kuiba mbao zake usiku unavurugwa, badala ya kupeleka ulikodhamiria kupeleka kama ni kwa mteja au kwako, unajikuta umepeleka nyumbani kwake.
Ukifika pale kwake unamkuta anakusubiria, anakuonesha sehemu ya kuweka na kukushukuru sana. Baada ya hapo ndio unapata akili na kuondoka kwa aibu.
Nahisi dawa ilitokana na huyu mdudu.
 
Hiyo ya kunukia wali porini nilishawahi kuishuhudia ndani ya msitu mzito
Kule kijijini mkiwa porini na mbwa ile hali ya kuhisi tu kuwa kuna joka kubwa karibu, kama mlikuwa mnatembea huku mnacheza, hachezi tena zaidi ya kulia, kufyata mkia na kuelekea aliko. Anakuwa hawezi kutii sheria tena bila shuruti. Unachofanya ni kutumia nguvu kwa kipigo au kumkamata kwa nguvu ili mbadili uelekeo.
Uzoefu wangu kutoka maeneo yenye historia ya kunukia wali porini kunakosababishwa na uwepo wa nyoka wakubwa.
 
Back
Top Bottom