New KASI Internet from Vodacom Plc

New KASI Internet from Vodacom Plc

Bei sasa ndio tatizo hapo...huchelewi kuambiwa laki kwa mwezi
mi hawa watu na Tigo nilishawashindwa.....najuta kujisajili nao zaidi ya miaka nane iliyopita.....sasa sijui niende wapi hasa kwa ajili ya Data...kwa voice nimeambiwa Airtel wako vizuri .....ndiyo kwanza nimeanza nao
 
Bongo huwa hakuna kitu kinaitwa kasi internet, fast internet, super fast internet na vyote vinavyofanana na hayo majina kwa mitandao inayotumia minara ya simu...

Such internet speed inawezekana tu kwa huduma za FTTx na sio hizi mambo zenu za wifi broadband/LTE etc...

Huwa mnakula tu hela za waTz kwa kuweka majina mazuri mazuri lakini hakuna lolote...
Mkuu hii FTTx naomba maelezo kidogo kama hutojali.
 
Mkuu hii FTTx naomba maelezo kidogo kama hutojali.
Fiber To The X (FTTx)...X inaweza ikawa office, nyumbani or eslewhere...

Yaani huduma ya internet inakufikia nyumbani kwa mfumo wa fiber cable...

Kwa nchi zilizoendelea, aina hii ya FTTx hubeba si internet tu bali hata Video contents like cable tv services etc...

Kwa bongo sina uhakika kampuni gani inafanya hivi maybe jamaa wa Raha.com...
 
Fiber To The X (FTTx)...X inaweza ikawa office, nyumbani or eslewhere...

Yaani huduma ya internet inakufikia nyumbani kwa mfumo wa fiber cable...

Kwa nchi zilizoendelea, aina hii ya FTTx hubeba si internet tu bali hata Video contents like cable tv services etc...

Kwa bongo sina uhakika kampuni gani inafanya hivi maybe jamaa wa Raha.com...
Yes....Raha chini ya Liquid Telecom wanafanya hizo huduma.
 
.sasa sijui niende wapi hasa kwa ajili ya Data.
TTCL
- 5GB kwa TZS 5,000 Kwa mwezi mmoja
- Unajiunga mara nyingi kadri umalizapo hizo 5GB.

Jinsi ya kupata hizo 5GB
1. Piga *150*71#
2. Chagua 3
3. Chagua 2
4. Chagua 2 (Tena)
5. Chagua 3
 
Nina siku chache zimebaki ili niuhame Mtandao wenu. Yaani kidogo tu eti kifurushi cha Internet kimeisha. Wakati mwingine siingii YOUTUBE wala ku-download video yoyote lakini kifurushi cha Internet kinakuwa kimekata.

Hii haikubaliki kabisa.!
 
Naona wameamua kuja kujaza tu server za Jf. Maana hata wazo la kujibu hoja za wakuu hapa ndani hawataki. Janga hili
 
Bongo huwa hakuna kitu kinaitwa kasi internet, fast internet, super fast internet na vyote vinavyofanana na hayo majina kwa mitandao inayotumia minara ya simu...

Such internet speed inawezekana tu kwa huduma za FTTx na sio hizi mambo zenu za wifi broadband/LTE etc...

Huwa mnakula tu hela za waTz kwa kuweka majina mazuri mazuri lakini hakuna lolote...
Labda standard yako wewe ya fast internet ni ipi? Maana Hao voda wanavuka average speed ya dunia kwa speed.
 
Back
Top Bottom