NGOSWE2
JF-Expert Member
- Dec 19, 2013
- 635
- 547
Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.
Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu.*Naye akanena, Enenda tena mara saba.
Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie...(1Wafal 18:42b-45).
SOMO KUU: MAOMBI YENYE NGUVU.
Pointi ya Kwanza: Sababu za kuombea.
Biblia inatoa sababu za wazi kabisa Kwa nini watu wa Mungu wanapaswa kuomba:
(1). Ya kwanza na ya muhimu zaidi, waumini wameagizwa na Mungu kuomba. Agizo la kuomba linotoka kwenye midomo ya mtunga Zaburi (Zab 105:4; 1 Nyak 16:11), manabii (Isa 55:6; Amo 5:4,6), mitume (Efe 6:17-18; Kol 4:2; 1Thes 5:17), na Bwana Yesu mwenyewe ( Math 26:41; Lk 18:1; Yoh 16:24). Mungu anapenda sana ushirika wetu; Kwa njia ya maombi tunadumisha uhusiano wetu pamoja naye.
Mpendwa wangu katika Bwana,
Neno la Mungu linatuagiza na kusema :*"mtakeni Bwana na nguvu zake"*inamaansha tunaalikwa sio tu kuutafuta uwepo wa Mungu bali pia uwezo na nguvu za neema yake Kwa sababu zifuatazo:
(a). Sisi sote tunahitaji nguvu za Ki-Mungu ili kudumu katika wokovu, kuishi maisha yanayomoendeza Mungu, na kushuhudia katika uwezo wa Roho Mtakatifu (Mdo 1:8; 2:4)
(b). Ni lazima Kila siku tumwangalie Mungu na neema yake, la sivyo tutashikwa na udhaifu wa kiroho na kushindwa, hivyo basi, ni lazima tuchochee wenyewe siku zote kumtafuta Kwa bidii Kwa moyo wote ( Math 7:7-8) na tutarajie ishara za uwepo wake na nguvu katika maisha yetu ( 2Nya 26:5; Kumbu 4:29).
N.B: KUMBUKA MWAKA HUU 2024 NI MWAKA WA KUZAMA KWENYE KILINDI CHA MAOMBI ILI UTOBOE
Nakutakia Siku njema, nakuombea neema ya maombi iwe juu yako Mwaka huu wa 2024.
Akamwambia mtumishi wake, Kwea sasa, utazame upande wa bahari. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu.*Naye akanena, Enenda tena mara saba.
Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika, ushuke, mvua isikuzuie...(1Wafal 18:42b-45).
SOMO KUU: MAOMBI YENYE NGUVU.
Pointi ya Kwanza: Sababu za kuombea.
Biblia inatoa sababu za wazi kabisa Kwa nini watu wa Mungu wanapaswa kuomba:
(1). Ya kwanza na ya muhimu zaidi, waumini wameagizwa na Mungu kuomba. Agizo la kuomba linotoka kwenye midomo ya mtunga Zaburi (Zab 105:4; 1 Nyak 16:11), manabii (Isa 55:6; Amo 5:4,6), mitume (Efe 6:17-18; Kol 4:2; 1Thes 5:17), na Bwana Yesu mwenyewe ( Math 26:41; Lk 18:1; Yoh 16:24). Mungu anapenda sana ushirika wetu; Kwa njia ya maombi tunadumisha uhusiano wetu pamoja naye.
Mpendwa wangu katika Bwana,
Neno la Mungu linatuagiza na kusema :*"mtakeni Bwana na nguvu zake"*inamaansha tunaalikwa sio tu kuutafuta uwepo wa Mungu bali pia uwezo na nguvu za neema yake Kwa sababu zifuatazo:
(a). Sisi sote tunahitaji nguvu za Ki-Mungu ili kudumu katika wokovu, kuishi maisha yanayomoendeza Mungu, na kushuhudia katika uwezo wa Roho Mtakatifu (Mdo 1:8; 2:4)
(b). Ni lazima Kila siku tumwangalie Mungu na neema yake, la sivyo tutashikwa na udhaifu wa kiroho na kushindwa, hivyo basi, ni lazima tuchochee wenyewe siku zote kumtafuta Kwa bidii Kwa moyo wote ( Math 7:7-8) na tutarajie ishara za uwepo wake na nguvu katika maisha yetu ( 2Nya 26:5; Kumbu 4:29).
N.B: KUMBUKA MWAKA HUU 2024 NI MWAKA WA KUZAMA KWENYE KILINDI CHA MAOMBI ILI UTOBOE
Nakutakia Siku njema, nakuombea neema ya maombi iwe juu yako Mwaka huu wa 2024.