Gaga
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 4,558
- 1,968
Hi wana Jf MMU, tunaongea habari nyingi sana, mikasa ya mapenzi,ugomvi na kadhalika.Nimeona sio mbaya pia niwakumbushe wote leo ni jpili si vibaya tukakumbushana Kusali, kutoa kwa maskini, na kupendana , kujaliana na kusameheana jumapili ya leo. nimeamua kushare na nyie hili cause leo tumefundishwa na tumeambiwa tuwaambie na wenzetu misingi ya maneno hayo hapo juu.
Katika hayo yote mie nimeamua niongelee kutoa kwa maskini na wasiojiweza, watu wengi tunasahau kwamba maisha haya tunayoishi leo inaweza kuwa kwa yule kesho kwetu. hivo basi tujifunze kutoa kusaidia kadri tuwezavyo, kwani kutoa sio utajiri au kwamba unacho sana.Tusiwasahau wazazi wetu kwani bila wao leo hii tusingekuwepo. Inasikitisha kuona mtu anaweza kutumia pesa hovyo bila mpangilio ila linapokuja kutoa msaada kwa wazazi tunajisahau sana.Tuwapende wazazi wetu na kuwaonyesha kwamba bila wao sisi si kitu.Mzazi ni Mungu wa pili wa kila binadamu.
Nawapenda nyote Jumapili jema
Katika hayo yote mie nimeamua niongelee kutoa kwa maskini na wasiojiweza, watu wengi tunasahau kwamba maisha haya tunayoishi leo inaweza kuwa kwa yule kesho kwetu. hivo basi tujifunze kutoa kusaidia kadri tuwezavyo, kwani kutoa sio utajiri au kwamba unacho sana.Tusiwasahau wazazi wetu kwani bila wao leo hii tusingekuwepo. Inasikitisha kuona mtu anaweza kutumia pesa hovyo bila mpangilio ila linapokuja kutoa msaada kwa wazazi tunajisahau sana.Tuwapende wazazi wetu na kuwaonyesha kwamba bila wao sisi si kitu.Mzazi ni Mungu wa pili wa kila binadamu.
Nawapenda nyote Jumapili jema