Neno 'dear'

Umesema vema. Neno la kiingereza 'dear' lina 'utata' (i.e. lina maana zaidi ya moja!). Kwenye kiingereza neno 'dear' linaweza kutumika kama kivumishi (adjective), interjection, jina(noun) au adverb (kielezo).

Kama alivyodadavua Creative Thinker hapo juu, neno 'dear':

Likitumika kama kivumishi (adjective), linaweza kuwa na maana zifuatazo:

  • ‘mbaya’ (i.e. severe, sore – mfano: “.. in our dear peril”)
  • ‘enye thamani’ (highly valued – Mfano “dear friend”) – kwenye barua za kiofisi nadhani linabeba maana hii.
  • ‘enye kupendwa’ (affectionate, fond)
  • ‘aghali’ (expensive – mfano: mangoes are very dear just now)
Pia linatumika kama kielezo (‘adverb’) kumaanisha ‘sana’ au ‘kiasi kikubwa’ (mfano: “The effort would cost them dear”).

Linatumika kama jina (noun), linaweza kuwa na maana ya: Mwenye kupendwa/mpenzi (a loved one – sweetheart!) au Mtu anaependeka (a lovable person).

Pia, neno dear linatumika kuonesha kukerwa, kushangazwa nk (interjections or exclamations) – mfano: “Oh, dear! Does it hurt?”, “Dear me! That’s a surprise!”


Mkuu hapa tuko pamoja. Ambaye hatataka kuelewa kutokana na maelezo yako, shauri yake!!!!

Tiba
 
hili neno la kingereza lina utata katika matumizi. maana yake hasa ni nini? kwenye barua utakuta Dear sir/madam. tunaambiwa dear ni mpenzi, so tuseme mpenzi kwenye barua rasmi? maana yake hasa ni ipi? naombeni jibu

teh teh

Dear Sir / Madam
Mpendwa ....../......

ila siku hizi watu tumeipotosha ime kuwa ni D sasa hapo yakanganya kidogo ni D=Dear au D= Darling ?? hata kwa sms utakuta Dia????? what does it mean????

Na je wale waliko maofficen uta sikia jamani Swetiii honeiiiii haichagui kama ni SHE au HE mara kampiga na file kwa makalio na vicheko vingi sasa ni utani au?? mtu akiniambi kuna utani basi amwite shoti au shostito huo ndio utani

Thankx to my Dia

 
hili neno la kingereza lina utata katika matumizi. maana yake hasa ni nini? kwenye barua utakuta Drea sir/madam. tunaambiwa dear ni mpenzi, so tuseme mpenzi kwenye barua rasmi? maana yake hasa ni ipi? naombeni jibu


1.Tusichanganye maneno ya mitaani katika mawasiliano rasmi.

2."Dear" ina maana nyingi na siyo lazima iwe "mpenzi"..Neno "Dear" lina maana kadhaa kwa kiswahili ukiachilia mbali hiyo "mpenzi" ambayo kiingereza sahihi ni "darling".Hebu tutafsirie mpenzi wangu kwa kiingereza - ina maana utasema "my dear" au utasema "my darling"?

3.Nionavyo mimi katika lugha rasmi neno "Dear" Linamaanisha "mpendwa" au "kitu cha thamani".The opposite of "dear" is "cheap"
 
1.Tusichanganye maneno ya mitaani katika mawasiliano rasmi.

2."Dear" ina maana nyingi na siyo lazima iwe "mpenzi"..Neno "Dear" lina maana kadhaa kwa kiswahili ukiachilia mbali hiyo "mpenzi" ambayo kiingereza sahihi ni "darling".Hebu tutafsirie mpenzi wangu kwa kiingereza - ina maana utasema "my dear" au utasema "my darling"?

3.Nionavyo mimi katika lugha rasmi neno "Dear" Linamaanisha "mpendwa" au "kitu cha thamani".The opposite of "dear" is "cheap"

thanks for ur kind concern my dear
 
mshakaji kuna baadhi ya maneno huwezi kupata maana halisi hususan unapo litafsiri toka lugha moja kwenda nyingine, Dear ni neno la heshima na si la mapenzi thats why hata kwenye barua muhimu kama za kikazi una andika Dear sir/madam.

nakubaliana nawe....

pengine maana ya karibu ingawa sina hakika kama ni tafsiri sahihi ni

Mpendwa Ally Mkali....salaamu sana na amma baada ya salamu....hii ni kwa mujibu wa namna ya kuandika barua kama tulivyofundishwa enzi za mwalimu.

kuna tofauti kubwa baina nya mpenzi na mpendwa na pengine huu ni mjadala mwingine
 
nakubaliana nawe....

pengine maana ya karibu ingawa sina hakika kama ni tafsiri sahihi ni

Mpendwa Ally Mkali....salaamu sana na amma baada ya salamu....hii ni kwa mujibu wa namna ya kuandika barua kama tulivyofundishwa enzi za mwalimu.

kuna tofauti kubwa baina nya mpenzi na mpendwa na pengine huu ni mjadala mwingine

mpendwa katika Bwana. hii wanayo walokole
 
hili neno la kingereza lina utata katika matumizi. maana yake hasa ni nini? kwenye barua utakuta Drea sir/madam. tunaambiwa dear ni mpenzi, so tuseme mpenzi kwenye barua rasmi? maana yake hasa ni ipi? naombeni jibu

You use dear to describe someone or something that you feel affection for.

You use dear in expressions such as `my dear fellow', `dear girl', or `my dear Richard' when you are addressing someone whom you know and are fond of. You can also use expressions like this in a rude way to indicate that you think you are superior to the person you are addressing.

Dear is written at the beginning of a letter, followed by the name or title of the person you are writing to.

If you say that something is dear, you mean that it costs a lot of money, usually more than you can afford or more than you think it should cost.

If something that someone does costs them dear, they suffer a lot as a result of it.

In British English, you begin formal letters with `Dear Sir' or `Dear Madam'. In American English, you begin them with `Sir' or `Madam'.

Have fun!
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya DEAR na DARLING, tatizo tulilonalo Wabongo ni kupenda mno lugha za watu tusizo zijua vizuri. Wemgi wetu tunatumia dear mahala pa darling matokeo yake ni vurugu tupu. Hasa uswazi ambako elimu yake mara nyingi ni std saba.

Suluhisho ni kutumia lugha yetu TUKUFU NA ADHIMU.
 
hili neno la kingereza lina utata katika matumizi. maana yake hasa ni nini? kwenye barua utakuta Drea sir/madam. tunaambiwa dear ni mpenzi, so tuseme mpenzi kwenye barua rasmi? maana yake hasa ni ipi? naombeni jibu
Umenikumbusha, jamaa yangu mmoja, siku za mwanzo alikuwa anapata tabu sana, haswa anapokuwa anampisha mtu mzima kiti (Vibibi vya kizungu) kwenye basi au train... Alikuwa ananilalamikia kwa kusikia akiambiwa Thanks you my love... au wakati mwingine Thanks you honey...

Ki uhakika hao waliokuwa wakipishwa sit za kwenye bus au train hawakuwa na fikra hizo ambazo jamaa yangu alikuwa anazifikiria. Wahusika walikuwa wanaonyesha shukrani zao kwa heshima na kujali kwa jamaa yangu... sasa ndugu ikawa inamchanganya kidogo... baadae alikuja zoea misemo ya namna hiyo...!

Msemo mmoja unaweza kuwa na maana tofauti kulingana na wakati au mtu unaye mkusudia... Nadhani walio tangulia wameeleza vizuri sana matumizi ya ilo neno 'Dear.'
 
Umenikumbusha, jamaa yangu mmoja, siku za mwanzo alikuwa anapata tabu sana, haswa anapokuwa anampisha mtu mzima kiti (Vibibi vya kizungu) kwenye basi au train... Alikuwa ananilalamikia kwa kusikia akiambiwa Thanks you my love... au wakati mwingine Thanks you honey...

Ki uhakika hao waliokuwa wakipishwa sit za kwenye bus au train hawakuwa na fikra hizo ambazo jamaa yangu alikuwa anazifikiria. Wahusika walikuwa wanaonyesha shukrani zao kwa heshima na kujali kwa jamaa yangu... sasa ndugu ikawa inamchanganya kidogo... baadae alikuja zoea misemo ya namna hiyo...!

Msemo mmoja unaweza kuwa na maana tofauti kulingana na wakati au mtu unaye mkusudia... Nadhani walio tangulia wameeleza vizuri sana matumizi ya ilo neno 'Dear.'

hakujichanganya na kuviomba? maana wabongo hatuchelewi. umenikumbusha tena na neno 'honey' kwa kiswahili halitamkiki unapoongea na mtu. eti asali!
 
hakujichanganya na kuviomba? maana wabongo hatuchelewi. umenikumbusha tena na neno 'honey' kwa kiswahili halitamkiki unapoongea na mtu. eti asali!
Ah ah ah ah...! Hakuwahi kujaribu maana naye alikuwa ndio kwanza ana wiki chache kuwepo ndani ya nchi, na baadhi ya misemo ilikuwa inampiga chenga.

Unajuwa hizi lugha kila jamii ina misemo yake, misemo ambayo ukitaka kuitafsiri moja kwa moja utaleta maana tofauti kabisa. Mara nyingine Kwa mfano neno Head of state... Tafsiri yake inaweza kuwa Mkuu wa nchi. Lakini ukileta tafsiri ya neno kwa neno utapata maana tofauti kabisa. Vile vile baadhi ya misemo... kama vile hit the road na mingineyo.

Neno Honey, nasi waswahili tunalitumia kwa njia nyingine, mfano "Huyu ndiye Asali ya moyo wangu" kiufupi tunaongeza maneno mbele yake.
 
1.Tusichanganye maneno ya mitaani katika mawasiliano rasmi.

2."Dear" ina maana nyingi na siyo lazima iwe "mpenzi"..Neno "Dear" lina maana kadhaa kwa kiswahili ukiachilia mbali hiyo "mpenzi" ambayo kiingereza sahihi ni "darling".Hebu tutafsirie mpenzi wangu kwa kiingereza - ina maana utasema "my dear" au utasema "my darling"?

3.Nionavyo mimi katika lugha rasmi neno "Dear" Linamaanisha "mpendwa" au "kitu cha thamani".The opposite of "dear" is "cheap"

Dear VC, umenikuna sana kwa hili!! You are so dear to the JF
 
ndio maana nataka kujua maana yake kwa kiswahili. badala ya dear ungetumia neno gani?

Mzee pole kwa kutoka jasho kutafuta mbadala wa hilo neno katika lugha ya bongo. Lakini pia nikupongeze kwani unaonekana kuwa na tabia ya kujishughulisha na kuyatafutia ufumbuzi mambo ambayo wengine hukubali kuwa yanatakiwa kubaki kama yalivyo.

Jambo unalopaswa kukumbuka ni kuwa mara nyingi lugha huenda sambamba na utamaduni wa jamii inayohusika. Nina maana kuwa jaribio la kutafsiri neno fulani kwenda lugha ingine linaweza kuwa rahisi au gumu kama jaribio la kutafsiri utamaduni wa jamii moja kwenda jamii ingine.

Kabla hatujaenda mbali nakupa zoezi la maswali mawili, ukimaliza kujibu tutaendelea na mada yetu:

1. Tafsiri utamaduni wa Kibongo wa 'nyumba ndogo' kwenda katika utamaduni wa Kimarekani.

2. Tafsiri neno 'Mwembechai' kwenda katika lugha ya Kiingereza
 
shockstoper:
it is simply concubine pamoja na mwembechai. hapo limetumika kama nomino ya sehemu. kiswahili cha darasani kimenitoka kidogo. tatizo jingine ni kuwa hasa wanawake wanatumia neno mpenzi katika maongezi. utasikia "unasemaje mpenzi". hilo nalo tatizo
 
hata hivyo tukianza kuchambua matumizi ya maneno tutakuwa tunajikosoa sana kimatamshi na maongezi. tumezoea neno dear = mpenzi, kumbe sio. wakati huo huo neno mpenzi linatumika sana katika maongezi ya kawaida kama nilivyosema hapo juu. kwa mfano tukisema mtu anayepanda mbegu ni mpanzi. mpanzi ndiye mtenda. na mtu anayependa ni mpenzi. sasa mimi nitamuitaje mtu mwingine mpenzi? si sawa na kuisemea nafsi ya mtu? nitajuaje kama anapenda kama ilivyo kwa mpanzi ambaye tunaona akipanda? mwisho wa siku tunarudi pale pale kuwa mtu anayependwa ni mpendwa si mpenzi. mpenzi ni yule anayependa. kwa maana hiyo, dear = mpendwa. darling pia ni mpendwa na si mpenzi. hebu tushauriane zaidi katika hayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom