NEMC yasema imewafungulia waliofungiwa kwa kupiga kelele lakini yatoa onyo kwa waliojisahau

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
b66a2555-7f0c-468c-b8e2-9cda2f19ceb5.jpeg

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt Samuel Gwamak

Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt Samuel Gwamaka awataka wamiliki wote wa baa na kumbi za burudani kuzingatia Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni zake wakati wakiendesha shughuli zao za burudani ili kuepusha bugudha kubwa kwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.


Amelitoa agizo hilo leo Septemba 12, 2023 katika Ukumbi wa mikutano wa NEMC alipokutana na vyombo vya habari kuzungumzia hali iliyopo kwa sasa katika jamii kufuatia kukithiri kwa sauti zilizozidi viwango na kusababisha athari kubwa.

Amesema kuna ongezeko la malalamiko ya uchafuzi wa mazingira kwa njia ya kelele ndani ya wiki mbili zilizopita.

Amebainisha kuwa baada ya kutoa adhabu ya faini na kuwafungia baadhi ya wahusika ikiwemo kumbi za starehe, baadaye wakafunguliwa, ndipo wahusika wameanza kujisahau na kuanza kupiga kelele.

Ametosema “Baraza tunawakumbusha Sheria bado ipo na inafanya kazi, kelele ni kero hasa zinapowagusa wasiohusika.

“Kuna watu wanaumwa na wanahitaji utulivu hasa wakati wa usiku, hivyo unapofanya sherehe au tukio kumbuka kuna raia wengine wanahitaji muda wa kupumzika na wanastahili haki hiyo.

“Naomba kutoa tahadhari kwa wote wanaoendesha vyombo vya starehe, si vema tukarudi tulipotoka, zoezi lile lilikwisha na elimu ilishatolewa."
 
Wananchi wahamie maporini watuachie walevi baa zetu, mkidikiliza sana wananchi ipo siku utadikia wanasema magari yasipite barabarani yanapiga kelele...
 
Sawa....
Kwahiyo wamefunguliwa baada ya kupewa adhabu/faini??
Je wamefunguliwa baada ya kusamehewa??
Je wamefunguliwa kwa maelekezo kutoka juu??
Je wamefunguliwa baada ya kuwapatia chochote hao kamati/bodi??
Yaani wamedunguliwa kwa vigezo gani??
 
Hii nchi siasa majitaka ndio zinaendesha,ila sheria na kanuni zimewekwa mfukoni.
 
Back
Top Bottom