Ndugulile aitaka Serikali kuondoa Tozo za Daraja la Nyerere (Kigamboni)

PendoLyimo

JF-Expert Member
Sep 30, 2014
879
956
1645090645156.png

Wakuu hi tozo ikiondolewa wakazi wa Kigamboni itawapunguzia Sana Ukali wa Maisha.

Mbunge wa Kigamboni Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) ameitaka Serikali kuondoa tozo za Daraja la Nyerere lililopo Kigamboni na badala yake Serikali ibebe mzigo wa deni la mkopo wa NSSF.

Ndugulile ameyasema haya leo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa anachangia taarifa ya Kamati ya Bajeti.

Ndugulile alieleza kwamba ni wakazi wa Kigamboni pekee nchini kote ambao wanalipia gharama ya daraja wakati kuna madaraja mengi yamejengwa kwa fedha za mikopo.

Dkt. Ndugulile alisema kuwa wakazi wa Kigamboni hawana njia mbadala ya kutumia kama ambavyo wakazi wa Msasani, Masaki na wengine wanaotumia Daraja la Tanzanite, hivyo kuwatoza fedha ni kutowatendea haki wakazi wa Kigamboni.

Wakazi wa Kigamboni wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu tozo za Daraja la Nyerere, hali inayopelekea kuongeza kwa gharama za maisha.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Nchi hii ina madaraja mengi Sana, na mengine bado yanajengwa. Kwanini daraja la kigamboni tuu ndo wananchi wapite kwa kulipia wakati madaraja mengine yoote ni barabara tuu tunalipa kwenye road licence? Kwanini kuwe na malipo yaziada kwenye hili daraja moja tu?
 
Nipo hapa najiwazia tuu, itafurahisha sana kama tozo za daraja la Kigamboni zitafutwa ili kuwapa unafuu wa makali ya maisha wakazi na watembeleaji wa Kigamboni.
 
Back
Top Bottom