A
Anonymous
Guest
Nimeshuhudia hilo jambo likifanyika mara nyingi tu kwa kuwa hiyo ni njia yangu.
Kinachotokea majira ya asubuhi ambapo kuna msongamano wa magari mengi hawafanyi huo mchezo, nilichobaini ni kuwa wanakuwa na hofu ya kwamba wakifanya hayo watabainika kwa sababu wanaopita mida hiyo ni watu wengi na wanaweza kuwemo wenye mamlaka, hivyo ikawa kwao.
Mara nyingi, majira ya mchana walinzi wa kwenye kizuizi hicho wanafanya majukumu yao kama kawaida kisha wakiona pametulia yaani hakuna purukushani nyingi za mpishano wa vyombo vya moto, wale wanaopokea hela na kutoa risiti wanajifanya kuingia ndani kwenye ofisi zao, wanabaki walinzi kadhaa kwa nje ambao wanasimamia upande wa Bodaboda.
Kila Bodaboda anayepita anatoa Shilingi 300 au 200 kwa kuwakabidhi wahusika (walinzi) ambao hawatoi risiti ya Kielektroniki na wanapeana zamu kukaa eneo la hilo.
Wakiona 'jau' wanarejea na kuanza kutoa risiti, ni kama vile wanapeana zamu kula 'matunda'.