Ndugu wasio na shukrani!

Ndugu wasio na shukrani!

Naam, kuishi kivyako ndo kwenyewe.

Laiti watu wengi wangekuwa na falsafa kama yangu ya 'live and let live', basi mitafaruku ingekuwa michache sana hapa duniani.

Bahati mbaya uhalisia wa maisha hauko hivyo!

..precisely! Kila mtu anaishi anvyoona inamfaa.
 
Ndugu wa hivi siwezi kabisa, miaka hii ni bora kuishi kivyako tu coz wenye uwezo wanalalamika, wasio na uwezo wanalalamika. Ya nini kumtembelea mtu ambaye atakutangaza kuwa ulienda kula ubwabwa kwake?
Kuna baadhi ya ndugu ni mtihani sana, hawezi kukutendea wema akanyamaza. Lakini tuvumiliane, hakuna mkamilifu, huenda hao tunaohisi wanatukwaza nao kwa namna moja au nyingine tunawakwaza pia bila kujijua.
 
Ndugu wengi sana mimi nimewapotezea....

Nna ndugu yangu mmoja huyo sasa hivi kutwa ananiomba hela
nikimtafutia kazi anaanza kusema subiri kwanza sijui nini
ila hela kuomba haachi

ndugu mzigo
Kuna baadhi ya ndugu ukitaka amani mkutane kwenye harusi...ugonjwa na misiba tu....

Vinginevyo lawama tu
 
Ndugu ni ndugu na ndiyo undugu wenyewe huo mmoja akitoka, basi inaaminika kwamba umefungua njia.

Mimi ndugu zangu hua wanastukia tu kuniona nipo around na ntakuwa na ratiba zangu.

Huwa nawaambia kwamba msaada mkubwa kutoka kwangu ni kukusaidia ada ya kozi (ku-top up) unayosoma yenye kuja kukusaidia maishani au kunisaidia shughuli zangu za shamba au kukusaidia mawazo ya ujasirimali.

Halafu wanafahamu siwezi kukusaidia tu bila kuja na business plan, kama kuwa na Barber shop, hair dressing saloon, grosery shop na aina yoyote ile ya biashara.

Lakini mimi sio benki kwani wengine wanaomba hata mitaji kabisa kama 10,000,000 hivi.

Sasa hii si anaweza kuipata akienda benki na business plan yake?

Ila siwasahau ndugu zangu kwa vitu vidogovodogo ambavyo ukiwapa anaweza kuwa nacho wakati wote kama kofia, top original ya Arsenal na handset ya kawaida.

Akiwa nacho anakuwa akikukumbuka kwamba ndugu upo.

Halafu mkuu NN, jaribu kuwaunganisha ndugu zako kwenye WhatsApp Group ndiyo utaona hizo feeds za maombi na utaweza kuchuja zipi za kuzingatia.

WhatsApp inaleta togetherness baina ya ndugu na mnakuwa mkiwasiliana kila mara.

Hizo feeds zingine unapotezea tu.

Mkuu wewe ni family man...na appreciate your level ya mashirikiano...

Cha ajabu mimi,kwenye magrupu nilijitoa,ni kusnitchiana tu,kwa mtazamo wangu

Sipendi mashirikiano na ndugu at all...kama sijazaliwa na mtu na baba na mama mmoja,sina muda kabisa...kwanza kuonekana sionekani kabisaa,plus sijawahi mtafuta ndugu kuomba chochote,tunakutana December na mnakaa unaona kabisa watu hapa wamekuja kuringishiana na baadhi kujiona,na wengine wana tabia ya kujifanya kutawala wengine kisa kakuzidi umri vitu kama hivyo,etc

I wish ningekua na moyo wa kupenda ukoo kiivyo,ila ndio siwezi kabisa

Sipendi protokali za kijinga,umangimeza,etc...halafu kuna ile familia flani hivi ndani ya ukoo zinajifanya ndio zimeshika mpini,nyie wengine ni ng'ombe wa kuwafuata hao...na kwenye hizi koo kuna mawivu ya kijinga mno..

I wish ningekua na moyo wa kifamilia/ukoo...sina kabisa na jiona niko poa tu...

Ila kupenda mambo ya ukoo na undugu ni kitu kizuri,maana ni togetherness,alimradi kusiwe na unafiki tu
 
Ndugu wengi sana mimi nimewapotezea....

Nna ndugu yangu mmoja huyo sasa hivi kutwa ananiomba hela
nikimtafutia kazi anaanza kusema subiri kwanza sijui nini
ila hela kuomba haachi

ndugu mzigo

Heri hata kuomba hela..hela ni mambo ya kupita tu,na kama anaomba kinyume ni rahisi kumpa hoja za kumkatalia ajue u mean business

Tatizo ni ndugu wenye wivu,usengenyaji,roho mbaya,umangimeza,uonevu,umbea,kujiona,dharau,etc

Hao ndio hua hatari kabisa,sipendi kua karibu sababu ya mambo kama hayo,ndugu akikufanyia hayo yanauma zaidi..

Kuhusu hela wala sioni tatizo,anapigwa sound anakaa sawa tu
 
Huwa unawaambia lakini au ndio unakuja kumalizia machungu JF?
 
Huwa unawaambia lakini au ndio unakuja kumalizia machungu JF?

Ohoo mimi tena? Sinaga simile hata kidogo.

Ni makavu bila vilainishi.

Atakayenichukia na anichukie.

Kwanza napenda kuchukiwa.

Hususan pale yule anayenichukia anapokuwa hawezi kufanya lolote zaidi ya kulialia kwa watu.
 
Ohoo mimi tena? Sinaga simile hata kidogo.

Ni makavu bila vilainishi.

Atakayenichukia na anichukie.

Kwanza napenda kuchukiwa.

Hususan pale yule anayenichukia anapokuwa hawezi kufanya lolote zaidi ya kulialia kwa watu.

Hahahaaaa....
 
Mkuu nilidhani hili tatizo ninalo Mimi tu, Mimi sio ndugu tu hadi marafiki long story short. tangu nije ughaibuni kuna ndugu walianza kunitafuta ambao kabla hata salamu sikuwai kuipata. cha ajabu ni kwamba mara kadhaa wamekua wakiomba hela ukiwatumia hata kujibu kama wamepata inabidi Mimi ndio niwapigie tena simu kuuliza . hili jambo limekua likinikera Kwa mda mrefu sana ila sasa hivi nimepata suluhisho ni sina hela basi. ni mwaka wa pili sasa Nina amani vibaya sana na nahisi wameshtuka coz hata kiwango cha pesa walichokua wanaomba mwanzo kimepungua sana .na bado sina
 
Hivi na nyie wengine mnao ndugu wasio na shukrani?

Ndugu ambao hukukumbuka wakati wa shida zao tu?

Huwa mnakabiliana nao vipi watu wa aina hiyo?

Mimi wananikera sana kwa kweli.

Mtu anakuja na kukulilia shida zake lukuki, nawe kwa moyo mweupe kabisa unamsaidia.

Tena unamsaidia kwa kwenda mbali zaidi ya kile alichokiomba.

Cha ajabu [ingawa si ajabu kivile] ukishamsaidia tu, mwenzio anapotea.

Anapotea bila hata kutoa 'ahsante' ya msaada uliomsaidia.

Na akishapotea ndo imetoka hiyo. Kuja kusikia tena toka kwake labda ni awe na shida au kwenye msiba.

Hata salamu tu ya kujuliana hali toka kwake inakuwa tunu.

Naamini katika kutenda wema na kwenda zangu lakini pia sipendi mambo ya kufanyanya wapumb.avu.

Yaani kuniona nakufaa tu wakati wa shida zako. Ukiwa huna shida hata simu zangu hupokei.

Hovyo kabisa hao.....
Wewe si ulisema ni msukuma? Ndivyo mlivyo wasukuma.

Kila siku na bic zenu kwenda kwa shemeji, halafu mnadi nauli ya kurudi home, bic mnapakiza kwenye tata juu kabisa.

Na kila weekend lzm mwende kula chakula kwa dada yenu nauli ya kurudi atoe shemeji.

Sasa mziki awe hajalipa ngwekwe, atajuta kuolea usukumani
 
Wakati mwingine ni heri rafiki kuliko ndugu.... Rafiki anaweza kua mwepesi kukusaidia kwa moyo mkunjufu kuliko ndugu.

Ndugu wengine hawaridhiki iwe amekusaidia ama umemsaidia ni full lawama. Ni ndugu wachache wanaoelewa undugu na kuthamini msaada wa ndugu
 
Daaaah, nilidhan hii kitu inanikumba mm tu, unajitahidi kuwasaidia ,lakini cku ukiwaambia huna wanakununua. Wakidhani we kila siku ni unayo tuu na huna majukumu mengine zaidi ya kuwasaidia wao.
Inaniuma ila ndo hivo unamwachia mungu.
 
Kuna baadhi ya ndugu ukitaka amani mkutane kwenye harusi...ugonjwa na misiba tu....

Vinginevyo lawama tu

Tena ikiwezekana ni kuonana makaburini tu....
ukishazika hapo kila mtu safari ya kurudi kwake....

Huwa natamani tuwe na taasisi za misiba...
sio misiba ya majumbani
mnaenda kama kwenye ukumbi hivi una sign kitabu na mchango wako
huyooo......wanazika taasisi kama nchi zingine
 
Hivi na nyie wengine mnao ndugu wasio na shukrani?

Ndugu ambao hukukumbuka wakati wa shida zao tu?

Huwa mnakabiliana nao vipi watu wa aina hiyo?

Mimi wananikera sana kwa kweli.

Mtu anakuja na kukulilia shida zake lukuki, nawe kwa moyo mweupe kabisa unamsaidia.

Tena unamsaidia kwa kwenda mbali zaidi ya kile alichokiomba.

Cha ajabu [ingawa si ajabu kivile] ukishamsaidia tu, mwenzio anapotea.

Anapotea bila hata kutoa 'ahsante' ya msaada uliomsaidia.

Na akishapotea ndo imetoka hiyo. Kuja kusikia tena toka kwake labda ni awe na shida au kwenye msiba.

Hata salamu tu ya kujuliana hali toka kwake inakuwa tunu.

Naamini katika kutenda wema na kwenda zangu lakini pia sipendi mambo ya kufanyanya wapumb.avu.

Yaani kuniona nakufaa tu wakati wa shida zako. Ukiwa huna shida hata simu zangu hupokei.

Hovyo kabisa hao.....

Kabla ya kupeleka lawama/shutuma kwa ndugu zako hao kwanza jiulize, "Je mimi huwa nawatafuta ndugu zangu kuwajulia hali." Ikiwa jibu ni ndio basi una haki ya kushutumu; ila jibu likiwa ni hapana basi utakuwa na lile tatizo la Kiafrika la umungu mtu.

Kuna msemo unasema "Usichotaka kufanyiwa basi nawe usimfanyie mwenzio"

Kikawaida Waafrika tulio wengi tupatapo kitu (hasa uwezo wa kifedha) huwa tuna tabia ya kujiona kuwa sisi ni bora kuliko ndugu wasionacho na kuwaona kuwa wana wajibu wa kututumikia (kama sio kutunyenyekea) kana kwamba sisi ndio Mungu wao duniani.

Ushauri wangu tu Bwana Nyani Ngabu....Kama ulikuwa huwatafuti nduguzo kuwajulia hali kama unavyotaka wakujulie hali basi anza wewe kufanya hivyo ili kujustify your innocence kabla ya kujudge nduguzo
 
Kabla ya kupeleka lawama/shutuma kwa ndugu zako hao kwanza jiulize, "Je mimi huwa nawatafuta ndugu zangu kuwajulia hali." Ikiwa jibu ni ndio basi una haki ya kushutumu; ila jibu likiwa ni hapana basi utakuwa na lile tatizo la Kiafrika la umungu mtu.

Kuna msemo unasema "Usichotaka kufanyiwa basi nawe usimfanyie mwenzio"

Kikawaida Waafrika tulio wengi tupatapo kitu (hasa uwezo wa kifedha) huwa tuna tabia ya kujiona kuwa sisi ni bora kuliko ndugu wasionacho na kuwaona kuwa wana wajibu wa kuwatumikia (kama sio kuwanyenyekea) kana kwamba wewe ndiwe Mungu wao duniani.

Ushauri wangu tu Bwana Nyani Ngabu....Kama ulikuwa huwatafuti nduguzo kuwajulia hali kama unavyotaka wakujulie hali basi anza wewe kufanya hivyo ili kujustify your innocence kabla ya kujudge nduguzo
Najua ninachokizungumzia hapa. Sijakurupuka tu bila kufanya na kujifanyia tathmini. Umakini wangu hauna mfano!
 
Huwezi kumfurahisha kila mmoja, kuna mwezi nilikaa nikawa narekodi kila aliyenipigia simu kuomba hela bila kujali kama nimempa au la, mwisho wa mwezi nikajumlisha zote nikaona ilikuwa ni zaidi ya kipato changu. Hapo ndo nilipothibitisha kuwa siwezi kusaidia kila tatizo linalokuja mbele yangu, mwanzoni nilikuwa napata tabu sana navoona nashindwa kusaidia shida ya ukweli mpaka nakopa ili nimpe mtu mwingine ambao wengi huwa hawalipi au watachelewa sana kulipa
What a thought? Nimeipenda hii!
 
Back
Top Bottom