Ndugu wa mume wanaichonganisha ndoa yangu

Ndugu wa mume wanaichonganisha ndoa yangu

hamuna ndugu anayekupenda hapo. utaletewaje maneno halafu uamini anakupenda? unajua anachokusema kwa ndugu wengine?
nashtuka. unazungukwa. pole yako

mmmh hilo nalo neno miss kwa kweli umenizibua masikio,ila cha kumshukuru Mungu huwa namsikiliza bila kuonesha nimechukizwa
 
Duh hilo mie mwenzio lilinikuta kua niache kazi lakini nilikua na msimamo sana sababu mume alinikuta na kazi yangu
na nilimwambia unanioa lakini kazi yangu siwachi ukikubali sana laa huwezi unataka mama wa nyumbani mie sie..
usijali shosti zidi kumuomba mungu yataisha mwanzo mgumu lakini wataacha wenyewe fisadi hao....

Asante sana!!
 
kwa kweli umenigusa.....neno nalikumbuka nadhan na mume wangu analikumbuka...hawa ndugu hukaa zaid ya miezi 2 ndo anaindoka kesho yake anakuja mwingne.maisha wanayoish kwangu ni yakibosi mno wanaishia kumpelekesha msichana wa kazi.muda wote wanajiona wagen ila mie navumilia tu.na kazi ya kufanya hawana muda wote wako idle.kazi kupiga simu kijijin kwao kuhusu yanayoendelea nyumban kwangu.sikujua kama ndoa ndo zilivyo.

kwakweli hapo dadangu ndoa lazma itavunjika....mwambie mmeo munahitaji faragha na kupanga maendeleo sio kila siku pesa yenu nyie kutuma nauli kuleta na kurudisha wataliii...au kwenu mna-mbuga za wanyama?
Mwambie mzee msaada mnaotoa ni kwa wale wenye uhitaji wa kweli na lazima kuja dar na wengineo kuna m-pesa na tigo pesa. Mfano..

Mnakubaliana kuwa mtapokea ndugu mgonjwa amekuja kwa matibabu na akipona atarudi nyumbani, mwanafunzi amekuja kafikia kwenu then anajiunga shule aliyoitwa na atakaa boarding/hostel, mnapokea ndugu aliyeitwa kwa interview ya kazi na akipata kazi atakaa kwenu miezi 6 then anatoka kwenda kupanga na kuishi kwake..

Na mahitaji mengineyo ya lazima sio utalii huo wa ndani uliojaa umbeya .....kuwa makini mie naona uzembe na upole wenu utawavunjieni ndoa.

Au dadangu ndio mambo ya nyumba mmepangiwa na shirika/ serikal full mi-vyumba iddle haina kazi plus dstv kila kona...watu wanakuja kupumzika kwenu...

Kama vipi iddle rooms fuga kuku na mgeni akija kazi yake kusafisha mabanda na kumtuma kila siku kununua chakula cha kuku na kukata majani ya ngombe...kama hawajakata miguu.

najua nimekuambia ukweli mgumu ila bila kuwa hivyo...mtapiga maktaimu mpaka mnazeeka hata maendeleo hamuyaoni.... Na mwisho wa siku ndoa inavunjika mnatuzalishia watoto wa mitaani.
 
Huoni kama mumeo ni tatizo, umesema mwenyewe kuwa anawatumia nauli kuja hapo kwenu, kwanini anawaleta ndugu zake hapo kwenu, hao ndugu wanaingiza kipato chochote katika familia yako zaidi ya kukuchonganisha na mumeo, na akiambiwa maneno kwanini anakuwa na hasira na wewe. Hatukatai ndugu wasije, waje wasalimie ck mbili tatu waondoke, to me mumeo ndo tatizo

tatizo kivipi? mwanzon hakuwa ivyo kabsa
 
kwakweli hapo dadangu ndoa lazma itavunjika....mwambie mmeo munahitaji faragha na kupanga maendeleo sio kila siku pesa yenu nyie kutuma nauli kuleta na kurudisha wataliii...au kwenu mna-mbuga za wanyama?
Mwambie mzee msaada mnaotoa ni kwa wale wenye uhitaji wa kweli na lazima kuja dar na wengineo kuna m-pesa na tigo pesa. Mfano..

Mnakubaliana kuwa mtapokea ndugu mgonjwa amekuja kwa matibabu na akipona atarudi nyumbani, mwanafunzi amekuja kafikia kwenu then anajiunga shule aliyoitwa na atakaa boarding/hostel, mnapokea ndugu aliyeitwa kwa interview ya kazi na akipata kazi atakaa kwenu miezi 6 then anatoka kwenda kupanga na kuishi kwake..

Na mahitaji mengineyo ya lazima sio utalii huo wa ndani uliojaa umbeya .....kuwa makini mie naona uzembe na upole wenu utawavunjieni ndoa.

Au dadangu ndio mambo ya nyumba mmepangiwa na shirika/ serikal full mi-vyumba iddle haina kazi plus dstv kila kona...watu wanakuja kupumzika kwenu...

Kama vipi iddle rooms fuga kuku na mgeni akija kazi yake kusafisha mabanda na kumtuma kila siku kununua chakula cha kuku na kukata majani ya ngombe...kama hawajakata miguu.

najua nimekuambia ukweli mgumu ila bila kuwa hivyo...mtapiga maktaimu mpaka mnazeeka hata maendeleo hamuyaoni.... Na mwisho wa siku ndoa inavunjika mnatuzalishia watoto wa mitaani.

mmmh kwa kweli umeongea ukweli mtupu,nitazingatia mawaidha yako.
 
Pole sana, Busara zako unazozitumia ndiyo msingi tosha wa kuiokoa ndoa yako simamia kwenye kweli jenga msimamo machoni mpaka rohoni na pia omba mungu akuongoze kwenye kweli yatakwisha na utayasahu ubarikiwe sana!
 
Huoni kama mumeo ni tatizo, umesema mwenyewe kuwa anawatumia nauli kuja hapo kwenu, kwanini anawaleta ndugu zake hapo kwenu, hao ndugu wanaingiza kipato chochote katika familia yako zaidi ya kukuchonganisha na mumeo, na akiambiwa maneno kwanini anakuwa na hasira na wewe. Hatukatai ndugu wasije, waje wasalimie ck mbili tatu waondoke, to me mumeo ndo tatizo

Hapo umenena ram
 
Pole sana, Busara zako unazozitumia ndiyo msingi tosha wa kuiokoa ndoa yako simamia kwenye kweli jenga msimamo machoni mpaka rohoni na pia omba mungu akuongoze kwenye kweli yatakwisha na utayasahu ubarikiwe sana!

amina.
 
Ndo sababu nakuambia kuwa mumeo ndo tatizo hapa, nauli anatuma mwenyewe, ndugu wanakuja, wanakaa tu tena bila kazi yoyote, kazi yao kupika majungu, kichwa cha familia kiko kimya tu, tena kikiambiwa majungu kinanuna, akha! waje hapo kwako sio kwangu

Haya kila la heri bibie na wifi na mashemeji zako kutoka singida

kwa kweli umenigusa.....neno nalikumbuka nadhan na mume wangu analikumbuka...hawa ndugu hukaa zaid ya miezi 2 ndo anaindoka kesho yake anakuja mwingne.Maisha wanayoish kwangu ni yakibosi mno wanaishia kumpelekesha msichana wa kazi.Muda wote wanajiona wagen ila mie navumilia tu.Na kazi ya kufanya hawana muda wote wako idle.kazi kupiga simu kijijin kwao kuhusu yanayoendelea nyumban kwangu.Sikujua kama ndoa ndo zilivyo.
 
mhh pole dada,ndugu wa mume ni pasua kichwa inahitaji uwe mkali ni bora wakuchukie lakini simamia ukweli.Na wakikaa kipind kirefu namna hiyo shoga yangu wataitawala nyumba yako.usikubali kabisa nyumba yako itawalike.
 
Yah sure, inaweza piga mvua hadi ukashangaa ikikatika sasa jua lake utadhani haijawahi kuunyeesha hata siku moja, so utakuja lini tena

Jua, mvua lote lenu napenda sana hili jiji THE ROCK CITY
 
watongoze watakimbia wenyewe,au singizia wanakutaka,fanya kama mke wa farao hawatarusha tena mguu
hapo

ushauri wa nguvu za ngiza naomba usiutumie huu achana nao ni mabya zaidi kusingizia kitu kama hiki maana kinagusa direct maisha ya ndoa yenu kinaweza kukusababishia kuachwa au hata kuuwawa kwa hao ndugu zake au hata wewe acha kabisaa usifuate huu ushauri muachie aliyeleta na shetani wake
 
Back
Top Bottom