Ndugu wa mume wanaichonganisha ndoa yangu

Ndugu wa mume wanaichonganisha ndoa yangu

activisty

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
315
Reaction score
107
Habari ndugu wanajf,naomba mniwie radhi kama nitakuwa sina mpangilio mzuri wa andiko hili.
Nimekuja hapa jf nikiamini ni mahali pekee nitakapopata ushauri ambao utanisaidia kuiokoa ndoa yangu.
Yapata mwaka na nusu sasa tangu nifunge ndoa na mume wangu kipenzi,tumejaliwa kupata mtoto mmoja wa miez 6 sasa.Tangu nifunge ndoa ndugu wa mume hawachoki kuja nyumban kwangu kutoka kijijini kwao huko singida,mwanzo ndoa yetu ilikuwa na furaha mno ila tangu movements za hawa ndugu naona dosari zinaanza.
Wamekuwa ni watu wasiokuwa na fadhila hata kidogo,wamekuwa walalamishi mno.mbaya zaid wamekuwa wakipeleka maneno ya uongo kwa kaka yao hususan pale ndugu na rafik zangu wakija kunitembelea wanasikiliza maongez yetu(maongez ambayo ni ya kawaida sana ndo maana huwa tunaongea mbele yao) wanadai kuwa ndugu zangu wananipa kiburi sasa cjui kiburi cha nn maana naish nao vizuri na kuwajali vizuri tu.
Nashindwa kuelewa lengo haswa la hawa ndugu ni nini maana sasa hivi wanakuja kwa kupokezana utafikir wanalinda kitu.Mume wangu huwa analalamika kuja kwao ila yeye ndiye anawatumia nauli sasa cjui ananijaribu?? Ila siku zote huwa nakaa kimya pale anapolalamika.
Nimejua wao ndo wachonganishi maana kuna mmoja kati yao ananipenda sana hivyo huwasikiliza wenzie na kuja kuniambia,nikajaribu kuwa busy na mambo yangu wanalalamika tena hadi mume wangu akaniambia niwe napiga nao story maana wanalalamika...hilo pekee ndilo aliloniambia ila sijaweza kumwambia sababu ya mimi kuwa mbali nao sitaki kuwachonganisha.
Mambo mengne wanayopeleka kwa kaka yao sijui hata wanayapata wapi!! Naona tu mume wangu anakuwa na hasira zisizoisha,mbaya zaid na yeye ni mtu wa kukaa na vitu moyoni.
Naipenda ndoa yangu na nataka kuinusuru...maana nimeanza kuwachukia hawa ndugu kutokana na matendo yao.Nifanyaje wanaJF??
Naomben ushauri wenu ili niinusuru ndoa yangu.Mume wangu ananipenda sana na mimi nampenda sana.naomben msaada wenu.
 
duh pole sana hilo ni tatizo ila kuwa mvumilivu tu huna jinsi
 
Kwanza pole shosti na matatizo ya ndugu wa mume,hayo mambo niyakawaida lakini kwasababu wewe ni mgeni kwenye ndoa
ila mtangulize mwenyezi mungu kwenye kila jambo lako,zidisha mapenzi kwa mumeo na kumbuka wawili wakipendana adui hana nafasi...
 
Wanyiramba nao.... usiombe kukutana na wifi wa kinyiramba, kwa ufupi tu mumeo ndio tatizo katika ndoa yenu
 
Wanyiramba nao.... usiombe kukutana na wifi wa kinyiramba, kwa ufupi tu mumeo ndio tatizo katika ndoa yenu

tatizo kivipi? mwanzon hakuwa ivyo kabsa
 
Kwanza pole shosti na matatizo ya ndugu wa mume,hayo mambo niyakawaida lakini kwasababu wewe ni mgeni kwenye ndoa
ila mtangulize mwenyezi mungu kwenye kila jambo lako,zidisha mapenzi kwa mumeo na kumbuka wawili wakipendana adui hana nafasi...

Asante shosti matatizo ni makubwa mno.uniombee sana mfano mama mkwe anamwambia mwanae niache kazi niwe nakaa nyumbani muda wote,nashukuru Mungu mwanaume alilipinga hilo.
 
Mnhhh...anyway kama naweza kukuuliza vile...mlivofunga ndoa nkanisani kunasomo huwa linasomwa kuwa utawaacha baba na mama zako na kuambatana na mumeo vivo hivo mume atawaacha baba na mama zake na kuambatana na mkewe...sooo ndugu hapa wanakujaje na kutaka kuvunja ndoa yako?

Mwambie mumeo na wewe pia muwe-very bold kwa ndugu...kama anakuja aje kusalimia mwisho 1 week na kama anakuja kuishi nanyi awe na kazi ya kufanya sio kuja kukaa vijiwe umbea na kuanza kumchunguza mke/mume wa ndugu yao....iddle mind iz the devilz hauz...ahahahahaaa

ni hayo tu kwa leo.
 
Funguka mweleze mumeo juu ya ujio wa hao ndugu mara kwa mara, mwambie unawapenda sana lkn muwasaidie huko huko maana wanaitia ndoa yenu katika majaribu. Nadhani atakuelewa na umtangulize mungu kabla ya kuzungumza naye. Ndoa ni watu wawili zungumza na mwenzio kwa nia njeama nae ataona tatizo na mtaweza kulimaliza.
 
watongoze watakimbia wenyewe,au singizia wanakutaka,fanya kama mke wa farao hawatarusha tena mguu
hapo
 
usione soo sema nae bwana huyo mume wako. wewe unasema mumewe ni mtu wakuweka vitu moyoni na wewe pia una tabia hiyo hiyo. sasa ongea na kiustarabu na eleza kuwa bwana wee haya mambo ya ndugu hapa home kila leo mie sipendi period. sijasema kuwa hawawezi kuja ila waje kimpangilio bwana.....tumeona ili tuwe na kwetu tuenjoy upendo wetu sio kuingiliwa. mazungumzo ni muhimu dada ongea na mumeo bwana.
 
Funguka mweleze mumeo juu ya ujo wa hao ndugu mara kwa mara, mwambie unawapenda sana lkn muwasaidie huko huko maana wanitia ndoa yenu katika majaribu. Nadhani atakuelewa na umtangulize mungu kabla ya kuzungumza naye. Ndoa ni watu wawili zungumza na mwenzio kwa nia njeama nae ataona tatizo na mtaweza kulimaliza.

Asante kwa ushauri wako,cha kushangaza yeye mwenyewe muda mwingine analalamika kwamba "fulani anataka kuja...anakuja kufanya nini?? wanasumbua sana sina hela mm" haipiti wiki yule ndugu anakuwa amewasili tena yeye ndo kamtumia nauli....sijui ata nitaanzia wapi kuongea naye.
 
usione soo sema nae bwana huyo mume wako. wewe unasema mumewe ni mtu wakuweka vitu moyoni na wewe pia una tabia hiyo hiyo. sasa ongea na kiustarabu na eleza kuwa bwana wee haya mambo ya ndugu hapa home kila leo mie sipendi period. sijasema kuwa hawawezi kuja ila waje kimpangilio bwana.....tumeona ili tuwe na kwetu tuenjoy upendo wetu sio kuingiliwa. mazungumzo ni muhimu dada ongea na mumeo bwana.

Asante Mzabzab huwa natamani kuongea ila naona kama nitaingilia mambo yake na nduguze...kwa ushaur wako nitaongea naye liwalo na liwe.
 
Asante kwa ushauri wako,cha kushangaza yeye mwenyewe muda mwingine analalamika kwamba "fulani anataka kuja...anakuja kufanya nini?? wanasumbua sana sina hela mm" haipiti wiki yule ndugu anakuwa amewasili tena yeye ndo kamtumia nauli....sijui ata nitaanzia wapi kuongea naye.

Utaanzia kuelezea kuwa wewe na yeye ni mtu na mume so mnatakiwa kujenga maisha yenu na kuishi kwa amani, upendo na furaha ndugu wapo na watakuwepo na wanamaisha yao pia so mnatakiwa kupanga jinsi ya kuwasaidia na si kuwa sehemu ya maisha yenu ya kila siku..............
 
Mnhhh...anyway kama naweza kukuuliza vile...mlivofunga ndoa nkanisani kunasomo huwa linasomwa kuwa utawaacha baba na mama zako na kuambatana na mumeo vivo hivo mume atawaacha baba na mama zake na kuambatana na mkewe...sooo ndugu hapa wanakujaje na kutaka kuvunja ndoa yako?

Mwambie mumeo na wewe pia muwe-very bold kwa ndugu...kama anakuja aje kusalimia mwisho 1 week na kama anakuja kuishi nanyi awe na kazi ya kufanya sio kuja kukaa vijiwe umbea na kuanza kumchunguza mke/mume wa ndugu yao....iddle mind iz the devilz hauz...ahahahahaaa

ni hayo tu kwa leo.

kwa kweli umenigusa.....neno nalikumbuka nadhan na mume wangu analikumbuka...hawa ndugu hukaa zaid ya miezi 2 ndo anaindoka kesho yake anakuja mwingne.Maisha wanayoish kwangu ni yakibosi mno wanaishia kumpelekesha msichana wa kazi.Muda wote wanajiona wagen ila mie navumilia tu.Na kazi ya kufanya hawana muda wote wako idle.kazi kupiga simu kijijin kwao kuhusu yanayoendelea nyumban kwangu.Sikujua kama ndoa ndo zilivyo.
 
Asante shosti matatizo ni makubwa mno.uniombee sana mfano mama mkwe anamwambia mwanae niache kazi niwe nakaa nyumbani muda wote,nashukuru Mungu mwanaume alilipinga hilo.
Duh hilo mie mwenzio lilinikuta kua niache kazi lakini nilikua na msimamo sana sababu mume alinikuta na kazi yangu
na nilimwambia unanioa lakini kazi yangu siwachi ukikubali sana laa huwezi unataka mama wa nyumbani mie sie..
usijali shosti zidi kumuomba mungu yataisha mwanzo mgumu lakini wataacha wenyewe fisadi hao....
 
Back
Top Bottom