Ndoa yangu inakaribia kuvunjika,msaada jamani

Ndoa yangu inakaribia kuvunjika,msaada jamani

huyo mwanaume ana mawazo mgando kipindi cha mvua yanayeyuka kwa tabu mpeleke akafanyiwe maombezi au mpige talaka tatu oh sorry kumbe wanaotoa talaka tatu ni wanaume tu,cha msingi waone wazazi kwa ushauri zaidi.Mungu akutangulie na kukutia nguvu hawa viumbe hata uwapende vipi utaambulia manyoya.
 
Mtoto tu wa kiume? hapana hapo kuna jambo jingine. Una uhakika huyo ni mwanae au ulichomoa pengine? au umeshaanza kuwa na macho mawili?. Tafadhari wanajamvi mubaneni vizuri huyu asije kuwa anatumalizia bundle zetu kwa ujinga wake.
 
Huyo mume mtu anajua makabila yote ni kama wao, wanawake wa machame hapa arusha wanaitwa "wapalestina" mkizaa watoto wawil akienda kwao ndugu zake wana muuliza 'naore kabat ya mbeho, naore radio ya picha' kama jibu ni ndio, akirudi unapotea...ndio stereotype iliyojaa mtaani kuhusu wanawake wa kichaga hususan wamachame
 
Wadada wa hilo kabla ndo walivyo ujue wameshamtafutia shangingi wewe endelea kuomba na ukiweza piga simu kwa huyo hapo kwenye avatar ya mamndenyi akufanyie maombi.
 
Labda wapare wa MACHAME mana wao ndo wanadaiwa walikua na tabia ya kufanya matukio kama hayo,Au wanataka kukugeuza hela.wapare original kama mimi hawauwi waume zao hata siku 1 awe tajiri au mpate mtoto wa kiume,Wapare wana mapenzi ya dhati.

Keba umvirwe.. Avo mawifi vavo ni manyawi kabisa.
 
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani

Duh kweli kua yakukute na si uyakute!
Yaani mumeo mpaka sasa mtu mzima na familia yake bado anachukua maneno ya dada zake kama yalivyo..?!
Hana ubongo wa kufikiria na kuchambua lipi jema na baya?
Ye kila anachoambiwa anakubali kama kilivyo?! Pole sana dada kama mume ulipata!!
Kweli ndoa huvyunjwa kwa mikono ya wanandoa wenyewe haijalishi mume au mke!
Pole sana.., ila kazi ya kumtapisha mmeo maneno ya dada zake sio ndogo, maana anaonekana anawaamini kupita kiasi kuliko vile anavyokuamini wewe mkewe!
 
hiyo ni kama excuse tu kwa huyo,ila kuna zaidi ya hicho.maana haiingii akilini hata kidogo.utafikiri ana miaka 10 bwana.kaa nae muelimishe,au mwambie mtu mzima yoyote yule amueleweshe
 
Pole sana dada yangu,jaribu kuwahusisha wazazi wa pande zote 2 ili waweze kukusaidia katika hilo. Lakini PIA mwambie afanye uchunguzi ni wapare wangapi wameua waume zao kwa sababu hiyo
 
Pole sana Kima Mdogo, mchunguze mumeo vizuri, inawezekana anatafuta tu sababu ya kukuacha, kwa sababu kama anakupenda kweli hawezi kuamua kuamini mila ambazo wamachame wenge hawaziamini.
 
Kweli kuishi ni kuona mengi, yaani hii inanikumbusha jamaa mmoja ambaye alikatwa kiganja cha mkono wa kushoto na mashine ya kuchana mbao akataka kujiua lakini wasamaria wakamuokoa!! kufka hospitali akakuta mwenzake amepata ajali mbaya na amekatwa miguu yote na mkono mmoja, ghafla akasahau kabisa kama kukosa kiganja ni issue na very soon akaizoea hiyo hali. Maana yangu ni kwamba kuna watu kwenye ndoa/mahusiano ambao hawana hata mtoto wa dawa na wamehangaika kila kona imeshindikana; kuna watu wamepata watoto wa kike tu na wamehangaika kubahatisha kupata wa kiume wameishia kufikisha watoto mpaka 10 bila mafanikio. Mwisho mbona hayo ni mambo ya kizamani sana?? Wanawake wa kimachame huko nyuma ndio walikuwa na historia ya kuuwa wanaume wao ili wapate mali, kama alivyosema angel msofe tatizo ni huyo mume kumepelekwa puta na dada zake na asipostuka atavunja ndoa yake. Itisha kikao na wazee wenye busara wa pande zote mbili wahusishwe.
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani
 
Last edited by a moderator:
Kweli kuishi ni kuona mengi, yaani hii inanikumbusha jamaa mmoja ambaye alikatwa kiganja cha mkono wa kushoto na mashine ya kuchana mbao akataka kujiua lakini wasamaria wakamuokoa!! kufka hospitali akakuta mwenzake amepata ajali mbaya na amekatwa miguu yote na mkono mmoja, ghafla akasahau kabisa kama kukosa kiganja ni issue na very soon akaizoea hiyo hali. Maana yangu ni kwamba kuna watu kwenye ndoa/mahusiano ambao hawana hata mtoto wa dawa na wamehangaika kila kona imeshindikana; kuna watu wamepata watoto wa kike tu na wamehangaika kubahatisha kupata wa kiume wameishia kufikisha watoto mpaka 10 bila mafanikio. Mwisho mbona hayo ni mambo ya kizamani sana?? Wanawake wa kimachame huko nyuma ndio walikuwa na historia ya kuuwa wanaume wao ili wapate mali, kama alivyosema angel msofe tatizo ni huyo mume kumepelekwa puta na dada zake na asipostuka atavunja ndoa yake. Itisha kikao na wazee wenye busara wa pande zote mbili wahusishwe.
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani
 
Last edited by a moderator:
nasikia ukiolewa na mmachame hakikisha hana madada,kama ana dada bora usiolewe nae.pole sana vumilia tu hilo nalo litapita

haya unayoyaongea umeyasikia ila huja proove kam ni kweli yanatokea.
nina kaka 1 na tupo dada 5 hatujawah hata kumuuliza wifi anaish vipi na mumewe. sembuze kumtilia bifu??? bifu ni aina mtu na sio kabila.
 
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani

Sijawahi sikia Wapare wanaua waume zao! Wamekuchoka wanakutafutia sababu. Jiandae kwa lolote, usiogope ikibidi ndoa kufa acha na ife hao wachaga wapate wakati mzuri wa kufanya matambiko yao!
 
Dada pole sana kwa yanayokukuta, Kama alivyoshauri Lara 1, tumieni viongozi wenu wa kiroho /Dini kuwekana sawa ili imani inayopandikizwa hapo ife, vinginevyo ukichelewa kulifanyia kazi, utashangaa mara anaanza kula kwa dada zake/mama yake akidai huenda chakula chako kina sumu, pengine anzishe nyumba ndogo huko kwa kisingizio hiko hiko, mwishowe atahama nyumbani kabisa.

Tafadhali zingatia kuwashirikisha hao mapema, ‘shetani hatamani kuona upendo na umoja katikati yetu, kwa sababu yeye ni baba wa uongo hupandikiza chuki/uongo ili kuleta mafarakano’

Endelea kuomba sana juu ya hilo, Na wachache wetu pia tutaendelea kukuombea.
 
Back
Top Bottom