Ndoa ya CCM na CUF ilifanyika lini?

Ndoa ya CCM na CUF ilifanyika lini?

Lisemwalo lipo...!

kama halipo linakuja, mimi naona lishakuja walichofanya chadema sijuwi kama wametumwa na CCM au wamefanya wenyewe, kwasababu vigogo wa usalama wa taifa (akina Marando) wamepelekwa huko, ni kuugawa upinzani na nguvu zake, mimi nakubalina na Mwiba kwa hoja kuwa U-turn ya Dr. Slaa imedhoofisha nguvu ya upinzani. It was untimely and not well calculated....may be they are being used.
 
A lot will be talked. Tunataka kusikia vyama vitatufanyia nini. Slaa ametoa vipaumbel vyake. Soma MwanaHALISI la leo utaziona. They make a lot of sense!
 
Hivi na busara zenu mnaamini kuwa laiti JK na CCM wangekuwa na uhakika wa ushindi wangehangaika kuchangisha bilioni 50 kwa ajili ya kampeni?Au kubwa zaidi,laiti JK angekuwa na uhakika wa kushinda kirahisi angeanguka Jangwani kwa panic?

kama Chadema ingekuwa na uhakika wa kushinda ingepokea sh. milioni 100 kutoka kwa Sabodo wa CCM.
 
.

kwani JF ni ya mgombea yupi hadi una mashaka na wanaCCM kuwemo humu?

Karibu sana PIPIJOJO hapa kwenye jamvi letu. Ila huwa kuna sheria humu; muda si muda utapewa ndo uendelee. Kama umejiunga kuokoa jahazi lenu pia si mbaya, tulia tuli upate sheria zetu.

PIPIJOJO
  • profile.png
    View Profile
  • forum.png
    View Forum Posts
  • message.png
    Private Message
  • article.png
    View Articles
  • add.png
    Add as Contact
  • email.png
    Send Email
user-online.png
Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join Date Thu Aug 2010
Posts 19
Thanks : 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power0
 
Tungoje wote wakianza kampeni, ndipo tutajua. Lakini ieleweke kuwa watanzania hasa huku porini/kijijini kwetu wamechoka sana. Nashindwa kuelewa wanatoa wapi nguvu hizi za kuhudhuria minkutano.

Wangechoka wasingehudhuria mikutano ya CCM....umeona kampeni za Kikwete zinavyojaa watanzania wengi.
 
Mwiba usemi wa kuwa CUF wangeshinda labda visiwani but sio bara kama ilivyotokea 2005.
CHADEMA walimtangaza Dr late as a strategy assuming CCM wanajua figures ni zile zile Lipumba,Mbowe,Mrema etc
The UTURN approach made by CHADEMA ndo inawafanya CCM kuhaha daily ata kufikia kiwango cha kuhonga watu kwenda kwenye mikutano ya hadhara
 
Hapa unamsema Benjamin Mkapa aliyevunja mkono au Mrisho JK Mziray?

AU ndiyo unawa-Confuse (changanya) wote wawili?

aaaaaha kumbe unaelewa sina maana wa CCM ni wa Chadema. Wenye vifafa huwa wanaanguka na kuvunja mikono
 
.

kwani JF ni ya mgombea yupi hadi una mashaka na wanaCCM kuwemo humu?

Nashangaa, kuna wakati nasoma post za watu huku ndani na kujiuliza kama JF ni mtandao huru au wa chama fulani.

Ndugu zangu, lazima tukubaliane hii ni free speech forum. Anayeamini na kuipenda CCM ana haki sawa na wale wanaoipinga alimradi havunji sheria.
 
Hahahaa Nyamizi. Naona ile story ya Mbayuwayu inaendelea................

"Rais wa Kifafa changanya na Rais wa kuanguka na kuvunja mkono."

Marehemu Mzee JK Kifimbo aka Nyerere angelikuwa hai, angelisema kama alivyoambiwa Mwinyi na kuongoza nchi akiwa Kitandani na Sitti Mwinyi. Kangelisema waziwazi na live ili kila mtu asikie na bila kuuma maneno:

"Rais wetu ni mgonjwa, tena mgonjwa sana. Ila kwa kuwa si vizuri kumuondoa Rais madarakani, basi tusubiri muhula wake uishe.........."
Sasa hivi angelikuwa akigombea mtu mwingine kabisaaa..........

Anawasema wote wawili! Nimecheka sana:smile-big:
 
Wapenzi wa CCM safari hii hadi mnatia huruma tofauti na mwaka 2005, mngekuwa mnajiamini msingekuwa mnakesha kwenye mitandao kama hivi wakati huu mngekuwa mmelala.
Nadhani wewe unafikiri wote wanakesha kama wewe.
 
Mhhh another conspiracies! I beg you to communicate with ur brain before posting rubbishes and worms in the forum!


Ukisoma habari hii utagyundua ni kweli CHADEMA hawakuwa na mpango wa kumsimamisha mgombea urais..... Endelea

WAKATI vyama vya CCM na Chadema vikiwa vimetangaza kampeni za angani, CUF imetangaza kuwa itashambulia kwa kutokea ardhini, huku ikimtaka Zitto Kabwe akae chonjo kwenye Jimbo la Kigoma Kaskazini.

CUF imetangaza mkakati huo jana, ikieleza kuapnai kuzibomoa ngome za CCM na Chadema kwenye Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa kuwachukua makada wake maarufu, akiwemo Sijapata Nkayamba, aliyekuwa mbunge viti maalumu wa chama hicho tawala.

Akitangaza mpango mzima wa kampeni za chama hicho zitazozinduliwa Ijumaa kwenye Uwanja wa Kidongo Chekundu, mkurugenzi wa siasa wa CUF, Mbaralah Maharagande alisema uamuzi huo umezingatia kwa kina tathmini ya kampeni katika vipindi vyote vya nyuma.

"Tumefanya tathmini katika chaguzi zilizopita kuanzia mwaka 1995, 2000 na 2005, tulibaini kulikuwa na makosa, kwa hiyo hatutaki tena kurudia makosa yale yale katika kampeni," alisema Maharagande.

"Kwa hiyo... tutatumia nchi kavu; kuweka kambi na kuelimisha vema watu wetu wasimamie kura kuhakikisha haziibwi na mawakala wa usimamizi wa uchaguzi. Tuna mtandao hadi vijijini... hiki si chama cha promotion sawa na bidhaa mpya.

"Tutafanya kampeni za kistaarabu... tumeona unaweza kutembea juu, lakini huku chini kura zikakosa wasimamizi wa kutosha. Sisi tumejifunza na hatutaki kufanya makosa tena."

Alifafanua kwamba baada ya uzinduzi wa kampeni zao, msafara wa viongozi wa CUF utakuwa tayari kusambaa maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya kufanya kile alichokiita mashambulizi ya nchi kavu ya kuing'oa CCM Oktoba 31.

Maharagande alisema Agosti 27, msafara tofauti ya viongozi wa chama hicho, ikiongozwa na mgombea wao wa urais, Profesa Ibrahim Lipumba na mgombea mwenza Juma Duni Haji, itaanza kuelekea mikoani.

Katika ratiba hiyo, Maharagande alisema Profesa Lipumba ataanzia mkoa wa Pwani kwa kupita Kibiti, Ikwiriri na baadaye kuelekea Kilwa, Lindi na ukanda mzima wa kusini huku mgombea mwenza akianzia Kagera.
Alijigamba kwamba wanayo magari ya kutosha ya msafara na yale ya uhamasishaji.

Alitamba kwamba sababu za kutumia kampeni za nchi kavu wanazo ikiwa ni pamoja na mtandao wake mkubwa katika ngazi za vijiji na mitaa na kuongeza kuwa "CUF si chama cha promotion kama vile bidhaa mpya".

"Ni chama ambacho kimejikita vema hadi vijijini... hata katika uchaguzi wa serikali za mitaa baada ya CCM ni CUF. Ni chama ambacho mgombea urais alifahamika mapema, siyo chama ambacho bado siku 72 kwa uchaguzi mgombea urais hajulikani, na kubaki kudhani mara mgombea mwenza atakuwa Hamad Rashid; sijui nani; hatuko hivyo."

"Tutafanya kampeni kitongoji kwa kitongoji; tutaweka kambi kuhakikisha watu wanasimamia vema; watu wetu lazima waelewe kulinda kura kwanza; siyo unapaa angani wakati chini kura zako hazina msimamzi wala huna mtandao. CUF chama kubwa."

Akizungumzia programu nyingine, alisema keshokutwa pia chama hicho kitazindua Ilani yake katika hafla ambayo watu mbalimbali wamealikwa na kwamba ilani hiyo inatoa dira ya mabadiliko nchini.
Maharagande alisema ilani hiyo itaonyesha ni kwanini ilikuwa ni makosa kuendelea kuipa CCM nafasi ya kuongoza na kusababisha umasikini katika miaka yote 49 ya uhuru.

Katika hatua nyingine, CUF imefanikiwa kuzibomoa ngome Chadema na CCM mkoani Kigoma kwa kuchukua makada maarufu ambao wanakiweka chama hicho katika nafasi nzuri ya kuweza kutwaa majimbo mawili mkoani humo.

Nkayamba, ambaye aliangushwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM kwa kuwa mtu wa nne na kuhamia CUF, anawania ubunge wa viti maalumu Kigoma Kaskazini, huku mshindi wa pili wa kura za maoni kutoka chama hicho tawala naye akijiunga na chama hicho cha upinzani na kuwa mgombea wa jimbo hilo ambalo linawaniwa pia na Zitto.

Akitangaza ujio wa wanachama hao, naibu mkurugenzi wa habari wa CUF, Ashura Mustafa alisema Zitto akae chonjo kwa kuwa ngome hiyo sasa imehamia CUF kutokana pia na kada maarufu wa Chadema na diwani kwa miaka 15 katika kata yenye watu wengi ya Mwandiga, kuhamia chama hicho pinzania.

Omar Musa Nkwarulo, ambaye alikuwa mshindi wa pili katika kura za maoni CCM, alisema ameamua kukihama chama hicho tawala kutokana na siasa za kubebana na kuonya hizo ndizo zitachangia kifo cha CCM.

Nkwarulo alidai kuwa ana uhakika alikuwa ameshinda kwenye kura za maoni CCM, lakini kura katika eneo alikozaliwa lenye watu karibu 2,500 hazikuhesabiwa kwa kile alichokiita kuwa ni chama kumbeba mgombea mwenzake.

Alitamba kwamba kutokana na nguvu na ushawishi mkubwa wa kisiasa alionao ana uhakika wa kulinyakua jimbo hilo huku akimpa onyo Zitto kwamba ataanguka kutokana na kusahau jimbo hilo na kuliacha likiwa na umasikini wa kutisha.

CUF pia imemnyakua Optatus Likwelilo kutoka CCM ambaye naye atasimama kugombea ubunge Jimbo la Kigoma Kusini, huku akitamba kulinyakua kutoka katika chama hicho tawala.

Kwa upande wa Nkayamba alisema CCM ni chama ambacho kimejaa mizengwe huku akisisitiza kwamba licha ya kuwa mshindi wa tatu bado alitupwa hadi nafasi ya nne katika mchakato wa kuwania jimbo hilo.

Naye diwani huyo wa muda mrefu wa Chadema wa tarafa hiyo ya Mwandiga alikituhumu chama hicho kuwa kimejaa makundi, ubinafsi ambao unaanzia kwa uongozi wa ngazi ya juu.

Source: Mwananchi
 
Back
Top Bottom