Kwa hilo jicho bama analomwangalia huyo mama wa kichina, naapa kama hajapiga laaazma atapiga! Bisha usibishe.
UDAKU mwingine jama ni kiboko sasa hapo kuna picha gani mbaya
Maana huyo mdada kuSmile kwao ni jadi hata alipokutana na Kikwete.
sasa wameshamzushiwa Michelle wa Obama kuwa anaondoa Ikulu.
Ni KITU KISICHOWEZEKANA
Mchaga wa wapi wewe xmas inakukuta Magomeni?
Ndoa ya Rais wa Marekani Barak Obama na Michelle Obama ipo hatarani kuvunjika kufuatia kitendo cha Obama kuonekana katika picha za kimahaba na waziri mkuu wa Thailand Shinawatra. Inasemekana picha zenye kutiliwa shaka pia zilipigwa kati ya Obama na waziri mkuu wa Denmark.
Habari za ndani zinaeleza kuwa tayari Michelle ameshaanza kulala kwenye kitanda cha peke yake, na anajiandaa kuondoka Ikulu na kuhamia kwenye nyumba yake binafsi. Taarifa zinaeleza zaidi kwamba hadi hivi sasa, wawili hawa hawapo kwenye ndoa, bali wanajaribu kuwa pamoja kwa ajili ya watoto na kwa ajili ya kulinda status ya Obama. Hata hivyo taarifa zinaeleza kwamba Michelle anaonekana kushindwa kabisa kuvumilia kuwa kwenye mahusiano ya mke na mme na Obama kwa kuwa anahisi kudhalilishwa vibaya kufuatia kitendo hicho cha Obama kupiga picha za kimahaba hadharani. Tayari Michelle anajadiliana na mwanasheria wake kuona kama anaweza kudai talaka.
Hii itakuwa ni aibu kubwa kwa Obama iwapo mkewe ataamua kuomba talaka na kuondoka white house kabla ya Obama kumaliza muda wake wa Urais. Washauri wanajitahidi kumtuliza Michelle ili asubiri hadi Obama amalize muda wake madarakani. Japo jambo hili limeelezwa kuwa ni siri kwa muda mrefu, tayari taarifa za mifarakano ya wawili hawa zimeshavuja kwenye vyombo vya habari vya marekani.
Kwa taarifa zaidi soma hapa:
Obama, Michelle
Celebrity Gossip and Entertainment News: First Lady Furious Over President's Flirting with Thai Prime Minister
Acha longo longo wewe, hujaona kwamba nimeweka na links hapo ili ujisomee mwenyewe? MImi nina sababu gani ya kupageuza hapa Sani au Kiu? Pananisaidia nini kwa kufanya hivyo?Kwahiyo juzi walipopiga picha hapo south ndiyo ilianzia hiyo ishu au ??
Maana naona hapa jfk umeshaapafanya kiu ijumaa na sani sasa
Hii Nayo itakuwa imechangia timbwili timbwili
Mchaga wa wapi wewe xmas inakukuta Magomeni?