Ndoa ngumu jamaani, ushauri tafadhari

Ndoa ngumu jamaani, ushauri tafadhari

Realme

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
214
Reaction score
155
Napenda kufahamishwa ni mambo gani ya kuvumilia katika ndoa na yapi sio ya kuvumilia?(Yaani yapi yakitokea ndoa ife? na yapi ya kusamehe)

Unawezaje kumsamehe na kuendelea kuishi na mwanaume ambaye amezaa nje ya ndoa tayari akiwa katika ndoa?

Inamaanisha nini watu wanaposema vumilia katika ndoa kwa ajili ya watoto?, eti usiwe m-binafsi kujiangalia mwenyewe.

Na maneno kama simama upiganie ndoa yako. napiganaje?

Je ni mwanamke pekee ndo anahitajika kupigania ndoa yake?
 
Napenda kufahamishwa ni mambo gani ya kuvumilia katika ndoa na yapi sio ya kuvumilia?(Yaani yapi yakitokea ndoa ife? na yapi ya kusamehe)
Unawezaje kumsamehe na kuendelea kuishi na mwanaume ambaye amezaa nje ya ndoa tayari akiwa katika ndoa?
Inamaanisha nini watu wanaposema vumilia katika ndoa kwa ajili ya watoto?, eti usiwe m-binafsi kujiangalia mwenyewe.
Na maneno kama simama upiganie ndoa yako. napiganaje?
Je ni mwanamke pekee ndo anahitajika kupigania ndoa yake?

Nadhani kwa hilo hakuna ushauri mzuri utakaoupata zaidi ya kutulia kwanza, kuepuka hasira, kufikiria kwa kina maisha na mambo yake + ubinadamu, kisha uusikilize moyo na nafsi yako. Hapo lolote utakaloamua kutokana na haya utakuwa sahihi kama hautapingana nayo.
 
hujitambui kiaina!!!!!!
uvumilivu unaosemwa ni ule wa maswala ya kawaida ya kijamii yanayoudhi, k.m. kuchelewa kurudi home, kulewa, kuzozana, uchochezi wa wanandugu n.k.

Masuala yanayohusu faragha yamefungamanishwa kwa wanandoa tu, ikitokea mmoja kati yao akaenda kinyume na kanuni hii hakutakuwa na laumu ya maana ndoa ikivunjika.
 
1. Kutembea nje ya ndoa au niseme usaliti, uwe wa kihisia au kimwili. Hili kwangu halina mjadala kabisa. If I find out you're two-timing on me, we are through. I call it one strike and you're out policy.

2. Physical violence. Ukinitwanga na frying pan kichwani au ukinitandika chupa ya Balimi usoni, kutakuwa hakuna tena ndoa hapo. Kwa sababu nita-swing for the fences, and if I connect, lights out. Lose-lose situation there.

3. Vices nyingine kama ulevi usio wa kupindukia, uvutaji sigara, matumizi mabaya ya pesa, uvivu wa kufanya kazi, kuvaa nguo kama hoochie mama, kutumia lugha chafu chafu, uchafu wa mwili na mazingira, ili mradi tu hazijavuka mipaka na kuwa kero ambazo siwezi kuzivumilia, nadhani ni vitu ambayo mimi na yeye tunaweza kukaa chini, tukavijadili, na kukubaliana namna ya kuvikabili na kuvirekebisha.

Lakini watu tumetofautiana. Wapo ambao hata wachitiwe namna gani bado watang'ang'ana kupigania ndoa zao. Wengine hata wawe wananyanyaswa kiasi gani, iwe kihisia au kwa kupigwa bado tu watang'ang'ana.

Well, siwezi kuwakosoa sana maana huo ni uamuzi wao. Lakini huwa siamini katika upuuzi wa kudhani kuwa kwa vile tu mtu uko kwenye ndoa na kwa vile labda mna watoto basi ndo uendelee kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga.

Kufanya hivyo (kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga) ni kuwa mpuuzi na mjinga. Hata kama kuna watoto, hiyo haina maana ndo ushikwe mateka katika ndoa yenye kila aina ya manyanyaso.

Inafika wakati mtu unaweka mguu wako chini, unachora mstari na kusema 'sasa basi, imetosha'. Unasepa unaenda kuendelea na maisha yako.
 
Napenda kufahamishwa ni mambo gani ya kuvumilia katika ndoa na yapi sio ya kuvumilia?(Yaani yapi yakitokea ndoa ife? na yapi ya kusamehe)
Unawezaje kumsamehe na kuendelea kuishi na mwanaume ambaye amezaa nje ya ndoa tayari akiwa katika ndoa?
Inamaanisha nini watu wanaposema vumilia katika ndoa kwa ajili ya watoto?, eti usiwe m-binafsi kujiangalia mwenyewe.
Na maneno kama simama upiganie ndoa yako. napiganaje?
Je ni mwanamke pekee ndo anahitajika kupigania ndoa yake?

Follow your heart, kama una uwezo wa kiuchumi anza mbele. Kwasababu atacheat tuu..Kama mume ndio tegemeo la familia yako then ng'ang'ania.
 
1. Kutembea nje ya ndoa au niseme usaliti, uwe wa kihisia au kimwili. Hili kwangu halina mjadala kabisa. If I find out you're two-timing on me, we are through. I call it one strike and you're out policy.

2. Physical violence. Ukinitwanga na frying pan kichwani au ukinitandika chupa ya Balimi usoni, kutakuwa hakuna tena ndoa hapo. Kwa sababu nita-swing for the fences, and if I connect, lights out. Lose-lose situation there.

3. Vices nyingine kama ulevi usio wa kupindukia, uvutaji sigara, matumizi mabaya ya pesa, uvivu wa kufanya kazi, kuvaa nguo kama hoochie mama, kutumia lugha chafu chafu, uchafu wa mwili na mazingira, ili mradi tu hazijavuka mipaka na kuwa kero ambazo siwezi kuzivumilia, nadhani ni vitu ambayo mimi na yeye tunaweza kukaa chini, tukavijadili, na kukubaliana namna ya kuvikabili na kuvirekebisha.

Lakini watu tumetofautiana. Wapo ambao hata wachitiwe namna gani bado watang'ang'ana kupigania ndoa zao. Wengine hata wawe wananyanyaswa kiasi gani, iwe kihisia au kwa kupigwa bado tu watang'ang'ana.

Well, siwezi kuwakosoa sana maana huo ni uamuzi wao. Lakini huwa siamini katika upuuzi wa kudhani kuwa kwa vile tu mtu uko kwenye ndoa na kwa vile labda mna watoto basi ndo uendelee kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga.

Kufanya hivyo (kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga) ni kuwa mpuuzi na mjinga. Hata kama kuna watoto, hiyo haina maana ndo ushikwe mateka katika ndoa yenye kila aina ya manyanyaso.

Inafika wakati mtu unaweka mguu wako chini, unachora mstari na kusema 'sasa badi, imetosha'. Unasepa unaenda kuendelea na maisha yako.

Umenigusa sana...
 
yote ni decision yako wewe binafsi..wewe ndo utajiwekea kitu gani ni cha kuvumilia na nini hautaweza au hauwezi once you have that unaweza kuendelea na maisha vizuri ila usipo make a decision utakuwa stuck..try everythng,ila usiwe stuck, decision yako ndio itamake foundation ya muendelezo wa maisha yako in love affairs, watoto wanaweza kukua vizuri tu depending na malezi yako ila wasipo kuwa wanamuona baba mara kwa mara ina matatizo yake na kiukweli wanaume wakiachwa na watoto wakachukuliwa wengi wao dont care anymore
 
Kila mtu na moyo wake au hisia zake,na wanaume wengi wanafanya siri jambo hili la kuzaa nje ya ndoa na kama kakwambia basi hakuwa na nia ya kukupoteza tofauti ungesikia kwa watu wengine ,we vumilia tena chukua kabisa ulee maisha yaende ,I swear to u mumeo atakupenda zaidi ya hapo .
 
1. Kutembea nje ya ndoa au niseme usaliti, uwe wa kihisia au kimwili. Hili kwangu halina mjadala kabisa. If I find out you're two-timing on me, we are through. I call it one strike and you're out policy.

2. Physical violence. Ukinitwanga na frying pan kichwani au ukinitandika chupa ya Balimi usoni, kutakuwa hakuna tena ndoa hapo. Kwa sababu nita-swing for the fences, and if I connect, lights out. Lose-lose situation there.

3. Vices nyingine kama ulevi usio wa kupindukia, uvutaji sigara, matumizi mabaya ya pesa, uvivu wa kufanya kazi, kuvaa nguo kama hoochie mama, kutumia lugha chafu chafu, uchafu wa mwili na mazingira, ili mradi tu hazijavuka mipaka na kuwa kero ambazo siwezi kuzivumilia, nadhani ni vitu ambayo mimi na yeye tunaweza kukaa chini, tukavijadili, na kukubaliana namna ya kuvikabili na kuvirekebisha.

Lakini watu tumetofautiana. Wapo ambao hata wachitiwe namna gani bado watang'ang'ana kupigania ndoa zao. Wengine hata wawe wananyanyaswa kiasi gani, iwe kihisia au kwa kupigwa bado tu watang'ang'ana.

Well, siwezi kuwakosoa sana maana huo ni uamuzi wao. Lakini huwa siamini katika upuuzi wa kudhani kuwa kwa vile tu mtu uko kwenye ndoa na kwa vile labda mna watoto basi ndo uendelee kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga.

Kufanya hivyo (kuvumilia kila aina ya upuuzi na ujinga) ni kuwa mpuuzi na mjinga. Hata kama kuna watoto, hiyo haina maana ndo ushikwe mateka katika ndoa yenye kila aina ya manyanyaso.

Inafika wakati mtu unaweka mguu wako chini, unachora mstari na kusema 'sasa badi, imetosha'. Unasepa unaenda kuendelea na maisha yako.

Nashukuru sababu ninavyowaza tunawaza wengi..
 
hakuna kisichoweza kuvumilika katika ndoa.kila kitu kinavumilika na ndoa huwa haifi.hata sisi tunaokupa ushauri tunavumilia hivyo hivyo kwenye ndoa.
 
hujitambui kiaina!!!!!!
uvumilivu unaosemwa ni ule wa maswala ya kawaida ya kijamii yanayoudhi, k.m. kuchelewa kurudi home, kulewa, kuzozana, uchochezi wa wanandugu n.k.

Masuala yanayohusu faragha yamefungamanishwa kwa wanandoa tu, ikitokea mmoja kati yao akaenda kinyume na kanuni hii hakutakuwa na laumu ya maana ndoa ikivunjika.

Mpuuzi mkubwa wewe!
Wewe ndio hujitambui, kutaka kuvunja ndoa za watu ndio nini sasa????
 
Napenda kufahamishwa ni mambo gani ya kuvumilia katika ndoa na yapi sio ya kuvumilia?(Yaani yapi yakitokea ndoa ife? na yapi ya kusamehe)
Unawezaje kumsamehe na kuendelea kuishi na mwanaume ambaye amezaa nje ya ndoa tayari akiwa katika ndoa?
Inamaanisha nini watu wanaposema vumilia katika ndoa kwa ajili ya watoto?, eti usiwe m-binafsi kujiangalia mwenyewe.
Na maneno kama simama upiganie ndoa yako. napiganaje?
Je ni mwanamke pekee ndo anahitajika kupigania ndoa yake?

Ningekushauri usitoe maamuzi ukiwa na jazba!
 
unaeza mwaya kuishi na mwanaume aliyezaa nje ya ndoa, inauma sana lkn unasahau na maisha yanasonga, ilimradi km mwenyewe kaomba msamaha na kajirekebisha..

hata ukisema uondoke utaacha wangapi, unaweza kukuta huyo mwingine si malaya lkn ana tabia zingine mbaya zaidi au akawa malaya zaidi ya uliye nae sasa.

pili vumilia tu kwa ajil ya watt wako, ujue ukiondoka hapo ndio unampa mwenzio nafasi ya kuja hapo kuwa mama na mwishowe wanao walelewe na mama wa kambo..

ila ukiona machungu yamekuzidi sana waweza na wewe kurevenge na kuwa na kidumu chako kinakuliwaza huko nje ila ndoa huvunji na nyumbani huondoki.....siku hizi wanawake hatuondokagi bana hasa km mmejenga pamoja, mmezaa..tafuta furaha popote lkn baki hapo hapo
 
Mahusiano yako tofauti na kila case ni tofauti kutegemeana na mazingira na tabia za wahusika. Cha msingi ni kutafakari mwenyewe kwanza nini kimetokea na why kimetokea. Je athari zake ni nini? Je hali inaweza kurekebishwa na kusamehe. Position ya mwenzako ni nini. Option ulizonazo ni zipi? Na mengine mengi. Kama vipi ni pm email yako nikutumie guide itakayo kuwezesha kufikia uamuzi.
 
Mtoa mada kuwa mvumilivu na usome hiki kisa kilichotokea mbele ya macho yangu

Jamaa yangu wa karibu sana alikuwa na mke ambae waliishi kwa upendo mkubwa sana kwa muda wa miaka 4 ,maisha yaliendelea kama kawaida lakini jamaa yangu huyu kuna kitu hakukijua kwa mkewe ambacho ni usaliti ambao mkewe alikuwa anaufanya kwa siri sana

Kama ilivyo ada jamaa yangu alikuja kumfumania siku moja tena ndani ya nyumba yake mwenyewe

Jamaa yangu alipanga kumuacha mkewe lakini kabla ya kufanya hivyo aliamua kwenda kumtaarifu baba yake.Baada ya kumpa baba yake hizi taarifa baba yake alimuambia kuwa kama ana uhakika mwanamke ambae atakuja kumuoa hata msaliti kama huyu,jamaa yangu alisema ana uhakika.Baba yake alimuuliza huo uhakika kama alikua nao wakati anamuoa huyu wa sasa na akasema ni kweli alikuwa na uhakika,baba yake akamuambia ni kitu gani kimetokea hadi akasalitiwa jamaa yangu hakuwa na jibu

Baba yake akamuambia kuwa kuna wakati unaweza kukosewa na ukasamehe tu bila ya kujiuliza sana kwani maisha ndivyo yalivyo na inawezekana jamaa yangu akawa huyu tunaezungumza nae sio baba yake halisi kwani huenda mama yake alifanya mambo ya hovyo nyakati hizo,Jamaa yangu kusikia hivyo aling'aka na kusema kuwa mama yake hawezi kufanya hivyo,baba yake akamuuliza kuwa kama akithibitisha hilo atafanya nini jamaa yangu akasema kuwa kama mama yake nae alikuwa au anafanya uhuni basi hatamuacha mkewe kwasababu anamuamini sana mama yake

Basi baba yake alimuambia jumapili dadazake na jamaa yangu watakuwepo nyumbani kwani watakuja kusalimia kutoka huko walikoolewa na mama yake atakuwepo na akamuagiza aje tu asubuhi na akija wakiwa sebuleni yeye na baba yake ajidai kuwa ameanguka na kuzimia ili awe anasikiliza kitakachokuwa kinaendelea

Kama kawaida jumapili ilifika na jamaa yangu alikwenda na aliniomba niende nae na alinijulisha kila kitu,tulifika na tuliwakuta wote kama baba yake na jamaa alivyosema na baada ya kusalimiana nao walikwenda jikoni kuandaa chai na sisi yaani mimi,jamaa yangu na baba yake jamaa yangu walituacha sebuleni

Baada ya nuda baba yake jamaa yangu alimuambia jamaa yangu kuwa huu ni wakati muafaka wa tukio kwani kuna mtu ameshamuandaa wakuja kufanya jambo,basi jamaa yangu alilala chini na baba yake jamaa yangu aliwaita dada zake na mama yake jamaa yangu kwa hamaki kuwa jamaa yangu amepatwa na tatizo,kama kawaida ya wanawake walikuja kwa hamaki na kuanza kuhaha bila majibu.Kiukweli nilijikaza sana nisicheke kwani ilikuwa kama tunacheza muvi

Baba yake na jamaa yangu alisema ngoja amfuate mzee mmoja ambae huwa anamfanyia mambo yake ambae huwa anaishi jirani sana na nyumbani pale,basi baba yake na jamaa yangu alikwenda na bila kupoteza muda yule mzee alikuja na kuanza kumtibu jamaa yangu kwa geresha tu kwani ishu alikuwa anaijua na baada ya nuda alisema kuwa mizimu ja kwao na baba yake ilikuwa imekasirika kidogo lakini ameipoza na dawa pekee ni mtu ambae ni msafi [ambae hajafanya ngono nje ya ndoa kwa muda wa wiki moja uliopita] akamguse jamaa yangu kichwani na fahamu zitamrejea,kumbuka hiulo linafanyika mimi nipo pamoja na jamaa yangu aliyejidai kuzimia pamoja na dada zake wawili ambao wameolewa na mama yake jamaa yangu

Basi yule mzee "mtaalam' alianza kumuita dada yake jamaa yangu akamguse jamaa yangu akagoma,akamuita wa pili akagoma kisha akamuita mama yake jamaa yangu nae akagoma kisha akaitwa baba yake na jamaa yangu na akaenda kumshika kichwani na jamaa yangu akainuka

Yule mzee akamuagiza mambo ya kufanya ili asirudiwe na ile kadhia mambo ambayo kiuhalisia yalikuwa ni geresha tu na yule mtaalam aliondoka na dada na mama ya jamaa yangu walirudi kwenye mambo yao ya kuandaa chai

Unajua nini kilitokea ni kuwa jamaa yangu hata chai ilimshinda na tuliondoka,jamaa yangu alisema kumbe haya mambo yanafanyika na hata mama yangu na utu uzima wake anafanya? Aliamua kutokumuacha mkewe na sasa wana watoto wawili na ndoa yao haikuwahi kupata mgogoro tena


Ninachotaka kukuambia hapa ni kuwa kwenye maisha hakuna jambo baya au zuri ila wewe mwenyewe ndie unaeamua kulipa tafsiri

Hilo lako unaweza kuliona kuwa ni baya au la kawaida tu na ukaendelea na maisha yako na huyo bwana au ukaamua kuachana nae

Lakini kuachana nae sio gerentii ya kuja kumpata ambae ametulia,kama unaachana nae achana nae kwasababu nyingine na sio uaminifu kwani huenda ukaja kumkosa muaminifu na ukajilaumu sana kumuacha huyo ambae tayari mmeshaishi kwa muda na mnafahamiana kwa mambo mengi!
 
'kwenye maisha hakuna jambo baya au zuri ila wewe mwenyewe ndie unaeamua kulipa tafsiri'.. well said eiyer
 
Back
Top Bottom